Monday, May 27, 2013

WALAANI KUWAJENGEA CHUKI WANAHABARI

Moja ya nyumba zulizochomwa moto


Nathan Mtega,Songea
 BAADHI ya waandishi wa habari na wadau wa habari mkoani Ruvuma wamelaani vitendo vya ukatili dhidi ya waandishi wa habari vilivyofanywa na baadhi ya wakazi wa mkoa wa Mtwara ikiiwa ni kuwazuia kufanya kazi yao kwa uhuru ya kuhabarisha ikiwa  pamoja na kuchoma moto nyumba na gari la mwandishi wa habari wa kituo cvha utangazaji cha taifa.
 Wakizungumza na Radio One Stereo kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi hao wa mjini Songea walisema kuwa vitendo vya namna hiyo mbali ya kuhatarisha usalama wa waandishi wa habari lakini pia vimekuwa vikiwaathiri kisaikolojia na kiuchumi kwa sababu wanajengeka na hofu ya usalama wao.
 Akizungumza mmoja wa wadau wa habari Anthon Ngonyani mkazi wa mjini Songea alisema kuwa waandishi wa habari ni miongoni mwa watu muhimu katika jamii kwa sababu mchango wao ni chachu ya maendeleo ya jamii nzima na kwa maslahi ya taifa  zaidi hivyo kila mmoja ana wajibu wa kujali mchango wao na siyo kuwadhoofisha kwa namna yoyote.
Naye Mwandishi wa habari Juma Nyumayo alisema kuwa habari ni hewa ya oksijeni ya maendeleo ya nchi na ili waweze kuelekea kufanya shughuli zao kwa usahihi ikiwa watapata ushirikiano wa waandishi wa habari na jamii husika  na kitendo cha baadhi ya wananchi hao kuwazuia au kuwadhuru waandishi kufanya kazi yao ni sawa na kumziba mtu kupata hewa hiyo muhimu.
Aidha hivi karibuni kumezuka tabia ya baadhi ya viongozi wa vyama vya kisiasa kuwashambulia kwa maneno waandishi wa habari wa baadhi ya vyombo vya habari jambo ambalo linapandikiza chuki baina ya wananchi na waandishi wa habari na kusababisha baadhi yao kushambuliwa au kutishwa.
 Akizungumza mmoja wa viongozi wa dini mjini Songea ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa ni vyema mamlaka husika zikaona umhimu wa kuzuia vitendo hivyo visiendelee kujitokeza kwa kuziba mianya ya kutokea badala ya kusubiri vitokee ndipo hatua zichukuliwe na vikiachwa utageuka utamaduni wa kuwadhuru.

Mwisho.




No comments:

Post a Comment