Saturday, April 20, 2013

UJUMBE WA JUMAMOSI TOKA KWA DADA YASINTA WA MAISHA


KIJANA WA DADA YASINTA (KUSHOTO)  WALIPOTEMBELE OFISI YETU  RURAL PRESS, SONGEA ILIYOPO UWANJA WA SABASABA-MATARAWE SONGEA AKIWA NA WAZAZI WAKE (HAWAPO PICHANI) AMEKAA NAMI JUMA NYUMAYO. MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO NILIFURAHI SANA FAMILIA HIYO KUTUTEMBELEA OFISINI NA KUJIFUNZA TUFANYAYO.
Nimekuwa msomaji wa marakwa mara wa Blogu ya MAISHA ruhuwiko.blogspot.com, na VANGONI zote hizo za Dada yetu Mpendwa Yasinta Ngonyani anaeishi Sweden. Yasinta na familia yake tumewahi kuonana machokwamacho. Watoto wa siku hizi wanasema "live." Tulizungumza mengi. Kilichonifurahisha katika hayo mengi ni pamoja na ujumbe huu wa Jumamosi ya Leo, Siku moja tu kabla ya kuadhimisha siku yangu ya kuzaliwa hapo kesho Tarehe 21, Aprili.
Ninajivunia Dada Yasinta kwakuwa mmojawapo aliyejiunga na Blogu yangu ya "Jamii ya wana Ruvuma" www.http//ruvumapress.blogspot.com. mwanzoni na kuijumuisha katika Blogu anazozifuatilia. Asante saana Dada    

Ujumbe wa Jumamosi nimeuchukua Katika Blogu yake ya www.http//ruhuwiko.blogspot.com  na ukibonyeza tu hapo utakumbana na "kisima cha maarifa."  Utafaidi.

Namuomba radhi kwa kuchukua ujumbe wake huu, naamini ataikubali kwakuwa lengo lake tunufaike wote. Asante Dada Yasinta.

Ukiwa DUNIANI USIHUZUNIKE na usiwe MNYONGE hata kama una UMASKINI kiasi gani. Mungu yuko pamoja nawe na unatakiwa kuzingatia haya:-
1. Usijilaumu kwa lolote lililokutokea
2. Usihofu kuhusu hali uliyo nayo sasa.
3. Usijilinganishe na mtu yeyote duniani.
4.
5. kumbuka Mungu ndie mpangaji wa kila linalokutokea.
6. Usiwaze sana kuhusu kesho waza kuhusu leo.
7. Ukikosa ulichokikusudia yote ni mipango ya Mungu.
MUWE NA SIKU/JUMAMOSI  NJEMA

1 comment:

  1. Kwanza nachukua nafasi hii na kusema ahsante sana. Ni kweli wote tuna nia moja..ahsante kwa kuupokea ujumbe kihivyo.

    ReplyDelete