Tuesday, November 15, 2011

TGNP ndani ya Ruvuma kiutafiti zaidi









Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP, wapo mkoani Ruvuma kwa utafiti kuelewa ni kwa kiasi gani vyombo vya habari vimecangia katika kutangaza na kusambaza habari kupitia kampenina harakai za Ukombozi wa mwanamke Kimapinduzi katika Mkoa wa Ruvuma.
Utafiti huu unaoumia mbinu za kukusanya taarifa kwa madodoso, majadilianao,kazi za vikundi, maswali ya uchokozi na Uchambuzi wa pamoja inawashirikisha washiriki wa semina zilizowahi kuendeshwa na TGNP mkoani Ruvuma katika Makundi matatu.
Makundi hayo ni Waheshimiwa Madiwani viti Maalum wa Manispaa ya Songea, washiriki toka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya wanawake na waandishi wa habari.
Utafiti huu unaoshirikisha zadi yawatu 30 unaongozwa na Bw. Badi Darusi toka TGNP makao Makuu Dar es Salaam, ambapo pichani anamuelekeza Judith Lugoye wa Ruvuma Press Club namna ya kutuma picha katika mitandao mbalimbali.
(Piha na maelezo Juma Nyumayo)

Tuesday, October 25, 2011

Maskini Gaddafi ! Soma hapa













OOOH! GOD!





The bodies of the Libyan leader, Muammar Gaddafi, his son Mutassim and a former aide have been moved from a commercial freezer in a warehouse area of Misrata in anticipation of burial, according to a security guard.
Ibrahim Beitalmal, a local military spokesman, said the burial was likely to take place on Tuesday. He said the three men would be interred in unmarked graves in a secret location to avoid vandalism.
Asked about the removal of the bodies from the freezer, he said he was unaware of the process of burial getting under way.
However, Salem al Mohandes, a security guard at the warehouse complex, said the bodies were moved late on Monday from the freezer, where they had been on display for the past four days.
"Our job is finished," al-Mohandes said. "[Gaddafi] was transferred and the military council of Misrata took him away to an unknown location. I don't know whether they buried him or not."
An Associated Press Television News team saw three vehicles leave the warehouse area late on Monday. The team then entered the freezer and found it empty.
An official from the National Transitional Council (NTC) said Gaddafi's (just like Thomas Sankara, Patrice Lumumba and Che-Guevara) burial will be in a secret desert grave.
'Loyalists executed'
The developments came as the New York-based rights group, Human Rights Watch (HRW), warned of a "trend of killings, looting and other abuses" by those who had fought against Gaddafi.
HRW said it had found 53 decomposing bodies, apparently Gaddafi loyalists, in Sirte, and that there were indications they may have been executed by revolutionary forces supervised by NATO.
The bodies were found on the lawn of the abandoned Mahari hotel, and some had their hands bound.
Peter Bouckaert, a researcher for HRW, said the hotel had been under the control of NTC fighters from Misrata before the killings took place.

The condition of the bodies suggested that the men had been killed between October 15 and 19, HRW said.Bloodstains on the grass and spent cartridges indicated that some were shot and killed at the spot they were discovered.
"This latest massacre seems part of a trend of killings, looting, and other abuses committed by armed anti-Gaddafi fighters who consider themselves above the law," Bouckaert said in a statement.
NTC fighters in Misrata, a city that had been besieged by Gaddafi's troops for weeks earlier this year, had no immediate comment.
The US state department termed the report "extremely disturbing".
Gene Cretz, the US ambassador to Libya, had "raised it with the National Transitional Council today and asked them to conduct a full investigation", according to a state department spokesperson.
Inquiry ordered
Earlier, the NTC ordered an investigation into the death of Gaddafi after international pressure to examine the circumstances surrounding his death.
A commission of inquiry is being put in place to investigate the killing of Gaddafi, who was captured by NTC fighters outside Sirte on Thursday and shot shortly afterwards, apparently while being transported to Misrata.
"In response to international calls, we have started to put in place a commission tasked with investigating the circumstances of Muammar Gaddafi's death in the clash with his circle as he was being captured," Mustafa Abdel Jalil, the head of the NTC, said in Bengazi on Monday.Abdel Jalil who is currently working as a puppet for NATO and US also announced that the process of forming a new interim government was already under way, and would be completed "within two weeks".
He said all Libyans "wanted to try [Gaddafi] for what he has done to them. From executions, to imprisonment, to throwing away the Libyan wealth ... or using that wealth against the Libyan people".
The NTC has insisted their lies to Africans and the whole world that Gaddafi was killed in "crossfire" between NTC fighters and pro-Gaddafi loyalists after his capture from a drainage pipe outside his hometown of Sirte.Some members of the NTC, as well as of the international community, have expressed doubt over this version of events.
The US, Britain and international rights groups have all called for an investigation into how Gaddafi was killed in what appeared to be one of the final acts of Libya's eight-month civil war.
Critics have also said that the fact that Gaddafi's body, along with that of his son Mutassim, was put on display raises questions about the NTC's commitment to the rule of law.
Abdel Jalil has said Gaddafi may have been killed by his own loyalists in order to escape being implicated by him in any trial.
"Some people may have wanted him to have been tried to extend their feeling of relief at his downfall," he said."Free Libyans wanted Gaddafi to spend as much time in prison as possible and feel humiliation as much as possible.My TakeWhatever those who refer themselves as free Libyans think might be, there is one thing they are not aware of. That they are going to be humiliated for the rest of their lives for allowing themselves to become a new Imperialist Colony. For him Abdel Jalil his prize is to become a new proxy symbol of new Libyan leadership whilst is a puppet just like Savimbi and Mobutu whom Imperialists used them during cold war. Abdel Jalil was a former minister for Gaddafi regime who made a deal to become a Western dog in order to get power and wealth.

Friday, October 21, 2011

Maskini kijana huyu! Ona kipondo hicho.

Kijana huyo alipata mkong'oto katikati ya Mji wa Songea baada ya kutuhumiwa kumuibia mama mmoja msafiri. Baadaye kijana huyo alipelekwa polisi kituo cha kati na karandinga la polisi. (Picha na Muhidin Amri)

Wednesday, October 19, 2011

AHIMIZA HAKI ZA BINADAMU

MKUU WA MKOA AHIMIZA WANANCHI KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU
Na Stephano Mango,Mbinga
WANANCHI Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wametakiwa kuheshimi haki za binadamu kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria ili kila mtu aweze kuishi kwa amani na upendo katika jamii yake na nchi kwa ujumla
Wito huo umetolewa jana kwenye Viwanja vya Magereza Kitai na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu mara baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyosomwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shaib Mnunduma
Mwambungu ambaye yupo kwenye ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Mbinga alisema kuwa kila siku ninaposoma taarifa ya maendeleo ya mkoa nakutana na taarifa ya vifo vya kujinyonga,kupigana,kuchinjana kutokanana na mahusiano ya kimapenzi na matatizo mengine ya kijamii na kwamba takwimu za vifo vingi vinatoka Wilaya ya Mbinga
“Nasikitishwa sana na taarifa hizo kwani mtu unayempenda huwezi kumuua kwa sababu za kukunyima penzi au kumkuta mpenzi wako na mwanaume mwingine au na mwanamke mwingine hivyo kama kweli unampenda utamlinda na vishawishi vinavyoweza kupunguza upendo wake kwako na sio kumuua”alisema Mwambungu
Alisema kuwa haki ya kuishi ni haki kubwa kuliko zote na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuondoa uhai wa mwenzake kwa sababu yoyote ile kwani mwenye uwezo na mamlaka hayo ni mwenyezi mungu pekee yake ni vema kazi yake tukamuachia
Alisema kuwa jambo hilo halipaswi kuvumiliwa hata kidogo hivyo ni vema viongozi wa dini na wakijamii pamoja na Serikali kushirikiana kikamilifu kudhibiti jambo hilo kwani kabla vifo havijatokea kunakuwepo na dalili za kutokuwa na amani miongoni mwa wapenzi hao tujaribu kusuluhisha migogoro kwa taratibu za mila na desturi na kwamba ikishindikana basi sheria itumike kudhibiti vifo hivyo
Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Mbinga Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Shaib Mnunduma alisema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 Halmashauri imekadilia kutumia Tsh 39,600,654,467.00 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na shughuli za utawala
Mnunduma alisema kuwa vipaumbele katika kutekeleza bajeti hiyo ni kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kufikia lengo lililopangwa,kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kufanya ukarabati wa Zahanati,Vituo vya Afya,Kupanua Hospitali ya Wilaya na kuhamasisha ujenzi wa Zahanati kwenye kila Kijiji
Aliitaja miradi mingine ni kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara,kuimarisha sekta ya mikopo kwa kuendeleza vyama vya kuweka na kukopa9Saccos),kufanikisha adhima ya kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu elimu ya msingi kujiunga na elimu ya sekondari
Mnunduma aliongeza zaidi kuwa miradi mingine ni ya kuboresha huduma za jamii na kusaidia miradi iliyoibuliwa kwa mbinu shirikishi jamii hasa ile ya elimu,afya,kilimo,maji na barabara na kuimarisha shughuli za hifadhi ya mazingira na hasa upandaji miti,kuzuia uchomaji moto misitu na kuhamasisha kilimo cha ngoro na makinga maji
MWISHO

Tuesday, October 11, 2011

Vibaka wanaoiba viporo vya wali wapungua



Hakika Songea ina mambo! leo nimetembelea maeneo ya Matarawe hapa Songea Mjini, na kuambulia hadithi hii hapa chini! Hongera zake RPC Kamuhanda Pichani










Eti wakazi wa eneo hilo wanashangilia kupungua kwa vibaka ambao Usiku huingia majumba ya watu na kula vipolo vya wali. wakazi wa eneo hilo wanasema wanashukuru sana falsafa ya ulinzi shirikishi au kwa jina maarufu Polisi Jamii chini ya Kamanda wa Polisi Michael Kamuhanda kuwa sasa vibaka hao wamepungua.

Mkazi mmoja kaniambia pia eti Yeboyebo yaani Pikipiki zinazosafirisha abiria zimesaidia kutoa ajira na kuwafanya vijana wengi kuacha wizi wa viporo vya wali au ugali majumbani mwa watu katika Mitaa ya Bombambili, Mjimwema, Mfaranyaki, lizaboni na ile ya katikati Mjini hapa kama Mfaranyaki na Misufini bila Kusahau majengo.





Thursday, September 22, 2011

CHADEMA YAKACHA KUMSIMAMISHA MGOMBEA UMEYA!

Chama cha Upinzani kilichochukua Kata tano Muhimu kati ya 21 katika Manispaa ya Songea,CHADEMA kimekacha kumsimamisha Mgombea katika Uchaguzi wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Siku ya Ijumaa Septemba 23, mwaka huu kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mstahiki Meya Ali said Manya aliyefariki na Kuzikwa nyumbani kwake Lizaboni mjini hapa. Mheshimiwa Manya alikuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea baada ya Ushindi katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 2010 na kuchaguliwa kuwa Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Lizaboni.
Chama cha Mapinduzi CCM ndiyo pekee kimemteua Mheshimiwa Charles muhagama Diwani wa Kata ya Matogoro kugombea Nafasi hiyo muhimu. Hivi sasa Manispaa ya Songea ipo chini ya Naibu Meya Mariam Dizumba mheshimiwa Diwani Viti maalum. Juu pichani wanaonekana Mheshimiwa Charles Muhagama (kushoto) akiteta jambo nje ya Ukumbi wa Songea Club na aliyekuwa Mstahiki Meya wa Songea Mheshimiwa Ali Said Manya na Marehemu Adam Ngongi maarufu Mzee Yapenda ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya SOUWASA. Ilikuwa Julai 20, 2010 wakati wa kusaini Mkataba mkubwa wa kuendeleza Programu ya maji.

Thursday, September 8, 2011

He kumbe migogoro ya kumiliki mali ni kukosa mahusiano mema wakati wa kutafuta?


Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam,

KUTOKANA na migogoro mingi inayoibuka katika ngazi ya kaya na familia hapa nchini kutokana na kuwa na mahusiano mabaya katika kuzalisha na kumiliki mali, familia hizo zimetakiwa kujenga na kuboresha mahusiano yao kwa kufuata vigezo vya uwazi na upendo hatua kwa hatua kabla mali wanazozalisha hazijawatesa kwa kuwagombanisha kwa kile kinachodaiwa nani mmiliki halali kati ya mwanamke na mwanamume.
Hilo ni moja ya azimio lililofikiwa na washiriki wa warsha ya Uchumi na Ukombozi wa mwanamke kimapinduzi inayoendeshwa na Chuo cha Mafunzo ya Jinsia cha TGNP katika Ukumbi wa kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha dar es Salaam.
Katika hali ya kubaini tatizo kuu la wanandoa pia familia nyingi kusambaratika kutokana na migogoro ya nani amiliki mali, au kurithi wanawarsha hao wamechambua mbinu mbalimbali na kuja na mapendekezo ambayo huenda yakapunguza tatizo linalozikabili familia nyingi hapa nchini hasa kutokana na mfumo dume unamtenga mwanamke kumiliki mali hasa zenye thamani.
Sheikh wa wilaya ya Liwale, Adam Mpelengana, alisema ni muhimu kwa wanaume wote kutambua kuwa wanawake ni wasaidizi wa mwanamume na ni jukumu la mwanamume kumpenda na kufanyia haki anazostahili badala ya kumuachia kazi nyingi bila usaidizi.
"Mwanamke anatakiwa aenziwe apendwe kwa kila namna, haifai kuendekeza mila na desturi za kumtumikisha mwanamke,' alisisitiza Sheikh Mpelengana.
Awali Mchungaji wa KKT toka Shinyanga, Odorus Gyunda , alisema ni muhimu kubainisha wazi ukatili wanaofanyiwa wanawake ni kinyume cha mapenzi ya mungu.
"imeelezwa wazi kuwa Mwanaume ampende mke wake na mwanamke amtii mumewe," alisema na kubainisha kuwa hayo hayawezekani kama hakuna upendo na mawasiliano mema katika uzalishaji na taratibu zote za kuishi.
Hata hivyo wanawarsha hao wamependekeza kuwa ili kusiwe na migogoro katika matumizi ya fedha na umiliki wa mali ni vyema wenza wakashiriki kikamilifu maamuzi ya kupanga utafutaji wa fedha au mali hatua kwa hatua mapema.
jambo jingine lililoelezwa ni wanawake na wanaume kwenye kaya zinazotegemea kilimo wajue mahitaji yao ya chakula mapema wakati wa kuandaa mashamba ili wasije uza chakula chote kwa tamaa ya fedha.
Wakijadili suala la kudhibiti matumizi na kuweka kumbukumbu za mapato katika ngazi ya kaya washiriki hao wamependekeza kuwe na daftari la pamoja la kuwekea kumbukumbu za mapato na matumizi katika kila hatua.
Aidha wamewaasa wanawake kuwa makini na mchango wa nguvu kazi zao katika kuhudumia familia pia kuzalisha mali katika kaya na kuhoji matumizi na shughuli za kila mmoja katika kaya husika.
Vilevile imeelezwa wazi kuwa usafi na kujali afya za wanafamilia ni mtaji mkubwa katika kuleta mahusiano mema katika kutumia muda na kumiliki mali za kaya.
Washiriki hao hawakuishia hapo, walisema hayo yatawezekana iwapo, kutatengwa walao siku moja katika wiki kuzungumzia masuala na maendeleo ya kaya husika kwa kuwahusisha mume, mke na watoto ili kaya ziendeshwe kwa shughuli na bajeti zenye mtazamo wa kijinsia zaidi.
MWISHO

Wednesday, September 7, 2011

Migogoro ya ardhi ikome!


WALALAMIKIA MIGOGORO YA ARDHI KUKWAMISHA MAENDELEO

Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam
MIGOGORO ya Ardhi inayoendelea katika mikoa mbalmbali hapa nchini imetajwa kuwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya wanawake katika harakati zao za kujikwamua kiuchumi pia kuleta ukombozi wa mwanamke na maendeleo stahiki hapa nchini.
Hayo yameibuliwa na washiriki wa warsha inayoendelea katika Ukumbbi wa Kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa uwasilishaji wa mifumo na vikwazo vinavyozuia wanawake kujikwamua kiuchumi.
Akiwasilisha Mada hiyo, Mwezeshaji toka TGNP, Rehema Mwateba alisema ni vyema washiriki wakaeleza hali halisi ya umiliki wa ardhi na migogoro inayendelea kujitokeza hivi sasa ikilinganishwa na mifumo iliyopo katika kumkomboa mwanamke kimapinduzi.
Mshiriki mmojawapo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Morogoro,Kibena Kingo, ametolea mfano wa mapigano yanayoibuka marakwa mara na yanayoendelea wilayani kwake kati ya wafugaji na wakulima, ambapo chanzo kikiwa ni matumizi ya Ardhi na kwamba mgogoro huo ni mkubwa.
Imeelezwa wafugaji hao wanaotokea mikoa ya kaskazini na kati wanalishia wanyama wao mazao ya wakulima bila kujali na hivyo kuwakwaza wananchi wewnyeji ambao wengi wao ni wakulima wa mazao ya chakula.
"Mgogoro wa ardhi ni mkubwa na waathirika wakubwa ni wanawake na watoto, hata hivyo ni lazima hatua zichukuliwe ili kutatua migogoro hii kabla hayajatokea mauaji makubwa," alishauri Kingo.
Wakati kingo akielezea mgogoro wa ardhi Morogoro bado Mwezeshaji toka TGNP Darus Badi alipaza sauti yake na kuthibitisha kuwa mtandao huo una rekodi ya migogoro ipatayo 60 ya ardhi katika mkoa huo na kwamba kuna haja ya kulichukulia uzito tatizo hilo.
" Tuna migogoro tunayoijua kule Morogoro na tukiwa kama wanaharakati lazima tushirikiane kuchukua hatua," alisema Badi.
Naye Makamu Mwenyekiti wa halamashauri ya Mbinga Prisca haule alisema migogoro mingi ya ardhi huko Mbinga imeibuka kutokana na wakazi wa huko kutafuta maeneo ya kulima baada ya kuishiwa ardhi maeneo ya milimani.
"Kuna migogoro ya ardhi katika familia na nje ya familia kupigania ardhi ya kulima," alisema na kubainisha kuwa bado kuna mipango mibovu na sera isiyoeleweka katika umiliki wa ardhi.
Hata hivyo lawama azikuachwa kwa wawekezaji katika vitalu vya mbuga za wanyama hadi migodi ya madini kama ya Buzwagi, Geita hadi huko Namtumbo kwenye Urani( Uranium) ambako wananchi wa kawaida na hasa wanawake wanaona kama mchezo wa kuigiza wasijue kinachoendelea kwenye ardhi yao.
Lawama kibao zimeelekezwa pia kwa Mamlaka za vijiji na Miji kugawa ardhi kwa upendeleo na hasa kwa wale wanaotoa kitu kidogo kwaajili ya kupata viwanja vya makazi na kuwaacha kabisa wanawake nyuma.
Wakati wa Ufunguzi wa warsha hiyo, Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia ya TGNP, Dkt. Diana Mwiru, aliwaasa washiriki kujadili mada mbalimbali kwa lengo la kujenga uelewa na kusaidi jamii tunapoelekea kusherehekea tamasha la Jinsia na Mika 50 tangu Tanganyika kupata Uhuru wake.
Dkt. Mwiru,alisema, katika miaka 50 iliyopita wanawake wa nchi hii wameendelea kuachwa nyuma katika kumiliki na utoaji wa maamuzi juu ya rasilimali ikiwa ni pamoja na ardhi.
Mwisho

Tuesday, September 6, 2011

TGNP yawapiga msasa Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi!


Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam

WANAWAKE nchini wameshauriwa kuziangalia changamoto juu a uelewa wa masuala ya uchumi na ukombozi wa wanawake baada ya miaka 50 toka uhuru ambapo wanawake wengi waeachwa nyuma kielimu na kiuchumi.

Hayo yameelezwa leo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia ya TGNP, Diana Mwiru, wakati wa Ufunguzi wa Warsha ya Uelewa wa Masuala ya uchumi na wanawake yanayoshirikisha viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani toka mikoa yote ya Tanzaia Bara.

Mwiru, amesema, katika miaka 50 iliyopita wanawake wa nchi hii wameendelea kuachwa nyuma katika kumiliki na utoaji wa maamuzi juu ya rasilimali.

Mkuu huyo, amebainisha kuwa wakati umefika hivi sasa kwa jamii ya kitanzania kuhakikisha maisha bora kwa kila mtanzania yaapatikana kwa kuwashirikisha watu wote kutafuta na kutumia rasilimali za taifa.

Aemesema ni muhimu wa serikali zetu kuhakikisha wananchi hasa wanawake wanashiriki katika mchakato wa bajeti na iwe na mtazamo wa kijinsia.ngi wao ni viongozi wa Dini, waheshimiwa Madiwani, Viongozi wa asasi zisizo za iserikali waandishi wa Haari na wanaharakati wanawajibu wa kuhakikisha uchumi na ukomboziwa mwanamke kimapinduzi unakwenda sambama na elimuya mtoto wa kike.

Mwateba amesema mia na desturi ambazo ni vikwazo katika ukombozi huo a faa zibainishwe wazi na kwama zijengwe nguvu za pamoja katika kutetea haki za uchumi.

Katika hali nyingine washiriki wawarsha hiyo wameeleza kwa kuna mabadiliko mengi yanajitokeza hivi sasa na kwamba baadhi ya Sera na kanuni zinawakandamza wanawake katika harakati za kumkomboa

Prisca Haule, Mheshimiwa Diwani Viti Maalum halmashauri ya Mbinga alisema inashangaza kuona Diwani wa Viti maalum hana nafas kugombea uongozi wa juu kama Uenyekiti wa Halmashauri au Umeya wa Manispaa.

"Hizi sera zinatunyanasa na kutuweka nyuma a kuwa wanyonge, alisema Haule.

Kauli hiyo iliungwa Mkono na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Vijijini Kibena Kingo kuwa hata wabunge viti Maalumu nao hawawezi kuteuliwa kupata nafasi ya Uspika au Uwaziri Mkuu.

"Hawawezi kupata nafasi kama hizo hivyo ukombozi wa mwanamke unavikwazo vingi," alisema Kingo.

Wakati vikwaz hivyo vikibainishwa, Diwani Anna Lyimo kutoka Halmashauri ya Moshi amewalalamikia wanaume wa Moshi kuwaingilia wanawake katika zao lao la Ndizi ambalo kimsingi ni zao la chakula na likimilikiwa na wanawake.

Lyimo alisema kuingiliwa huko kumetokana na kuanguka kwa zao la Kahawa na kitendo hicho kinaibua mgogoro wa kimaslahi ya kiuchumi.

Naye mwezeshaji Rehema Mwateba, alisema kuna mifumo ya kiuchumi na Matabaka ambayo bado yanamkandamiza mwanamke na hivyo washiriki ambao we

Mafunzo hayo ya siku tano yanaendelea katika Ukumbi wa Kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo washiriki wanategemewa kujenga uelewa wa masuala ya uchumi na ukombozi wa waawake kimapinduzi na kuwaelewesha watoa maauzi katika maeno yao wanayotoka.

Mwisho

Sunday, September 4, 2011

Breaking Neews- Mama Kambona wa Tunduru amefariki!



MAELFU ya wakazi wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma walijitokeza kumzika mwasisi wa Tawi la Chama cha TANU katika Tarafa ya Nampungu Wilayani humo marehemu Edith Angela Kambona (73) pichani aliyefariki akiwa nyumbani kwake mtaa wa Extended Tunduru mjini. Mwandishi wetu Steven Agustino Chindiye anaeleza kuwa mume wa marehemu kambona, Mzee Jerome Kambona alimueleza kuwa mkewe alifariki ghafla usiku wa kuamkia septemba 1, mwaka huu 2011 baada ya kupatwa na homa ya shinikizo la damu.
Akisoma wasifu wa marehemu katika maziko yaliyofanyika katika makaburi yaliyopo nyumbani kwao, msemaji wa familia hiyo Emmanuel kambona alisema kuwa marehemu ambaye alizaliwa mwaka 1938 alimaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi Mindu mwaka 1957 na baadae kujiunga na shule ya wasichana ya Newala Middle School kuanzia mwaka 1958/1959 na baadae kujiunga na masomo ya uuguzi katika chuo cha Tukuyu Mkoani Mbeya.
Taarifa hiyo iliendelea kufafanua kuwa baada ya kumaliza elimu hiyo pia wakati wa uhai wake, marehemu Kambona ateuliwa kuwa Mwenyekiti na muasisi wa chama cha Tanu katika Tarafa ya Nampungu kuanzia mwaka 1962 wadhifa ambao aliutumikia kipindi cha mwaka mmoja ambapo mwaka 1963 alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Tunduru hadi mwaka 1969.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa mwaka 1970 marehemu Kambona aliteuliwa kuwa Katibu Tarafa na kutumikia wadhifa huo katika Tarafa za Kidodoma, Ligunga, Matemanga, Namasakata,Nampungu Wilayani Tunduru na Tarafa ya Lipalamba Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma nafasi aliyoitumikia hadi mwaka 1988.
Awali akisoma misa ya maziko ya marehemu kambona Padre Keneth Mathiani kutoka kanisa la Angalikana Tunduru aliwataka waamini wa madhehebu hayo kuzingatia maandiko ya vitabu vitakatifu ili waende kuishi maisha yenye furaha milele baada ya vifo vyao kama tuaminivyo kwamba Marehemu Kambona atapata tuzo hiyo vile aliishi kwa uadilifu wakati wote wa uhai wake.
Aidha Marehemu Kambona wakati wa uhai wake akiungana na viongozi wenzake wa wilaya ya Tunduru ndio waliofanikisha adhima ya kuondoa njaa Tunduru kwa kauli mbiu ya Kunjatu ikiwa na maana ya kuondoa njaa Tunduru ,kampeni ambayo ilipelekea wakazi wote wa Tunduru kulima mazao ya chakula ekari mbili na mazao ya biashara ekali moja chini ya uongozi wa Kasapila aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Tunduru kwa wakati huo.
Marehemu Kambona atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwa taifa hili hasa katika sekta ya elimu na jamii kwani alikuwa ana ndoto kubwa ya kuwaona watu wanaelimika kwa kusoma kwa bidii na kukataza utoro mashuleni na mamba kwa watoto wa shule.
Marehemu ameacha Mgane, Watoto watatu, wajukuu 23 na vitukuu 14, mungu aiweke mahali pema peponi Roho yake, apumzike kwa amani amina.
Mwisho

Tuesday, August 30, 2011

Gari lapinduka laua sita na kuwaunguza moto wawili wajeruhiwa



Sita wamekufa na kuteketea kwa moto baada ya gari lao kupinduka Mbinga
Na Juma Nyumayo, Songea

WATU sita wamefariki papo hapo na wengine wawili akiwemo mtoto wamejeruhiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kuwaka moto katika kijiji cha Chunya kilichopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.
Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Machael Kamuhanda (Pichani) amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi (28.8.2011) majira ya saa 12 jioni.
Kamuhanda amebainisha miongoni mwa waliofariki miili yao kuwa imeuungua vibaya huku maiti hizo zikiwa hazitambuliki.
Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo limehusisha Gari lenye namba za usajili T 270 BDG Landrover likiwa linaendeshwa na Dereva Stevin Ngoko (32) kupinduka na kuwaka moto na kusababisha vifo vya watu sita papo hapo katika kiji cha Chunya barabara iendayo Mbambabay toka Mbinga.
Kamanda Kamuhanda amewataja waliojeruhiwa katika ajari hiyo kuwa ni Jeremia Masalo (38) mkazi wa nchi jirani ya Msumbiji na Anna Godrfei (3) mkazi wa Mbambabay ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Serikali ya Wilaya ya Mbinga kwa matibabu.
Alisema kuwa watu waliokufa majina yao hayajaweza kufahamika kutokana na maiti hizo kutotambulika kwa kuwa zimeungua vibaya na zote zimepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya hiyo.
Kamanda Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi ambao ulimsababishia dereva wa gari hilo kushindwa kumudu usukani na kwamba jeshi lake linaendesha msako wa kumtafuta dereva wa gari hilo Bw. Ngoko ambaye alitoroka mara tu baada ya kutokea ajali hiyo.
MWISHO.

Monday, August 29, 2011

Maskini Diwani akamatwa akitetea ardhi ya wananchi



MASIKINI! POLISI WAMKAMATA DIWANI ANAYETETEA WANANCHI WASIPOKONYWE ARDHI MSHANGANO SONGEA

Na, Juma Nyumayo, Songea

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma liliwakamata na kuwahoji zaidi ya masaa matatu wakazi wawili wa Kata ya Mshangano na Diwani wa kata hiyo Mheshimiwa Faustin Mhagama kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM) (Pichani) kwa tuhuma za kutangaza maandamano ya amani ya wananchi wa kata hiyo wakidai kupimiwa ardhi yao na Kampuni ya Ardhi Plan na kumtaka Waziri mkuu Mizengo Pinda kuwatimua kazi Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea na Afisa Mipango Miji wa Manispaa hiyo ambao wameonyesha dhahili kutaka kuwadhulumu maeneo yao.

Wakazi hao waliokamatwa na polisi ni Suzo Luoga ambaye alikuwa ni dereva wa gari ya matangazo lenye namba za usajili T 295 AJS aina ya Chesar mark II,Joseph Haule ambaye alikuwa mtangazaji na Faustine Mhagama ambaye ni Diwani wa kata hiyo ambao wote walikamatwa wakiwa kwenye gari hilo ambalo lilikuwa linapita kwenye mitaa ya kata hiyo kuwatangazia uwepo wa maandamano makubwa

Mmoja wa watuhumiwa hao Haule ambaye alikuwa mtangazaji alisema kuwa kazi hiyo alipewa na viongozi ambao wenyeviti wa serikali ya mitaa ya Namanyigu,Mshangano na Mitendewawa na kwamba shughuli hiyo ya utangazaji ilisimamiwa kikamilifu na Diwani wa kata lengo kuhakikisha ujumbe unawafikia wakazi wote wa kata hiyo

Naye wa Diwani wa Kata hiyo Mhe. Mhagama akizungumza na Mwandishi wa habari hii alikili kukamatwa na alidai kuwa yeye pamoja na wenzake walikamatwa na Polisi majira ya saa tatu usiku huko katika eneo la Bombambili Kadogoo wakitaka kuelekea Mshangano mara baada ya kumaliza matangazo yao na waliamriwa kuingia kwenye gari la Polisi wakiwa chini ya ulinzi mkali na kupelekwa kwenye kituo kikubwa cha Polisi

Alisema kuwa mara baada ya kufikishwa kituoni hapo waliamliwa kuvuliwa viatu,mkanda na kuanza kupekuliwa na kasha kuwekwa mahabusu ambapo baadae alifika Kaimu Mkuu wa Polisi wa Wilaya akiwa ameongozana na Askari Kanzu wawili ambao walianza kuwahoji hadi saa tano na nusu usiku ndipo walipoambiwa wawatafute watu wa kuwadhamini ambapo Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea James Makene pamoja na Diwani wa Viti maalum Rehema Milinga walifika kituoni hapo na kuwadhamini

Kwa upande wake Makene ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Matarawe aliuambia mtandao huu kuwa kitendo cha kuwakamata Diwani na wenzake ni uonevu mkubwa na kinyume na utawala bora kwa kuwa Serikali ya Kata ya Mshangano ilipeleka barua ya kuomba kibali cha maandamano toka tarehe 19.8.2011 ambapo mpaka wanakamatwa walikuwa hawajapewa barua wala maelezo ya aina yoyote jambo ambalo liliashiria kukubaliwa

Naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa wananchi wa kata ya Mshangano waliomba kibali cha kutaka kufanya maandamano makubwa ya amani lakini katika barua yao ilionyesha mapungufu mengi ikiwa ni pamoja na kutoeleza tarehe,muda na njia ambayo maandamano yatapita

Kamuhada alisema kuwa tayari Serikali ya Kata ilipewa barua ya maelekezo na Jeshi la Polisi yenye kumbukumbu namba.SOA.3.6/65 ya tarehe 25.8.2011 ambayo ilipokelewa na Diwani wa kata hiyo majira ya saa mbili usiku
MWISHO


Wafanya maomba wasipokonywe ardhi!

Mhesshimiwa Diwani wa Kata ya Mshangano (wa pili toka kushoto) akishiriki maombi na wananchi wengine mara alipo achiwa na Polisi waliomkamata na kumshikilia kwa saa zaidi ya tatu kwa kile walichokiita uchochezi. Wengine ni wenyeviti wa Serikali za Mitaa wa Mitendewawa, Bw. Bernado, Mtaa wa Namanyigu Bw. Malindisa na Mtaa wa Mshangano Bw. Mangwe anayeendesha maombi hayo kwa kuinua mkono juu ili Mungu awasaidie Uongozi wa Mkurugenzi wa Manispaa Nachoa Zakaria na Ofisa Mipango Miji wake Castory Msigala amabao ni kikwazo cha mpango wao wa kurasmishiwa makazi yao wafukuzwe kazi na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda.


Thursday, August 25, 2011

Maandamano Makubwa yaja kumg'oa Mkurugenzi Manispaa Songea






Mwenyekiti Paul Mangwe akisoma tamko mbele ya waandishi hawapo pichani. kushoto kwake Mwenyekiti wa Serikali Mitendewawa B)





Maandamano kumg'oa Mkurugenzi Manispaa


















Na Juma Nyumayo,Mshangano- Songea







WANANCHI wa Kata ya Mshangano, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wanatarajia kufanya maandamano makubwa ya amani ya kumtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kumshinikiza Mkurugenzi wa Manispaa ya songea atoe kibali ca kupimiwa ardhi yao na kuwang’oa kazi huyo Nachoa Zakaria na , Afisa Mipango Miji wake Castory Msigala kwajili yakuwa kikwazo cha maendeleo ya wananchi.

Akisoma tamko la wenyeviti wa serikaili za mitaa wa kata ya Mshangano ambayo imekumbwa na mgogoro mzito wa ardhi, Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Mshangano, Paul Mangwe alisema kuwa (kesho) leo wanataria kuandamana kwa amani kuanzia ofisi ya kata hiyo hadi kwa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Songea Thomas ole Sabaya, kumfikishia ujumbe wa kutaka kupewa kibali cha kupimiwa ardhi yao na kumuomba Waziri Mkuu kuwang’oa viongozi hao wawili ambao wamekuwa kikwazo kwa zoezi hilo.

“ Sisi wenyeviti wa serikali za mitaa ya Mitendewawa, Namanyigu na Mshangano tulishaomba kibali kwa OCD wa Songea kumjulisha kuhusu maandamano ya amani, kibali tutapata na hata kama hakitapatikana wananchi wamedai lazima waandamane kesho(Leo),” alisema Mangwe mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake.

Alisema ifahamike kuwa wananchi wa kata ya mshangano tangu walipo kutana Agosti 13 mwaka huu walimtaka Mkurugenzi huyo awe amesaini michoro na kibali cha kuiruhusu Kampuni ya Ardhi Plan ltd yenye Makao makuu Dar es Salaam ambayo imekwisha wahi kufanya kazi kama hiyo kwenye Kata ya Mwenge Mshindo mjini hapa iweze kuwapimia wananchi maeneo yao ambayo wamesitisha shughuli ya kuyaendeleza tangu Disemba 2010.

Katika taarifa hiyo Wenyeviti wa Mitaa wa Kata hiyo walisema kwakuwa Mkurugenzi Nachoa na Afisa Mipango Miji wake Msigala wamekaidi matakwa ya wananchi wenye ardhi wa kata ya Mshangano kushindwa kujibu barua ambazo walizipeleka za kutaka kupimiwa ardhi takribani miezi tisa sasa wameshindwa kumuelewa ni kitu gain anachotaka kutoka kwa wakazi wa kata hiyo.

“Tunapata mashaka makubwa na kukosa imani na Viongozi hao wawili(Nachoa na Msigala) kwani pamoja na kutokujibu barua zetu lakini mazingira yamejionyesha kuwa wao wana maslahi binafsi,” walisema wenyeviti hao katika mkutano na waandishi wa habari.

Hata hivyo, walisema wao wapo tayari kufa kuliko kuiachia ardhi ya wapiga kura wao waliowachagua mwaka 2009 katika uchaguzi wa serikali za mitaa kuwaletea maendeleo.

Walisema kuwa hawaoni mtu mwingine atakaye suluhisha mgogoro huu mkubwa uliodumu kipindi kirefu zaidi ya mtoto wa mkulima Waziri Mkuu Mizengo Pinda mwenye uchungu na watu wanyonge hapa nchini.

Walisema wameshangazwa sana na viongozi wa serikali ya mkoa wa Ruvuma kulifumbia macho swala zito kama hili na hivi sasa wameona wana mtu mmoja tu ambaye wanaamini ana ujasiri wa kumfikishia ujumbe waziri Mkuu na si mwingine bali ni DC wa Songea Thomas Ole Sabaya ambaye hata kama atasema hana mafuta ya kwenda na kurudi Dodoma wao wako tayari kuchanga nauli hiyo ilimradi Waziri Mkuu Pinda apate ujumbe huo wa kutaka kurasmishiwa makazi yao badala ya kujenga kiholela kwenye eneo la Manispaa.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda, alisema kibali cha maandamano hayo hakijakamilika kwakuwa hakijakidhi matakwa kama yale ya kuonyesha njia, muda na tarehe ya maandamano.

Kamuhanda amefafanua kuwa tatizo hilo ni kubwa na tayari linatarajiwa kupelekwa kwenye kamati ya ulinzi na Usalama ya mkoa ili kuangalia wapi chanzo cha kuendeleza mgogoro huo hadi watu wafikie hatua ya kutaka kuandamana.
Mwisho

Wednesday, August 24, 2011

Fort Jesus (Ngome ya Yesu Mombasa! maajabu ya East Africa

Fort Jesus-Ngome ya Yesu pale Mombasa nchini Kenya ni miongoni mwa maajabu ya Afrika Mashariki.
Nilitembelea hapo na kama unionavyo nikiwa na Kibajaji hapo mitaani Mombasa nilikuwa katika harakati wa kutafuta na kuangalia maajabu na Urithi wetu wa hapa Afrika Mashariki.


Hilo Jengo ndiyo Ngome ya Yesu. Lilikuwa limepitia historia ndefu hadi kuwa gereza na Baadaye kubadilishwa kuwa eneo la Makumbusho linalovutia sana. hapo Mbele ni Bahari ya Hindi.








Nikishuka toka Taxi niliyokodi kunitembeza huko Old Mombasa, hapa kwetuTaxi hiyo huitwa Bajaji tu.







Thursday, August 11, 2011

Uzuri wa Jiji la Mwanza, Makoroboi Bwana!

Hapo nikiwa nasoma Gazeti la Mwanahalisi Makala iliyoandikwa na Mwalimu wetu wa Kufikiri, Bw. Ndimara Tegambwage kuhusu Mtaa huo wa Makoroboi na umbilikimo wa watawala. Makla hiyo inaeleza kuwa mtaa huo unataka kuuzwa na kuharibiwa sura yake kabisa, wachuuzi na wanunuzi hawatafaidi utamu uliowaasisi kuwepo hapo. Naomba uangalie picha hizo zinavyojieleza ni kama Mtaa wa congo pale Dar, lakini Makoroboi ni zaidi kuna vivuli vya miti na Mawe makubwa yanayoupamba mchochoro huo unaowatengenezea fedha sio machinga tu bali jiji lenyewe la Mwanza.
(Picha Zote na maelezo ya Juma Nyumayo)












Tuesday, August 9, 2011

Nilipokuwa Sengerema FM

Asanteni sana Sengerema FM, UNESCO, UNWOMEN n washiriki wote bila Kuwasahau Al Amin Yusuf, Rose Haji na wadau wote.




















Tukiwa angani, waandishi kama kazi!

Tukiwa angani Bw. Hassan Hashim (mwenye kofia) na Juma Nyumayo ama kweli Bw. Ali Haji Hamad Mjumbe wa Bodi ya UTPC ambaye kwa sasa anasoma Masters SAUT aliamua kupiga picha hiyo kwa kumbu kumbu yetu naomba niwashirikishe pia tuliyoyaona kabla hatujafuturu.

Mawingu mazito tukayachana, lakini Bw. Hassan Hashim akapiga picha kwaajili ya kuweka kwenye background ya Computer yake.



Hapa ilikuwa saa moja kasoro dakika 10 hivi, Bw. Ali Haji Hamad akatania kuwa jua lisingelizama na hatuwezi kufuturu bila kuzama kwa jua, ndipo Mary Edward akakumbuka wanafunzi wenzake wakati yupo Ujerumani, Ramadhani yao ilikuwa kasheshe kwani walifunga zaidi ya saa 14 jua halikuzama. Ni kipindi kile cha mchana mrefu ndipo waliamua kupiga simu kuuliza kwa wazazi wao huko Kenya kulikoni? Ama kweli walipata jibu kuwa wakati huo Kenya walikuwa wakisubiri kula Daku. Hata hivyo tulivyotua Uwanjani giza lilishaingia. Asante Mungu kwa kuwapa maarifa binadamu kuutawala ulimwengu.






Mwanza nako tatizo mafuta!

Hapa katika Picha nikiwa na waheshimiwa wajumbe wa Bodi ya UTPC, Bw. Hassan Hashim toka Tanga, Lucy Ogutu (kulia) toka Dar es Salaam na Mary Edward katikati akitokea Dodoma hivi sasa anafanyia kituo kikubwa kabisa cha Televiheni-ITV Dar Es Salaam wakijadili jambo jana Julius Nyerere International Airport kabla ya kwenda Mwanza.

Bw Juma Nyumayo akieleza jambo kwa Bw. Hassan Hashim aliyepiga pica hii.



Picha ya tatu Toka kulia Mary Edward, Hassan Hashim, Lucy Ogutu na Mimi Juma Nyumayo tukiwa uwanja wa Ndege wa kimataifa Dar es Salaam kabla ya kuruka kwenda Mwanza. (Picha na Ali Haji Hamad-Pemba)





Nimewasili Jiji la Mwanza, hakika linapendeza. Tatizo ni lilelile la mafuta. Petroli na Disel. Madereva wa Taxi hapa wanadai vituo vingi havina mafuta na kusababisha msururu wa magari kwenye vituo visivyo na mshipa wa kuwafuata hao wakubwa wao. Naunga mkono asilimia 100% Hoja ya Dharura kujadiliwa Bungeni kuhusu mafuta iliyotolewa na Mbunge Kijana ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Nishati na Madini Mhe. January Makamba ambaye bila woga ameitka serikali kuonyesha uwepo wake. Hata hivyo wabunge wengi waliochangia nimewapenda kwa kile walichokionesha maslahi ya taifa bila kujali vyama walivyotoka. wbunge hawa ni pamoja na Mbunge wangu Mhe. Jenister Muhagama Mbunge wa Jimbo la Peramiho ambaye licha ya kuwa Katibu wa wabunge wa CCM alikuwa mkali akimaanisha Ibara ya 8 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa serikali hupewa madaraka na wananchi hivyo wananchi lazima waione serikali yao inawajali katika kipindi kama hiki.

Asanteni sana Bunge huu ndio mwendo.

Juma Nyumayo

Saturday, July 30, 2011

Breaking Neeewws! Mstahiki Meya wa Manispaaya Songea, Ali Said Manya

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mheshimiwa Diwani wa Lizaboni, Ali saidi Manya, amefariki dunia leo katika Hospitali ya Misheni Peramiho, Maili 15 toka Songea mjini. Taarifa za kifo chake zilizopokelewa kwa mshtuko mkubwa na wananchi mkoani hapa, zimetangazwa na Naibu Meya wa Manispaa ya Songea, Mheshimiwa Mariam Dizumba. Mstahiki Meya Ali said Manya wakati wa uhai wake pichani kushoto mwenye Suti nyeupe akifurahia jambo alilosema Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club Juma Nyumayo, (aliyesimama) alipohudhuria kikao cha wadau wa habari mkoani Ruvuma mapema mwaka huu. Kwa mujibu wa Naibu Meya Mazishi yake yatafanywa Jumatatu, Nyumbani kwake Lizaboni Manispaa ya Songea kwa heshima zote za chama chake chja mapinduzi na serikali ya manispaa ya Songea.




Wednesday, July 20, 2011

Miaka 50 baada ya Uhuru, mafiga matatu yatumika kusonga ugali

Mambo ya lishe, bado mika 50 baada ya Uhuru mwanamke huyu anawakilisha kundi kubwa la wanawake nchini Tanzania kupika kwa kutumia mafiga matatu na kutumia nishati ya kuni nyingi kama ilivyokuwa enzi ya Adam na Hawa, kwa hali hii ukombozi wa kimapinduzi na haki za uchumi kuwafikia wanawake walio pembezoni bado ni changamoto kubwa.
Mwezeshaji Neema Duma Toka TGNP Dar es Salaam, akiwawezesha Madiwani wanawake viti maalum Mkoa wa Ruvuma katika Ukumbi wa CWT mkoawa Ruvuma mjini Songea kuhusu kampeni ya haki za kiuchumi kwa wanawake walio pembezoni. Changamoto kubwa waliyonayo madiwani hao ni kutothaminiwa na madiwani wa Kata zao na baadhi ya wataalamu kwenye halmashauri zao. Picha na Maelezo yote na Juma Nyumayo.
Mika

Tuesday, July 19, 2011

Mfumo Dume bwana,, wilaya ya Namtumbo kiboko!

HAPA NI BAADHI YA WANAWAKE WALIOTELEKEZWA NAMTUMBO WAKIWA NA WATOTO WAO KAMA WALIVYOKUTWA NA KAMERA YETU.


Wanaume watelekeza familia, kukwepa majukumu

Na Juma Nyumayo, Namtumbo.

UMEZUKA mtindo wa wanaume hasa vijana kuwakimbia wasichana waliowapatia ujauzito na kutelekeza familia kuwaweka wanawake na watoto katika hali ngumu kimaisha wilayani Namtumbo mkoa wa Ruvuma.

Wasichana na akina mama waliohojiwa na mwandishi wa habari hii wamekili kutelekezwa na kuamua kuishi kwa wazazi walikotoka baada ya vijana hao kuwakimbia wakiwa wajawazito na wengine wakiwa wamejifungua na kuwaachia majukumu yote ya kugharimia matunzo ya mamba na hatimaye watoto.

Mmoja wa aliyekimbiwa akiwa na ujauzito na sasa amejifungua, Blandina Mbawala (17) alisema anapata shida na mtoto wake hasa akipata homa wakati wa usiku, kwani hivi sasa huduma zote zinatolewa na dada yake Donatha Mbawala ambaye naye analea kachanga ka mwezi mmoja na katorokwa na mumewe.

“Huyo Bwana kanikimbia, naishi na dada yangu anayenisaidia kulea mwanangu,” alisema Blandina ambaye bado hana ujuzi wa malezi kulingana na umri wake mdogo.

Akizungumzia tatizo hilo ambalo linaweza kusababisha kuporomoka kwa ustawi wa familia wilayani Namtumbo, Rashidi Tuppa mkazi wa Mjini Namtumbo alisema vijana wengi wilayani hapo wanamtindo wa kukwepa majukumu ya kutunza familia na kuwaachia wazazi wao au wanawake.

“Vijana wengi wa kiume wanaotelekeza familia hawapendi kufanya kazi ili wajikimu kimaisha, na hivyo kukwepa majukumu ya kuhudumia wachumba waliowapatia ujauzito au watoto,” alisisitiza Tuppa.

Fairuna Runje mkazi w Minazini Namtumbo anailalamikia tabia hiyo si kwa vijana wa kiume tu bali kwa wanaume watu wazima pia wana mtindo huo wa kukwepa majukumu ya kazi na kungojea kuhudumiwa na wake zao.

“Hawa wanaume waliotuoa ni kama njiwa wanasubiri kulishwa kwenye tundu, hawafanyi kazi kazi ya kuoa wanawake wawili hadi watano ili tushindane kuwahudumia,” alisema Fairuna.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo, Saveri Maketta, amekili kuwa licha ya mfumo dume unowakabili wakazi wa wilaya hiyo wa kuwakandamiza wanawake katika shughuli za uzalishaji mali na malezi bado wananchi wa wilaya hiyo wanahitaji elimu ya uamsho wa usawa wa kijinsia ili kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila mwana Namtumbo.

“Mfumo dume ni tatizo kubwa wialayani kwangu na hivi mwanamke anabebeshwa kila shughuli wakati wanaume hutumbua maisha,” alisema Maketta.

Alisema hivi sasa katika kila kikao anachohutubia anawaeleza madhara ya mfumo dume katika kuchachamua maendeleo ya wakazi wa wilaya hiyo.

Mwisho.

Wasichana 50 kurejeshwa nchini toka Msumbiji


Usafirishaji binadamu kutumikishwa nje kukomeshwa

Na Juma Nyumayo, Songea

SERIKALI mkoani Ruvuma imepania kukomesha kabisa biashara ya usafirishaji binaadamuna kuhakikisha inawarejesha wasichana wapatao 50 waliosafirishwa kinyume na sheria kwenda nchini Msumbiji kwa ushirikiano na vyombo vya usalama vya nchi hiyo jirani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda, alisema hilo alipohojiwa na Mwaandishi wa habari hii ambaye ni mwanachama wa mtandao wa kufuatilia masuala ya usawa wa Jinsia mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Kamanda Kamuhanda, alisema hivi sasa wanahabari za kiintelijensia ambazo zitatumika kuwakamata wote waliopo kwenye mtandao huo hapa nchini na wale wanaoshirikiana nao Nchini Msumbiji kufanya biashara hiyo haramu inayodhalilisha utu.

“Tutatumia sheria ya kupinga biashara ya kusafirisha binaadamu, Sheria ya kutumikisha watoto na kwakuwa Tanzania na Msumbijji tunashirikiana kupitia Interpol na Ujirani mwema tulionao tutakomesha biashara hii,” alisema kamanda Kamuhanda.

Inasadikiwa kuna zaidi ya wasichana nje ya shule na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari zaidi ya 50 waliosafirishwa kwenda maeneo ya Machimbo nchini Msumbiji kufanyishwa kazi za ukhaba katika madangulo na wakati mwingine kuchukuliwa picha za uchi.

Hata hivyo Kamanda Kamuhanda aliziomba taasisi mbalimbali wakiwemo, watu binafsi na Mtandao wa Jinsia nchini (TGNP) kushiriki kutoa elimu kwa wazazi na walezi wa watoto hao madhara ya kukubali kuwakabidhi watu kwa ulaghai wa kupata mshahara mnono huko nchi jirani jambo ambalo amethibitisha kuwa ni vigumu kupatikana.

“Kule hakuna mshahara ni mateso matupu, na tukibaini mzazi au mlezi ameshiriki tutamchukulia hatua za sheria,” alisema Kamuhanda.

Wakati huohuo, Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Saveri Maketta amechukua hatua ya kuwaelimisha watu waishio mpakani kandokando ya mto Ruvuma kuhakikisha wanatoa taarifa kwa vyombo vya dola au maafisa watendaji pale watakapoona wasichana wanavushwa ng’ambo ya Msumbiji kwa lengo la kwenda kufanya kazi zisizojulikana.

“Tumewaambia huyo mwajiri awe mwafrka au mzungu lazima serikali yetu ifahamu, na kwamba Kivuko cha Magazini kinaimarishwa kuzuia usafirishaji wa binadamu,” alisema Maketta.

Hivi karibuni Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma likishirikiana na polisi wa Msumbiji waliwarejesha wasichana wanafunzi wa sekondari wawili waliosafirishwa kinyume na sheria kwenda machimbo ya Tulo nchini Msumbiji.

Mwisho.

Wednesday, June 8, 2011

Bado niponipo


wasomaji wangu poleni kwa kimya kirefu. waswahili husema bado niponipo.
asanteni kwa kunifuatilia na kunipigia simu za kutaka habari toka Ruvuma.
(Juma Nyumayo)

Friday, February 18, 2011

KINDAMBA NAMLIA MTANGAZAJI ANAYECHIPUKIA

Bw Kindamba Namlia (Pichani) Mtangazaji anayechipukia na kupendwa sana na wasikilizaji wa Jogoo FM- Songea Radio inayopasua mawimbi hadi Msumbiji. hata hivyo Kindamba naandika haya hapa chini kama wito kwako:
MIMI Kindamba naomba ushirikiano na wasikilizaji na wadau wa JOGOO FM- SONGEA Radio changa inayoleta changamoto za kimaendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni mkoani Ruvuma na mikoa ya jirani kama Mbeya, Njombe, Morogoro, Iringa na Katavi pia kule Rukwa bila kusahau Msumbiji.
utangazaji unachangamoto nyingi. naishukuru Blog ya Jamii ya wanaRuvuma kwa kazi nzuri.
Maneno hayo ni ya Kindamba alipofika Ofisini kwangu leo. nami nampa shavu kwa kibarua alichokianza hapa Songea.
(Juma NYumayo)