Tuesday, August 9, 2011

Mwanza nako tatizo mafuta!

Hapa katika Picha nikiwa na waheshimiwa wajumbe wa Bodi ya UTPC, Bw. Hassan Hashim toka Tanga, Lucy Ogutu (kulia) toka Dar es Salaam na Mary Edward katikati akitokea Dodoma hivi sasa anafanyia kituo kikubwa kabisa cha Televiheni-ITV Dar Es Salaam wakijadili jambo jana Julius Nyerere International Airport kabla ya kwenda Mwanza.

Bw Juma Nyumayo akieleza jambo kwa Bw. Hassan Hashim aliyepiga pica hii.



Picha ya tatu Toka kulia Mary Edward, Hassan Hashim, Lucy Ogutu na Mimi Juma Nyumayo tukiwa uwanja wa Ndege wa kimataifa Dar es Salaam kabla ya kuruka kwenda Mwanza. (Picha na Ali Haji Hamad-Pemba)





Nimewasili Jiji la Mwanza, hakika linapendeza. Tatizo ni lilelile la mafuta. Petroli na Disel. Madereva wa Taxi hapa wanadai vituo vingi havina mafuta na kusababisha msururu wa magari kwenye vituo visivyo na mshipa wa kuwafuata hao wakubwa wao. Naunga mkono asilimia 100% Hoja ya Dharura kujadiliwa Bungeni kuhusu mafuta iliyotolewa na Mbunge Kijana ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Nishati na Madini Mhe. January Makamba ambaye bila woga ameitka serikali kuonyesha uwepo wake. Hata hivyo wabunge wengi waliochangia nimewapenda kwa kile walichokionesha maslahi ya taifa bila kujali vyama walivyotoka. wbunge hawa ni pamoja na Mbunge wangu Mhe. Jenister Muhagama Mbunge wa Jimbo la Peramiho ambaye licha ya kuwa Katibu wa wabunge wa CCM alikuwa mkali akimaanisha Ibara ya 8 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa serikali hupewa madaraka na wananchi hivyo wananchi lazima waione serikali yao inawajali katika kipindi kama hiki.

Asanteni sana Bunge huu ndio mwendo.

Juma Nyumayo

No comments:

Post a Comment