Tuesday, November 5, 2013

IMANI BILA MATENDO? WANANCHI WA NYASA WALA KIAPO KUILINDA TANZANIA

Kutumikia wapiga kura: Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum CCM Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Stella Manyanya akisalimiana na Mkurugenzi wa Blogu hii Jimboni Mjini Mbinga hivi karibuni wakati wa Ziara ya Mwenyekiti wa UWT  taifa ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na watoto, Mhe. Sofia Simba
Angalia bango katika ukuta wa jengo linalosema "Imani bila Matendo, imekufa," Watanzania tunahitaji matendo zaidi.

Maeneo Magumu: Mhe. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sofia Simba akiwasili kijiji cha Dar Pori kwa wachimbaji wa madini wilaya mpya ya Nyasa. Waziri Sofia Simba amekuwa waziri wa kwanza mwanamke kuwasili eneo hilo gumu kufikika ambalo lipo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji tangu nchi hii ipate huru 1961 (Kushoto) ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bw. Ernest Kahindi akimuongoza waziri huyo jukwaani wakati wananchi wakishangilia wakati wa ziara yake mkoani Ruvuma hivi karibuni.

Mikono Juu: Ni kiapo cha wananchi kuwa na  Utii wa kuipenda, kuitumikia na kuilinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kiapo hiki kilitolewa mbele ya waziri Simba huko Dar Pori wilaya ya Nyasa. Jengo la bati linaloonekana kwa mbali nyuma pale mlimani ni zahanati iliyojengwa kwa nguvu za wanakijiji hao wachimbaji wa madini.

No comments:

Post a Comment