Sunday, October 3, 2010

VITU TOFAUTI VIONJO TOFAUTI

Picha ya kwanza ni ya Boss wa TUJIFUNZE Kanda ya Kusini Bw. Christian Sikapundwa mara baada ya kufungua Blog ya TUJIFUNZE KUSINI. Huu ni uharibifu mkubwa wa mazingira, moto huo ulikuwa unawaka katika misitu ya Lilondo tarafa ya Madaba Songea Vijijini jana wakati tunarudi toka Dar na Bus la Super Feo hakika wanakijiji walipagawa kuuzima lakini wapi maana kila pembe na ujuavyo miti ya kupanda inavyopwaka utafikiri petroli Boss wangu kaniambia aliyechoma anajisifu eti ana mkono mkali.


Jamani uzuri ulioje sifa apewe Bwana kwa uumbaji hapa ni Shamba la Chai Kibena pale Njombe , unajua dereva akasema teremkeni mkachimbe dawa mie nikauona uzuri huo na huyo Bwana ni Mlonda au mlinzi wa shmba hilo lakini yeye halijui jina lake.

Picha ya Kushoto ni Bw. Adam Nindi katikati ni Bw Kiim ambaye ni Msanii wa uchoraji lakini pia ana asilia ya mkoa wa Ruvum,a na huyo kulia ni Juma Nyumayo Mwenyekiti wa ruvuma Press Club wakishauriana jambo kuhusu harakati za kijinsia katiak darasa Mojawapo la TGNP Dar es Salaam. picha hiyo ilinitetemesha sana hata kupiga sikuamini kuwa hapo ni Dar ni nyuma tu ya kiwanda cha Urafiki Dar es Salaam. Bongo nayo ipio hivyo je madongo poromoka ya mikoani inakuwaje.
(Picha zote na Juma Nyumayo)









1 comment:

  1. Ni kweli ni uhalibifu sana kuchoma moto mazingira. Nimefurahi sana umenifikisha mpaka nyumbani kabisa. Ahsante sana.

    ReplyDelete