Friday, November 8, 2013

UKATILI , UNYAMA WA WANAUME


Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria Songea,(Sopce) Fatuma Misango (mwenye kilemba cheusi) akimsikiliza mwanamke aliyejeruhiwa na mmewe bada ya kulewa huko ofisi ya mtendaji kata ya Tanga hivi karibuni.
HADITHI: Ulevi wa mume wake huyo ulimfanya achukue hatu ya kumpiga mwanamke huyo hadi kuzirai (Kuzimia) alivyomaliza kazi hiyo naye akalala fofo na kukoroma kama vile hakuna tukio alilolifanya hadi alipokuja kamatwa na mgambo kwa amri ya Afisa mtendaji wa kata hiyo.
KISA: Mwanaume huyo ana mtindo wa kwenda kulewa na kumuamuru mkewe asifunge mlango na komeo ili asipate tabu arejeapo nyumbani akiwa mitungi.
Hivyo mara kwa mara anaporudi husukuma mlango na kuingia ndani hujitupa kitandani akishapiga misosi yake hasa kama kuna kitoweo cha nyama.
SIKU YA TUKIO: Mwanaume huyo alikwenda kuzinyaka. kama ujuavyo pome si chai, usiku wa manane akarejea kwake. bahati mbaya akaukuta mlango u wazi haujaegeshwa. akaanza kulipuka kwa hasira kuwa ni vipi mlango ubaki wazi?
Mkewe akamjibu aliuegesha kama anavyofanya siku zote. Mume akasema haiwezekani ubaki wazi.
Mkewe akasema hapana mume wangu huenda upepo umeufungua.
Mume: Nasema haiwezekani, hapa atakuwa mwanaume amekimbia katoka humu ndani sikubali.
Kichapo kikaaanza kutembezwa.

No comments:

Post a Comment