Wednesday, February 3, 2016

Narudi tena katika Blogu,

Ama kweli, teknolojia  imekuwa kwa kasi kubwa.
Facebook, tweeter, na whatsApp viliniondoa kwa muda mtefu hapa.
hata hivyo nimeamua kurudi tena na kuendelea kupashana habari kama hobby.
Awali ya yote habari za mwaka mpya 2016. Kwa watanzania tunamshukuru mungu, maana serikali ya awamu ya tano ya Rais,  Dkt. John Pombea Magufuli, inaendelea kwa kasi kutumbua kila aina ya majipu, hata kama ni jipu chungu litatumbuliwa tu maana falsafa hapa ni ile ya HAPA KAZI TU! Elimu bure watoto wengi wameandikishwa madarasa ya awali na la kwanza. Sekondari ndiyo usiseme , Kumbe kweli umasikini na michango lukuki ya kuchangia elimu ilikuwa si kero tu bali kikwazo cha kusomesha watoto kwa wazazi na walezi waliowengi. Asante Dkt. Magufuli.
Mpaka siku nyingine tupo pamoja.

Thursday, February 6, 2014

SABUNI INAYODAIWA KUREJESHA UBIKIRA YAPIGWA "STOP"

WANAWAKE wameshauriwa kuacha kutumia sabuni za kunawia sehemu za siri ambazo hudaiwa kurejesha ubikira kwani zina madhara makubwa ikiwemo kusababisha kansa ya shingo ya kizazi.

Mkaguzi wa Dawa na Mfamasia wa Manispaa ya Dodoma Daria Mwanuka alisema hayo mwishoni mwa wiki katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi wakati wa uteketezaji dawa, vipodozi na vyakula visivyofaa kwa matumizi ya binadamu.

Kazi hiyo ilifanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Kanda ya Kati. Alisema kumekuwa na sabuni mbalimbali ikiwamo Kaisiki ambapo wanaoziuza wanadai zimekuwa zikisababisha bikira iliyopotea kurudi kitu ambacho si kweli.

“Sabuni hizo zinapunguza tu majimaji yaliyo sehemu za siri za mwanamke jambo ambalo husababisha wakati wa kufanya mapenzi mwanaume kupata ugumu kwenye muingiliano kwa vile mwili unakuwa umekataliwa kutoa maji na hivyo kuleta michubuko kitu ambacho ni hatari hasa wenye maambukizi ya magonjwa,” alisema.

Alisema michubuko inapotokea ni rahisi mwanamke kuambukizwa magonjwa ya zinaa hata virusi vya Ukimwi. Mtaalamu huyo alisema sabuni hizo zinatengeneza hali fulani ukeni lakini haiwezi kurejesha hali ya maumbile iliyopotea.

Alisema wanaotumia sabuni hizo wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa na hata kupata saratani ya shingo ya uzazi kwani kemikali zinazotumika katika kutengeneza sabuni hizo zina athari kubwa kiafya.

Alisema ni vyema wanawake wakatambua thamani yao na kuachana na matumizi ya sabuni hizo ambazo hazina manufaa yoyote na badala yake zimekuwa na madhara makubwa kwao.

Kwa upande wake, Fredrick Luyangi , Mkaguzi wa dawa kutoka TFDA alisema matumizi ya sabuni hizo huleta athari kubwa mwilini na wakati mwingine kutengeneza kansa taratibu bila mhusika kufahamu.

Alisema sabuni hizo husababisha kansa ya kizazi na kubainisha sabuni hizo licha ya kupigwa marufuku zimekuwa zikiuzwa kwenye maduka ya vipodozi.

Alisema mara nyingi kwenye operesheni zinazofanyika zimekuwa zikiondolewa sokoni lakini hata hivyo zimekuwa zikiingizwa kwa wingi hali inayofanya zoezi la kudhibiti kuwa gumu.

Alisema ni muhimu kwa wanawake kuacha matumizi ya sabuni hizo ambazo zina madhara makubwa sana kwao kwani zikikosa wanunuzi zitaondoka sokoni.
Source: Habari Leo

Tuesday, January 21, 2014

HABARI KATIKA MITANDAO YA KIJAMII



Mkurugenzi wa Demashonews Hamza Juma (Kushoto) akisikiliza maelezo toka kwa Mkurugenzi wa Jamii ya WanaRuvuma, Juma Nyumayo kuhusu mikakati ya kuwahabarisha wananchi kwa kutumia mitandao ya kijamii hivi karibuni.
 

Tuesday, January 14, 2014

MUFTI AWATAKA WAISLAMU KUACHA KULALAMIKA

SHEKHE Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba, ametaka Waislamu kuacha kulalamika, kwamba Wakristo wamekuwa wakipewa upendeleo, badala yake watumie fursa wanazopata kuondokana na malalamiko hayo. 

Akizungumza katika maadhimisho ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW), yaliyofanyika kitaifa mkoani Kigoma jana, Mufti Simba alisema chanzo cha malalamiko hayo ni Waislamu kushindwa kujitolea katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Akitoa mfano, alisema Waislamu wanapaswa kupeleka watoto wao kusoma elimu zote mbili na kuwaandaa kushika nafasi za kiutendaji ambazo wanalalamikia kuwa zimetolewa kwa upendeleo kwa Wakristo.

Alisema hata katika kukamata maeneo ya uwekezaji, Waislamu wamebaki nyuma kutokana na kushindwa kujitolea kuchangia fedha za kutosha za kuanzisha miradi ya maendeleo kwa ajili ya kuimarisha dini na kuendesha maisha yao.

“Msilalamike, tunisheni mifuko katika misikitini yenu muwe na fedha za kutosha zitakazokuwa kichocheo cha ninyi kushiriki katika shughuli muhimu za kiuchumi. Kosa ni lenu, msilalamikie Wakristo hawana tatizo hata kidogo katika hilo,” alisema Mufti Simba.

Madaraka misikitini Mjumbe wa Baraza la Ulamaa la Taifa, Ally Mkoyogore, alitaka Waislamu kuongeza bidii katika elimu na uchumi, badala ya kutumia muda mwingi kupigania madaraka misikitini.

Alisema kurudi nyuma kwa Waislamu, kunasababishwa nao wenyewe kushindwa kufuata maadili na misingi ya dini yao, badala yake wanagombea uongozi misikitini kwa ajili ya maslahi binafsi.

Maadhimisho hayo ya Maulid yalihudhuriwa na viongozi wa dini kutoka mikoa mbalimbali nchini, mashekhe kutoka Burundi huku Serikali ikiwakilishwa na Mkuu wa Mkoa Kigoma, Issa Machibya.

Mshikamano Akizungumza katika mkesha wa Maulid usiku wa kuamkia jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Rais mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alitaka Watanzania kujenga mshikamano kwa kusikilizana na kuvumiliana, kwa lengo la kudumisha tunu ya amani na utulivu iliyodumu kwa miaka mingi sasa nchini.

Katika salamu zake za siku hiyo, Alhaji Mwinyi alisema dini zote ukiwamo Uislamu, hazikatazi waumini kushirikiana katika masuala mbalimbali, hivyo ni wajibu wa kila upande kuusikiliza mwingine.

“Nchi zinaijua Tanzania kuwa kisiwa cha amani kisicho na utofauti wa dini, kabila wala rangi. Sote ni ndugu wamoja, tunapaswa kuendelea kuishi kwa usalama na amani.

“Pale inapotokea hali ya kutofautiana, tukae pamoja na kuzungumza ili tufikie mwafaka na si kugombana,” alisema Mwinyi.

Alisema Mtume aliongoza dini kwa kuhubiri mshikamano, kupenda wengine na kuthamini utu na si vurugu kama ambavyo wengine wanadhani.

Akimkaribisha Mwinyi kutoa salamu hizo, Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salumu, alisema amani na utulivu nchini ndio ujumbe wa sherehe hizo na kukumbusha Watanzania kuishi kwa umoja na kuwa watu wa Taifa moja lisilo na uvunjifu wa amani.

Kutokana na umuhimu huo, Shekhe Alhad alisema ndiyo maana sherehe hizo zikapewa kaulimbiu ya ‘Uislamu ni amani kwa wote’ lengo likiwa kukumbusha wanaofikiri kuwa misingi ya dini hiyo ni vurugu na kuhatarisha usalama au kujenga uadui kwa watu wengine.

Katiba mpya Shekhe Alhad pia alimpongeza tena Rais Kikwete kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa mchakato wa Katiba mpya ambao hivi karibuni utaingia katika hatua ya uundwaji wa Bunge Maalumu.

“Kama ni safari basi tayari mchakato wa Katiba umevuka Nungwi na karibu unaingia bandarini. Ni jambo la kumpongeza kwa sababu si mataifa yote yangeweza kufika hadi hapa tulipo bila vurugu, ila sisi tumeweza na hata pale palipotokea changamoto fulani, alikabiliana nazo,” alisema Shekhe Salum.

Alisema ni vema Watanzania wazidi kumwombea kiongozi huyo ili akamilishe salama mchakato huo na kumalizia muda wa uongozi na kumkabidhi mtu mwingine kuongoza Taifa. Miongoni mwa wageni waliokuwepo ni Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia. 

source: jumamtanda Blog

Monday, January 13, 2014

USIPITWE NA SOMO TOKA KWA SOPHIE LUCAS, SOMA HAPA

  1. Katika kijiji cha Matare wilaya ya
  2. Mugumu Serengeti, bwana
  3. Wambura alikamatwa kwa kesi ya
    kusingiziwa na kuhukumiwa kwenda
    jela miaka mitatu.
  4. Huku nyuma akiacha mke na
    watoto wanne waliokuwa
    wanasoma. Hukumu hiyo ilimtesa
    sana kichwa chake, alitamani kila
    mtu anayemhisi kuwa ana makosa...
    aingie katika moyo wake na
    kuupata ukweli.
    Alilia na umaskini wake, lambda
    angepata wakili mzuri angeweza
    kumtetea, kumkosa wakili
    kukahalalisha kifungo hicho!!
    Alikwenda gerezani huku akiumia
    sana rohoni. Aliyaanza maisha
    mapya kwa shida sana, akawa
    mnyonge kila mara na mwili
    ukapoteza afya kiujumla.
    Huko gerezani alifanikiwa kupata
    rafiki aliyekuwa na cheo ama
    jukumu la uzikaji wa wafungwa
    hasahasa ambao hawakuwa na
    ndugu ama ambao ndugu zao huwa
    hawajitokezi pale gerezani.
    Mzikaji alijaribu sana kumtia nguvu
    Wambura na kumwaminisha kuwa
    hiyo ilikuwa hatua tu ya maisha
    anapaswa kuizoea na siku moja
    ukweli utajulikana tu! Bwana
    Wambura maneno ya mzikaji
    hayakumuingia kabisa.. alizidi
    kunyong’onyea.
    “Siwezi kuvumilia kukaa gerezani
    miaka mitatu…..kama unajali kilio
    changu nisaidie nitoroke kwa
    namna yoyote ile ndugu yangu!!”
    Wambura alimsihi mzikaji.
    SIKU MOJA mzikaji akamwambia
    Wambura kuwa msaada
    umepatikana. Lakini yataka moyo!!
    “Nipo tayari kwa lolote ilimradi tu
    nitoke humu!!” alijibu kwa msisitizo
    huku akimtegea sikio mzikaji.
    “Msaada pekee wa kukutorosha
    humu ndani ni kwa njia ya jeneza…
    yaani mfungwa akifa mimi
    nakuunganisha naye kwenye
    jenerza…..” akashusha pumzi kisha
    akaendelea “Wewe ukisikia kengere
    ya msiba, njoo mara moja kwenye
    chumba cha maiti, utakuta tayari
    sanduku liko katikati ya chumba
    linakuwa halijafungwa, funua
    kifunioko ingia ndani yake ulale
    pembeni ya maiti kwani sanduku
    huwa kubwa la kutosha kila aina ya
    maiti na hata miili miwili inaingia.
    Kisha nitakuja na kulipigilia
    misumari. Baada ya muda
    tutalipakia kwenye gari na kutoka
    kwenda nje ya gereza makaburini
    nikiongozana na baadhi ya
    wafungwa na maaskari magereza.
    Tutakuzika huko lakini baada ya
    dakika 20 hadi 30 nitarudi
    kukufukua. Hautaweza kushindwa
    kupumua kwa dakika hizo, utatoka
    ukiwa huru.”
    JAPOKUWA wazo lilikuwa zuri lakini
    lilimtisha sana Wambura. Hata
    hivyo akaona afadhali afanye hivyo
    kuliko kukaa gerezani miaka mitatu
    bila kosa.
    Siku moja akasikia kengere ya
    msiba. Akafanya kama
    alivyoelekezwa na mzikaji. Akaenda
    na kuingia chumba cha maiti. Kweli
    akalikuta sanduku, akiwa na hofu
    kuu akaingia na kulala pembeni ya
    maiti iliyokuwepo. Mara akasikia
    mtu ameingia na kulipigilia
    msumari sanduku. Muda mfupi
    baadaye sanduku likainuliwa na
    kuwekwa kwenye gari.
    Gari ikatoka nje ya gereza hadi
    makaburini. Sanduku likashushwa
    na kuwekwa kaburini na kuanza
    kufukiwa.
    Wambura alijitahidi sana kuvumilia
    japo hofu ilizidi kutanda.
    Alimtegemea sana mzikaji na
    alianza kumuona mkombozi wa
    maisha yake.
    Kama alivyoambiwa, akasubiri
    dakika kumi, ishirini.. zikapita
    kimya!!
    Dakika thelathini kimya. Joto nalo
    likazidi kuongezeka.
    “Nitavumilia hadi afike…”
    alijisemea kisha akajiongezea kauli
    ya ujasiri.
    “Kama nilitakiwa kuishi gerezani
    miaka mitatu kivipi dakika kadhaa
    za hapa kaburini”
    KWA kuwa alishakaa gerezani kwa
    muda kiasi akatamani kujua
    aliyekufa ni nani… ni kwewli
    aliogopa kuitazama maiti lakini
    aliona kama inatisha zaidi ikiwa
    imefunikwa vile kuliko ikiwa wazi.
    Akaifunua upande wa usoni… Kwa
    kuwa kulikuwa na giza nene
    alikodoa sana macho kuitazama.
    LAHAULA!!! MACHO YAKAKUTANA
    NA SURA YA MZIKAJI!!!
    MZIKAJI ALIKUWA AMEKUFA NA
    AMEZIKWA NA AHADI ZAKE ZA
    UKOMBOZI!!
    ________________
    FUNZO::
    Usimtegemee sana mwanadamu
    katika maisha yako, kwanza ni
    dhambi!!
    Pili mwanadamu anakumbana na
    vikwazo kama unavyokumbana
    navyo wewe hadi kumwendea yeye.
    Hivyo kumpatia maisha yako ni
    kuzidi kuyaweka hatarini zaidi!!
    Umeonewa umesingiziwa
    unanyanyaswa….. mwachie Mungu
    afanye maamuzi…
    _______________
    Haya mzikaji aliyetegemea
    atamfukua naye ni maiti…… tazama
    mateso atakayoyapata hadi kufa
    kwake…..
    Bila shaka atatamani kurudi
    gerezani kwa miaka mingine kumi
    lakini haitawezekana tena!!!