Tuesday, May 7, 2013

DKT.EDWARD HOSEA ATOA MADA UBAYA WA RUSHWA KWA VIONGOZI WA DINI MIKOA


Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Dkt. Edward Hosea, anayepiga makofi akiingia eneo la Hoteli ya Herritage Cottage, Songea kwa lengo la kutoa mafunzo kwa Viongozi wa Dini  kupambana na Rushwa, anayefuatia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Thabiti Mwambugu wakiangalia kikundi cha ngoma hakipo pichani leo.


Kikundi cha Ngoma ya lizombi cha Shaba Group, (Kulia) wakimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Dkt. Edward Hosea, na  (Katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu na anayefuatia ni Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma, Daud Masiko


Kama hapo juu Dkt. Hosea na Mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu (aliyenyosha mkono juu), akiwapungia wacheza Ngoma ya lizombi wa Shaba Group kwa kazi nzuri


Mkuu wa Mkoa Said Thabit Mwambungu akitoa hutuba ya ufunguzi leo

Mkurugenzi  Mkuu wa TAKUKURU nchini, Dkt. Edward Hosea, akimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kumkaribisha Mkoa wa Ruvuma kwa kazi muhimu ya kutoa mada mafunzo kwa viongozi wa Dini mikoa ya Ruvuma, Njombe na Iringa leo




Mkuu wa Mkoa wa Ruvumna Said Thabit Mwambungu akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dkt Edward Hosea, wakati akitoa shukurani zake leo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi wa Dini wa mikoa ya Ruvuma, Njombe na Iringa leo.




Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Ruvuma, Daud Masiko akifuatilia hotuba ya ufunguzi leo mjini Songea



Dkt Edward Hosea, akisisitiza kuwa rushwa ni kosa na ni zambi kwa binadamu, hivyo ipigwe vita na kada zote hapa nchini




Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU , Dkt. Edward Hosea (Katikati) akiendelea na hotuba yake ya kupambana na Rushwa hapa nchini mbele ya viongozi zaidi ya 50 wa Dini za kiislamu na kikristu wa mikoa ya Ruvuma, njombe na Iringa leo. Pichani kulia ni Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Mwambungu na kulia ni Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Ruvuma, Daudi Masiko.

Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Ruvuma, Bw. Musa Misalaba akiwa nje ya Ukumbi wa Hoteli ya Herritage Cottage Manispaa ya Songea, akisisitza umuhimu wa mafunzo haya ya kupambana na Rushwa kwa viongozi, Dini Mkoani Ruvuma na jirani ya Njombe na Iringa leo  


No comments:

Post a Comment