Friday, October 29, 2010

Haya Dr Nchimbi na kampeni za mwishomwisho

Dr. Emanuel Nchimbi anayepungia mkono wananchi mara baada ya kuhutubia mkutano wake katika kata ya Bombambili Mtaa wa Miembeni akisindikizwa kwa maandamano makubwa yanayoashiria kuungwa mkono kwa CCm. Kata hiyo inakabiliwa na upinzani toka Chadema katiak kiti cha Udiwani ambapo mgombea wake Ken Moto anamtikisa mgombe toka CCM ambaye alikuwa Diwani awamu iliyopita Golden Sanga.
Mtoto huyo hapo juu jina lake halikuweza kufahamika mara moja akiangalia manjonjo ya Dr Nchimbi kumuombea Kura mgombea Udiwani Kata ya Bombambili Manispaa ya Songea Golden Sanga maarufu Sanga One wote ( awapo Pichani) chini toka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club Muhidin Amri na Katibu wa Mbunge huyo Andrew Chatwanga na dereva wao Jogoo eneo la Mjimwema Manispaa ya Songea
Sasa Kazi, Vijana wa IGP Mwema chini ya usimamizi wa Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda wakifuatilia matukio na kulinda usalama wa raia katika mikutano ya mwisho ya kampeni kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010 Siku ya Jumapili, hapa wakivinjari viwanja vya Samora kule kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea.



Mkurugenzi wa Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula nchini, Charles Walwa akistaajabu mahindi yaliyopo nje katika Ghala la wakala huyo lililopo Ruhuwiko Mjini Songea. Mkurugenzi huyo ametangaza nguvu nyingi kuelekezwa vijijini na kuwahakikishia wakulima na wafanyabiashara kununua kiasi chote cha mahindi hata baada ya Uchaguzi. hadi juzi tani 30,000 zimenunuliwa mkoani hapa na kiasi cha tani 20,000 zitanunuliwa kwa mpango mzuri zaidi.



No comments:

Post a Comment