Thursday, December 26, 2013

Mwanahabari Mkongwe Adam Mzuza Nindi afunguka


Mwanahabari Mkongwe, Mwakilishi wa Radio Free Africa na Star TV Mkoani Ruvuma, Bwana Adam Mzuza Nindi,  Amefunguka na tathimini ya kazi katika Blogu 
Haya hapa chini ndiyo Maneno  yake na picha hapo juu alipost katika Blogu yake ya : www. songeahabari.blogspot.com
  
Uchunguzi wa Habari za kuwa wafaa wananchi ni mhimu sana ,Hebu Tuone sasa tuna Maliza Mwaka yepi mazuri yaliyo fanywa na Wandishi wa Habari na Yepi mabovu yaliyo fanywa na Waandishi wa Habari. Tujitathini wenyewe tusipige katumba kuonyesha vidole kwa wenzetu Pale tulipo kosea tuji sahihishe na Pale tulipo fanya vizuri tuboreshe zaidi Bado siku chache za kumaliza Mwaka lakini lazima Waandishi Tujipange Hapo ni Mwandishi Mwandamizi Juma Nyumayo (aliyesimama) akiwa na Mkongwe wa Habari Adam Mzuza Nindi wakitathiminji mwaka 2013

Wednesday, December 18, 2013

LAKE OIL LTD KUFUNGUA MAUZO YA MAFUTA SONGEA

Mtumishi wa lake Oil Ltd, Bw. Moses Clemency, akiwa mbele ya moja ya Pampu mpya za mafuta katika Kituo hicho kilichopo eneo la Manzese, Manispaa ya Songea.

KAMPUNI ya mafuta Lake Oil Ltd ya Dar es Salaam, imefungua Kituo cha mafuta Manispaa ya Songea.

Kituo hicho kilichopo Mkabala na Ofisi za Zimamoto na kuangaliana na Soko la Wakulima Manzese mjini hapa, kimebadili Sura ya eneo hilo kutokana na Ukarabati na kujenga paa kubwa katika Pampu mpya za mafuta aina ya Diesel, Petroli na ya taa.

Kwa Mujibu wa Meneja wa Kituo hicho, Bw. Daud Mmasa Sevuri, alisema kuwa huenda Alhamisi wiki hii wakaanza kuuza mafuta kwa bei nafuu wakilinganisha na vituo vingine mjini hapa.
"Alhamisi wiki hii tunatarajia kuanza kuuza mafuta hapa songea," alisema.

Ujio wa Kampuni ya Lake Oil Mkoani hapa, utaongeza ushindani wa Biashara ya mafuta ya mitambo na Gas kwa matumizi mbalimbali na kusaidia kusukuma maendeleo ya sekta ya kilimo, madini, usafiri na utoaji huduma.

Mkoa wa Ruvuma haujaunganishwa na Umeme Grid ya taifa hivyo kuufanya kutegemea zaidi mafuta.
Kilio kikubwa cha wakazi wa mkoa huu kitabaki kupata wakala wa kuuza mafuta ya ndege.
Angelipatikana wakala huyo Uwanja wa ndege ulioko eneo la Ruhuwiko manispaa ya Songea, wenye ubora wa kutua ndege mbalimbali isipokuwa Boeng,  ungeweza kutumika ipasavyo kwa abiria na kupunguza gharama ya nauli wanayolipa sasa kwa kutumia ndege ndogo.

Tuesday, December 17, 2013

WABUNGE 160 WA CCM WALIA NA MAWAZIRI MIZIGO

Ukumbi wa Bunge, Dodoma
                                  DODOMA/DAR ES SALAAM.                                                                                                                                                                                                                                                                    WABUNGE 160 wa CCM wamejiorodhesha kuomba kuitishwa kwa kikao cha Kamati ya Wabunge hao kwa lengo la kuwajadili mawaziri wanaotajwa kuwa mizigo.

Pia wabunge hao wanataka Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahaman Kinana naye awepo kwenye kikao hicho.
Mjumbe wa Kamati ya Uongozi wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Hussein Mussa Mzee, alimwambia mwandishi wetu kuwa wamepokea barua iliyoambatana na orodha ya majina ya wabunge zaidi ya 160 waliotia saini kutaka kuitishwa kwa kikao hicho.
“Hata kama wangesaini wabunge 10 tu tungeitisha kikao. Bahati nzuri walisaini zaidi ya 160, kwa hiyo kikao kitaitishwa kwa kuwa ni haki yao kikanuni kutaka kukutana,” alisema.
Alipoulizwa kwa nini kikao hicho hakikuitishwa ndani ya wiki moja ambao ndiyo muda wabunge hao walioutaka kabla ya Kamati Kuu ya CCM kukutana wikiendi iliyopita, Mzee alisema hiyo lilitokana na Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kutokuwapo bungeni.
Mzee alisema pia kikao hicho kilishindwa kufanyika mara ya kwanza kutokana na Kinana kuwa safarini Afrika Kusini ambako alihudhuria mazishi ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Hata hivyo, alisema hawezi kujua ni lini kikao hicho kitafanyika lakini aliahidi kuwa itakuwa mara baada ya Kinana kurejea nchini.
Wiki iliyopita, gazeti hili liliandika kuhusu wabunge wa CCM kujiorodhesha ili kushinikiza kufanyika kwa kikao hicho.
Chanzo kimoja cha kuaminika kilisema kuwa fomu hiyo iliwasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa Wabunge wa CCM ikiambatana na barua inayotaka kuitishwa kwa kikao kitakachowakutanisha.
“Tuliwaomba waitishe kikao cha wabunge wa CCM ili mawaziri ambao tunawaona hawatimizi majukumu yao kikamilifu waweze kuhojiwa lakini wakawa wanasuasua,” kilisema chanzo hicho.
Kikao hicho kilitakiwa kufanyika Alhamisi iliyopita ili kuwahoji mawaziri hao kabla ya kikao cha Kamati Kuu.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikaririwa wikiendi hii akieleza kuwa mawaziri saba walihojiwa katika kikao cha Kamati Kuu na kumuachia Rais Jakaya Kikwete jukumu la kuamua kuwafukuza kazi, kuwahamisha au kuwataka kutekeleza majukumu yao kikamilifu. MWANANCHI

Monday, December 16, 2013

Simulizi ya Mandela

Toka kulia: Rais wa sasa Afrika kusini, Jacob Zuma , Rais wa kwanza mweusi wa Afrika kusini,  Mzee Nelson Mandela (enzi ya uhai wake) na Rais wa pili wa Afrika Kusini,  Thabo Mbeki

Ndugu Zangu. 
Nahitimisha simulizi za Mzee Wetu Madiba. Najisikia nimechukua jukumu langu la kugawana nanyi kile kidogo nilichoweza kukusanya kumhusu Mzee wetu Madiba.


Natumaini nitapata muda siku zijazo, nisimulie zaidi juu ya yale yenye kufanya maisha ya Madiba kuwa simulizi endelevu kwetu Waafrrika na watu wa dunia. 


Lakini, ukweli unabaki, kuwa leo dunia imemzika Mzee Madiba kijijini kwao Qunu. Yaliyobaki nyuma yake ni yale mema aliyoishi akayahubiri. Nasi tunapaswa kujifunza kutoka hayo.
Yumkini Mungu amechagua kupumzisha Mandela wakati muafaka. Maana, ni katika kipindi ambacho, Afrika Kusini inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani.



Chama kikuu cha ANC kinakabaliwa na changamoto za ndani ya chama na kwenye jamii. Kinapaswa sasa kijiandae kufanya mabadiliko makubwa yatakayorudisha imani ya wapiga kura wake wengi. Wapiga kura ambao wameanza kukata tamaa. Hawana furaha ya maisha yao. Wamekata tamaa ya kuona kuwa kesho yao yaweza kuwa bora zaidi.



ANC kihistoria imekuwa ikitegemea sana Jumuiya yake ya Vijana na Shirikisho la Wafanyakazi ( Cosatu) Jumuiya zote hizo zinaonekana kugawanyika. Kuna wanaoipa mgongo ANC. 


Na Mandela anausia; 
" The leader must keep the forces together, but you can't do that unless you allow dissent. People should be able to criticise the leader without fear of favour. Only in that case are you likely to keep your colleagues together"- Nelson Mandela. It is when Mandela gave a piece of advice to newly elected Party Leader, Thabo Mbeki at the ANC Congress in Mafikeng, 1997. 



Kwamba kiongozi unapaswa kuyaunganisha makundi, lakini, huwezi kufanya hivyo kama huruhusu sauti kinzani. Sauti za wenye kukupinga. Watu wawe huru kumshutumu kiongozi bila ya woga. Ni kwa namna hiyo tu kiongozi unaweza kuyaunganisha makundi. Mandela aliyasema hayo kule kwenye Mkutano Mkuu wa ANC uliompitisha Thabo Mbeki kuwa Rais wa ANC, ni mwaka 1997. 

Naye Askofu Desmond Tutu alipata kusema; 
"Kuna tofauti ya kimsingi kati ya kuwa huru na kuwa katika hali ya kukandamizwa. Kuwa huru ni pamoja na kupata huduma za msingi za kijamii, kuwa na ajira, maji ya bomba, umeme, makazi bora na huduma za msingi za afya. Kuna maana gani basi ya kuwa huru wakati ubora wa maisha ya watu haujaimarishwa? Kama sivyo, hata kura nazo hazina maana yoyote!" (Desmond Tutu- William Gumede; Thabo Mbeki And The Battle For The Soul Of The ANC, Uk. 67). 

Nkosi Sikelel i Afrika


Kwa hisani ya Juma Mtanda

WAPINGA MAENDELEO YA ELIMU MBINGA KUKIONA


Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga akitoa msisitizo wake mbele ya Wadau wa elimu wa wilaya hiyo(Hawapo pichani) katika ukumbi wa Umati uliopo mjini hapa, juu ya Katibu wa CWT wilaya humo kuwa ni kikwazo cha maendeleo ya elimu. 


Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

MKUU wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga amemshukia Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) tawi la Mbinga Samwel Mhaiki, akidai kwamba ni kikwazo cha maendeleo ya elimu wilayani humo, kutokana na katibu huyo kupenda kuendesha migogoro na kuchonganisha walimu mashuleni.

Ngaga alisema hayo alipokuwa akizungumza na Wadau wa elimu, Kata ya Mbinga mjini juu ya kukuza maendeleo ya sekta ya elimu wilayani humo, katika hafla fupi iliyofanyika ukumbi wa Umati uliopo mjini hapa.

Alisema kuwa katibu huyo amekuwa kinara namba moja wa kupita mashuleni na kushinikiza walimu waache kufundisha (Wagome) hadi watakapolipwa madai yao, jambo ambalo alilieleza kuwa limekuwa likileta mgogoro usio na tija katika jamii.

Alieleza kwamba licha ya Mhaiki kuitwa mara nyingi ofisini kwake na kumtaka aache kuendeleza migogoro hiyo, anashangaa kumuona bado akiifanya.


“Tumemuonya mara nyingi huyo Mhaiki, lakini amekuwa bado akitusumbua kwa kuandika mabarua na kusambaza mashuleni akishinikiza walimu wagome waache kufundisha….tulimwambia serikali inashughulikia madai ya hawa walimu na watalipwa malumbano haya anayoyaendeleza sasa ningelikuwa na uwezo mimi kama Mkuu wa wilaya hii ningemhamisha, kwa sababu ni kikwazo kwa maendeleo ya elimu hapa wilayani, leo walimu wakigoma watoto wetu watafundishwa na nani”, alisema Ngaga.

Mkuu huyo wa wilaya awali alisema wilaya hiyo hivi sasa imejipanga katika kukuza kiwango cha elimu kwa shule za msingi na sekondari, ambapo kwa kushirikiana na ofisa elimu wa wilaya hiyo Mathias Mkali wamekuwa wakiendelea na mfumo wa watoto kujisomea wakati wa likizo (Makambi) kwa kila kata wilayani humo, hususani kwa watoto wa darasa la sita ambao wanaingia darasa la saba mwakani.

Alisema wazazi wameitikia wito kwa kiasi kikubwa juu ya suala hilo na kukubaliana kutoa michango ya chakula, katika vituo hivyo ambavyo watoto wao wanasoma wakati huu wa likizo.

Alisisitiza kuwa mtu yeyote atakayeonekana anakwamisha mikakati waliyojiwekea ya kukuza kiwango cha elimu wilayani Mbinga, yupo tayari kumwajibisha ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo

Friday, November 8, 2013

USTAWI WA KIJAMII NA UCHUMI RUVUMA

Kanisa la RC lililopo Sinai  Manispaa ya Songea, Kanisa hili lipo kando ya barabara iliyojengwa kwa kiwango cha lami toka pacha ya Peramiho kuelekea mjini Mbinga. Eneo hilo sasa limepanda thamani kutokana na usafiri wa uhakika jambo linalovutia wengi kwenda kuwekeza katika kilimo, ujenzi wa nyumba na ufugaji.

Hapa ndiyo "Dar Pori" Wilaya mpya ya Nyasa ni kilomita nane hivi kuingia Msumbiji. Kijiji hiki kimeibuka wakati wa machimbo ya Madini hasa dhahabu. hiyo barabara unayoione imechimbwa kwa majembe ya mkono. hakuna kinachoshindikana kwa binadamu wakidhamiria. Vijana wa bodaboda maarufu kama yeboyebo mkoani Ruvuma wakisubiri abiria "waliobongoa" waliopata fedha au madini  kuwapeleka Mbinga, Nauli yake ni Shs 40,000/- kwa abiria mmoja. Kazi kwelikweli. 

Mkazi wa Dar es Slaam, Bw. Jacob Silvesta Nyumayo, akionyesha mkungu wa ndizi huko kijiji cha Mgazini Kata ya Kilagano Songea Vijijini ambao umezaa vya kutosha licha ya kutotunzwa vizuri. Bw. Jacob anasema udongo wa Songea unafaa sana kwa kuzalisha ndizi za aina zote na huenda ndizi zingeliweza pia kuchangia pato la wananchi wa mkoa wa Ruvuma wakithubutu hasa wakati huu ambao sasa barabara zimefunguka na kuacha kutegemea zao moja tu la chakula kama mahindi na kutupilia mbali mihogo, mtama na mazao mengine. 

UKATILI , UNYAMA WA WANAUME


Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria Songea,(Sopce) Fatuma Misango (mwenye kilemba cheusi) akimsikiliza mwanamke aliyejeruhiwa na mmewe bada ya kulewa huko ofisi ya mtendaji kata ya Tanga hivi karibuni.
HADITHI: Ulevi wa mume wake huyo ulimfanya achukue hatu ya kumpiga mwanamke huyo hadi kuzirai (Kuzimia) alivyomaliza kazi hiyo naye akalala fofo na kukoroma kama vile hakuna tukio alilolifanya hadi alipokuja kamatwa na mgambo kwa amri ya Afisa mtendaji wa kata hiyo.
KISA: Mwanaume huyo ana mtindo wa kwenda kulewa na kumuamuru mkewe asifunge mlango na komeo ili asipate tabu arejeapo nyumbani akiwa mitungi.
Hivyo mara kwa mara anaporudi husukuma mlango na kuingia ndani hujitupa kitandani akishapiga misosi yake hasa kama kuna kitoweo cha nyama.
SIKU YA TUKIO: Mwanaume huyo alikwenda kuzinyaka. kama ujuavyo pome si chai, usiku wa manane akarejea kwake. bahati mbaya akaukuta mlango u wazi haujaegeshwa. akaanza kulipuka kwa hasira kuwa ni vipi mlango ubaki wazi?
Mkewe akamjibu aliuegesha kama anavyofanya siku zote. Mume akasema haiwezekani ubaki wazi.
Mkewe akasema hapana mume wangu huenda upepo umeufungua.
Mume: Nasema haiwezekani, hapa atakuwa mwanaume amekimbia katoka humu ndani sikubali.
Kichapo kikaaanza kutembezwa.

Tuesday, November 5, 2013

IMANI BILA MATENDO? WANANCHI WA NYASA WALA KIAPO KUILINDA TANZANIA

Kutumikia wapiga kura: Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum CCM Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Stella Manyanya akisalimiana na Mkurugenzi wa Blogu hii Jimboni Mjini Mbinga hivi karibuni wakati wa Ziara ya Mwenyekiti wa UWT  taifa ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na watoto, Mhe. Sofia Simba
Angalia bango katika ukuta wa jengo linalosema "Imani bila Matendo, imekufa," Watanzania tunahitaji matendo zaidi.

Maeneo Magumu: Mhe. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sofia Simba akiwasili kijiji cha Dar Pori kwa wachimbaji wa madini wilaya mpya ya Nyasa. Waziri Sofia Simba amekuwa waziri wa kwanza mwanamke kuwasili eneo hilo gumu kufikika ambalo lipo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji tangu nchi hii ipate huru 1961 (Kushoto) ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bw. Ernest Kahindi akimuongoza waziri huyo jukwaani wakati wananchi wakishangilia wakati wa ziara yake mkoani Ruvuma hivi karibuni.

Mikono Juu: Ni kiapo cha wananchi kuwa na  Utii wa kuipenda, kuitumikia na kuilinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kiapo hiki kilitolewa mbele ya waziri Simba huko Dar Pori wilaya ya Nyasa. Jengo la bati linaloonekana kwa mbali nyuma pale mlimani ni zahanati iliyojengwa kwa nguvu za wanakijiji hao wachimbaji wa madini.

MITIHANI YA KIDATO CHA NNE 2013

Tunawatakia heri ya mitihani ya kidato cha nne, 2013.
Huo ndio mwanzo wa kupanda mlima wa elimu ya juu.
kila la heri wote wanaofanya mitihani, wasimamizi, wazazi, na wadau wote.

Tuesday, September 10, 2013

WAANDISHI NA VINGOZI WA SERIKALI

Baadhi ya Waandishi wa habari wanaume wa mkoa wa Ruvuma, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali ya Mkoa wa Ruvuma. (Mwenye shati la maua katikati) ni  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabith Mwambungu ( jirani yake kushoto )  ni Mkuu wa Wilaya ya Songea,  Bw. Joseph Joseph Mkirikiti . ( Picha kwa hisani ya Ruvuma Press Club)

MTIHANI WA DARASA LA VII - 2013

Tunawatakia wanafunzi wote wa Darasa la Saba (VII) nchini mtihani mwema wa kumaliza elimu ya Msingi. utakaoanza kesho Jumatano 11, September 2013.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa
Mtihani huu utakaofanyika kesho ndio msingi imara utakao amua kuendelea na masomo ya sekondari kwa mwanafunzi muhusika au la.
Miaka hii ya karibuni, tumeshuhudia waziwazi vyombo vyetu vya usalama vimewakamata baadhi ya wanafunzi, walimu na mara nyingine hata wazazi kushiriki kikamilifu katika uhalifu wa kielimu wa kuiba mitihani .
Uhalifu huu unafanywa ili kuwafaulisha wanafunzi wasiostahili na ndio wanaokuwa mizigo katika elimu yao ya upili. Jambo hilo ni baya kupita maelezo kwani elimu ni sawa na moto. Moto haukopeshi, ukiweka mkono katika kaa la moto utaungua mara moja. Na elimu hali kadhalika kama kijana hana uwezo akapitishwa kwa hila kuendelea na masomo, huwa ni mzigo kwa kijana huyo, familia yake pia taifa.
Tusishangae kuona madaktari feki, wahandisi kanjanja, walimu mizigo wanasiasa bomu na wengine kibao bila kusahau wakulima wasiozingatia kanuni za kilimo bora.
Lengo kuu hapa ni kuwatakia mtihani mwema, usio na hila za kuvujishwa wala kuvujisha.
Jamii ya wanaRuvuma inasema hakuna linaloshindikana, utavuna ulichopanda.
Mtihani Mwema 2013

Saturday, August 31, 2013

KISOMO MWANZA WAPETA

Na Juma Nyumayo, Songea
KITUO Cha Taifa Kisomo Mwanza kinaendelea kutoa huduma zake kwa kuzingatia Matokeo Makubwa sasa (Big result Now) Kituo hiki kinaongozwa na Naibu Mkurugenzi Kisomo Mwanza, Bibi Mary Salu ambaye amewakaribisha wakuu wa vituo vya uchapaji kanda vya Songea, Mbeya, Tabora na Mkuu wa Press 'A' Dar es Salaam. angalia Picha zifuatazo.
Watumishi wa Kituo cha Kisomo Mwanza wakiwa katika Idara ya Computer, anayeonekana mbele ni Rabeca Fred akiwa kazini.



Mr Andrew Kingu akionyesha Ubora wa kazi zinazochapwa na Kiwanda cha Kisomo Mwanza

Naibu Mkurugenzi Kituo cha  Taifa Kisomo Mwanza, Bibi mary salu ( kushoto) akitoa maelezo kuhusu kiwanda cha uchapaji kisomo mwanza (kulia) ni juma Nyumayo toka Tujifunze Songea.



Friday, August 16, 2013

WAANDISHI WA HABARI RUVUMA WAONYWA

Na Steven Augustino, Songea
WAANDISHI wa Habari Mkoani Ruvuma wameonywa kuamini habari kutoka
mitandao na kuzitumia kuhabarisha umma bila  kuzifanyia utafiti wa
kutosha katika internet na kutumia vyanzo vya kuaminika ikiwemo
kuwahoji wahusika kupata habari za ukweli ambazo zitakuwa na manufaa
kwa wasomaji.
Hayo yameelezwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa namna ya
kuandika Habari kwa kutumia mitandao ya Internet na kutuma picha za
kihabari  Mtandaoni yanayoendeshwa katika Ukumbi wa Veta,Manispaa ya
Songea, Taasisi ya Vyombo vya habari kusini mwa Africa (Media
Institute of Southern Africa) MISA TANZANIA.
Wanahabari hao pia wanafundishwa namna ya kufanya utafiti wa vyanzo
vya habari mbalimbali katika Internet na kufungua njia nyingine za
mawasiliano kama  ‘youtube’, Blogu na namna ya kuzitumia katika tasnia
ya kutengeneza na kutuma habari zikiwa na takwimu sahihi.
Awali akiongea katika ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku tatu, Afisa
Habari MISA -TANZANIA , Sengiyuva Gasiligwa,  alisema kuwa lengo la
mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wanahabari ili waweze kwenda na
wakati hasa katika teknolojia ya kimtandao.
Wanahabari hao pia wananolewa ili waweze kujua kwa undani maana ya
internet, ‘Worid Wide Web’ , ‘Computer’,  na matumizi yake kwa manufaa
ya maendeleo ya technolojia, uchumi, siaa na utamaduni na kujali
maadili
Gasiligwa alisema kuwa mafunzo hayo yanayo wahusisha Waandishi wa
Habari za Magazeti, Terevissin na Radio yanafanyika kwa ushirikiano
MISATAN na shirika la VIKES  toka Finland na kwamba kwa kuanzia
mafunzo hayo yalifanyika Mkoani Pemba huku Zanzibar Tanzania Visiwani
na sasa Ruvuma na baadaye mkoani mwanza.
Nae mwezeshaji wa mafunzo hayo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini
Iringa,  Saimon Berege,  pamoja na mambo mengine aliwataka Wanahabari
hao kuwa na ari ya kujiendeleza kielimu na kuwakaribisha kwenda kusoma
digrii ya pili (masters) Inayotolewa na chuo hicho.
Wakiongea kwa nyakati tofauti wanahabari hao pamoja na kuipongeza
taasisi hiyo kwa kuona umuhimu wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari
wamesema kuanzia sasa wataweza kufanya kazi za uandishi wa habari wa
kiuchambuzi kwa kuoanisha habari kutoka vyanzo vya mataifa mbalimbali,
kuandika habari kwa kutumia takwimu kutoka katika mitandao na kutumia
taarifa na hotuba zilizopita zilizotolewa na viongozi wa mataifa
mbalimbali duniani .
Aidha washiriki hao wameonyesha ushirikiano mkubwa katika uchambuzi wa
mada zilizotolewa na wameomba mafunzo kama hayo yatolewe mara nyingi
iwezekanavyo ili kuwakumbusha kuamsha ari ya waandishi.
Mwisho

Saturday, July 13, 2013

RUVUMA WAFANYA MAANDALIZI YA KUMPOKEA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA

 Hivi ndivyo mji unavyoonekana leo katika baadhi ya barabara za Manispaa ya Songea
 Gari likisukumwa baada ya kukaa muda mrefu katika garage bubu iliyopo mitaa ya Buhemba
 Mji safi
Hapa ni mtaa wa Dilux magari yakiwa yamepangwa katika utaratibu mzuri
Mji unawake
Wafanya biashara wa matunda katika eneo hili la Dilux wameondolewa kutokana na ujio wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda mkoari Ruvuma
Dereva Yebo wakiwa katika vituo vyao kwa utaratibu mzuri
Gari la Manspaa likiwa kazini maeneo ya bombambili huku wafanya kazi wakiwa wanazoa na njia hii atapita akiwa anaelekea kukagua miradi na kuweka jiwe la msingi katika baadhi ya maeneo
 Hii ni sehemu moja wapo iliyobomolewa vibanda ikiwa ni  kuweka mji safi
Hapa ni maeneo ya Bombambili upakaji wa rangi alama za barabarani ukiendelea siku ya leo kabla ya Waziri mkuu kutua Ruvuma hapo kesho

Habari kwa hisani ya www.demashonews.blogspot.com