Thursday, April 11, 2013

Jamani hii elimu ya ushirikina vipi tena? wafungua milango kwa kutumia makalio


Watoto wafuzu masomo bila wazazi kujua na wafungua milango kwa kutumia makalio
Na Steven Augustino, Tunduru

WAZEE wa tano kutoka katika Kijiji cha Mtonya, Wilaya Tunduru Mkoani Ruvuma wamezuiliwa katika Kituo kidogo cha Polisi Nakapanya ili kulinda usalama wa maisha yao na kuwafanya wasishambuliwe kutokana na kutuhumiwa kufanya ushirikina na kuwafundisha taaluma hiyo watoto wawatu bila ridhaa ya wazazi wao.
Tukio hilo la aina yake, lilitokea baada ya wazee hao wanaodaiwa kuwa na uwezo wa kufungua na kuingia katika nyumba za watu kwa njia za mazingara kufumwa wakifanya vitendo hivyo katika kijiji cha Mindu Wilayani Tunduru.
Taarifa zilizothibitishwa na Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Nakapanya,  Bw. Kubodola Ambali, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Spia Msusa (50), Ayana Iddi (75) Adresia Maulidi(68), Jenifa Saimon (60) na mwingine aliyefahamika kwa jina la Binti Nyoya (60).
Bw. Ambali, aliendelea kufafanua kuwa Mpango huo uligundulika baada ya wazazi wa Mtoto Ally Milongo,  kuamka na kuanza kumtafuta mtoto wao huyo mwenye umri wa miaka 10 kutoweka usiku wa manane ndani ya nyumba yao katika mazingira ya kutatanisha .
Baba wa Mtoto huyo Bw. Milongo Ally, alisema kuwa baada ya tukio hilo la kutoweka kwa mtoto wao yeye na mkewe waliamka na kuanza kumtafuta katika maeneo tofauti ya kijiji hicho ambapo  wakafanikiwa kuwaona Wazee hao wakiwa uchi wa mnyama pamoja na kijana wao na walipojaribu kuwasogelea vikongwe hao walitoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Alisema baada ya tukio hilo walimkamata mtoto wao na kwenda naye nyumbani kwao na  baada ya kumbana na kumtaka aeleze aliko kuwa ndipo akawataja watu hao ambao baada ya kuitwa walikiri na kuomba radhi kuwa hawatarudia kumchukua mtoto huyo ambaye walidai kuwa ni miongoni mwa washirika wao wa muda mrefu ambao tayari wameshampatia mafunzo ya kutosha.

Alisema katika tukio hilo wazee hao walitozwa faini ya Shilingi 100,000 ambayo waliilipa papo hapo na baadae wakaruhusiwa kuondoka kituoni hapo baada ya kundi la watu waliojitokeza kuwaangalia kuondoka.
Akiongelea tukio hilo Mtoto Ally Milongo,  alisema kuwa  mara kwa mara watu hao wamekuwa wakienda kumchukua yeye na watoto wenzake wanne na kuwapeleka katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwafundisha utaalamu kuingia na kuwachezea watu na baadae hurejea majumbani mwao na kufungua milango kwa kutumia matako huku wazazi wao wakiwa hawafahamu kinachoendelea.

Mwisho

 

No comments:

Post a Comment