Tuesday, August 9, 2011

Tukiwa angani, waandishi kama kazi!

Tukiwa angani Bw. Hassan Hashim (mwenye kofia) na Juma Nyumayo ama kweli Bw. Ali Haji Hamad Mjumbe wa Bodi ya UTPC ambaye kwa sasa anasoma Masters SAUT aliamua kupiga picha hiyo kwa kumbu kumbu yetu naomba niwashirikishe pia tuliyoyaona kabla hatujafuturu.

Mawingu mazito tukayachana, lakini Bw. Hassan Hashim akapiga picha kwaajili ya kuweka kwenye background ya Computer yake.



Hapa ilikuwa saa moja kasoro dakika 10 hivi, Bw. Ali Haji Hamad akatania kuwa jua lisingelizama na hatuwezi kufuturu bila kuzama kwa jua, ndipo Mary Edward akakumbuka wanafunzi wenzake wakati yupo Ujerumani, Ramadhani yao ilikuwa kasheshe kwani walifunga zaidi ya saa 14 jua halikuzama. Ni kipindi kile cha mchana mrefu ndipo waliamua kupiga simu kuuliza kwa wazazi wao huko Kenya kulikoni? Ama kweli walipata jibu kuwa wakati huo Kenya walikuwa wakisubiri kula Daku. Hata hivyo tulivyotua Uwanjani giza lilishaingia. Asante Mungu kwa kuwapa maarifa binadamu kuutawala ulimwengu.






No comments:

Post a Comment