Saturday, October 9, 2010

Mapokezi ya Kikwete CWT Songea na Mahafali ya Shule Luhira

Mwanafunzi wa Shule ya Msingi wasioona na wanaoona luhira manispaa ya Songea akitoka katika Choo iliyojengwa kwa msaada wa Shule ya Trinity-Scotland chini ya usimamizui wa Rev. Martin Mlata was GSM Songea. Mgeni Rasmi katika mahafali ya darasa la Saba Shule ya Msingi Luhira manispaa ya Songea, Rev Martin Mlata, akimpatia cheti mmoja wa wanafunzi Jafua juma Nyumayo jana ambapo Mchungaji huyo aliwaomba wazazi wasiwafiche watoto wenye ulemavu na watumie kamati za shule kutatua matatizo yanayowakabili katika kuendeleza elimu.
Mhe. Rais Jakaya kikwete, anayefungua pazia kuashiria uzinduzi wa jengo jipya la walimu (CWT) Mkoawa Ruvuma huku Rais wa CWT Mwalimu Gratian Mkoba katikati na Prof Jumanne Magembe, Waziri wa Elimu na Mafunzio ya Ufundi wakimwangalia. Jengo hilo lipo Mkabala na Jengo la Saccos ya walimu Mtaa wa Zanzibar Manispaa ya Songea.


Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma, Juma Nyumayo (Kushoto)akisalimiana na Kamanda wa Brigedi ya Kusini (Tembo) Brigedia Igoti, ambaye amerejea toka Masomoni nchini China hivi karibuni.



Maafisa wa Mawasiliano toka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi toka Kushoto, Juma Nyumayo, toka Kituo cha Songea, Magdalena Kishiwa toka Dar es Salaam na wa Mwisho Christian Sikapundwa Mhariri wa magazeti vijijini Kanda ya Kusini wakiwa Uwanja wa Ndege kumpokea Rais Kikwete Oktaba 5, 2010.


Baadhi ya Wafanyakazi waJengo la SACCOS ya walimu Songea Vijijini wakiwa pamoja na Beatrice Sweetbert wa Kagimbo Enterprises Mjini Songea (wa kwanza Kulia aliyeshika kiuno akiwa na shangazi yake mama Julie aliyeshika mfuko wa rambo) wakimsubiri Rais Kikwete katika eneo la tukio la kuzindua na kufungua rasmi Jengo la walimu CWT Mkoa wa Ruvuma Oktoba 5, 2010









No comments:

Post a Comment