Thursday, May 30, 2013

KADA MAARUFU WA CCM SONGEA, BW. MATHIAS NYONI , APATWA NA MSIBA WA MKEWE, WENGI WAQHUDHURIA MAZISHI


Kada wa CCM Wilaya ya Songea Mjini na Fundi Cherehani Maarufu, Bw. Mathias Nyoni (wa kwanza kulia) mara baada ya kumaliza kumhifadhi mkewe Salama aliyefariki jana na kuzikwa leo katika makaburi ya Namanditi kwa  kaleza nje kidogo ya mji njia ya  kuelekea Peramiho


Dua za mwisho kwa Mke wa Bw. Mathias Nyoni, hiyo ndio nyumba yake katika pumziko lake la milele.


Sheikh Abdalah Ndege aliyevaa kofia akitoa maelekezo ya watu mashuhuri waliofika katika msiba huo na kuwaomba watoe neon akiwepo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea mjini, Bw. Mhenga.



Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea Mjini, Bw. Mhenga akiwashukuru wananchi na kutoa rambirambi zake kwaniaba ya wana CCM Songea Mjini leo katika Makaburi ya Namanditi. Bw. Mhenga amewashukuru watu wote wakiwemo wa vyama vya upinzani, wafanyabiashara, wakulima na kutoka makundi ya vijana wanawake na wazee kwa kujitokeza kwa wingi kumzika mke wa Kada wa CCM  Salama na kwamba huo ndio msimamo wa CCM katika kuijenga nchi kuwa na amani.


Watu walioshirioki mazishi wakisikiliza shukurani toka kwa familia ya marehemu toka kwa Sheikh Abdala Ndege, aliyesimama kati ya wazee wawili waliokaa


Mhe. Meya wa Manispaa ya Songea, Charles Mhagama,( wa kwanza kushoto)  akiongoza watu toka makaburini eneo la Namanditi Manispaa ya Songea mara baada ya kuzika Alasiri ya leo


Watu wanaendelea kutawanyika toka makaburini


Kila mmoja natafuta usafiri wake kurejea alikotoka wengi wao wakitokea katikati ya mji wa Songea leo


Kina mama nao walikuwepo kwa wingi kumsindikiza Mke wa Mathias Nyoni, Salama ambaye pia alikuwa ni  Mtaalamu wa kuendesha Saloon mjini Songea


Baadhi ya vyombo vya usafiri vilivyowaleta watu ukiachilia mbali daladala zilizoleta watu kwa wingi katika msiba huo ambao ulikusanya watu wa makundi mbalimbali wakiwemo viongozi, watumishi wa serikali, wafanyabiashara, wakulima na wanachama wa vyama mbalimbali wakiongozwa na wana CCM wa wilaya ya Songea Mjini. (Picha zote na Maelezo na Juma Nyumayo)


No comments:

Post a Comment