Saturday, July 30, 2011

Breaking Neeewws! Mstahiki Meya wa Manispaaya Songea, Ali Said Manya

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mheshimiwa Diwani wa Lizaboni, Ali saidi Manya, amefariki dunia leo katika Hospitali ya Misheni Peramiho, Maili 15 toka Songea mjini. Taarifa za kifo chake zilizopokelewa kwa mshtuko mkubwa na wananchi mkoani hapa, zimetangazwa na Naibu Meya wa Manispaa ya Songea, Mheshimiwa Mariam Dizumba. Mstahiki Meya Ali said Manya wakati wa uhai wake pichani kushoto mwenye Suti nyeupe akifurahia jambo alilosema Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club Juma Nyumayo, (aliyesimama) alipohudhuria kikao cha wadau wa habari mkoani Ruvuma mapema mwaka huu. Kwa mujibu wa Naibu Meya Mazishi yake yatafanywa Jumatatu, Nyumbani kwake Lizaboni Manispaa ya Songea kwa heshima zote za chama chake chja mapinduzi na serikali ya manispaa ya Songea.




No comments:

Post a Comment