Sunday, October 31, 2010

PILIKA ZA UCHAGUZI OKTOBA 31, 2010

Dr. Emmanuel Nchimbi mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini, akipiga kura yake leo saa 1:00 Asubuhi Kituo cha Kupigia Kura- Mateka Manispaa ya Songea kulia ni Msimamizi Msaidizi wa Kituo hicho, Gerwada Kapinga akitoa maelekezo.
Baadhi ya wapiga kura katika Kituo cha Shule ya Luhira Kata ya Mshangano, wakiwa katika Mstari wakisubiri kuingia kupiga Kura. Wakati huo huo Waandishi wa Habari wakitoa matangazo ya Mojakwamoja, Mwenye Suti ni Riporter wa Star TV na Redio Free Africa mkoani Ruvuma, Bw. Adam Mzuza Nindi na anayepiga picha hiyo ni Mpenda Mvula ambapo aliyepachika Camera begani akiwa katika mstari ni Muhidin Amri wa Majira.


Hiyo ni jana wakati kampeni za CCM siku ya mwisho kule Kiburang'oma Lizaboni, Manispaa ya Songea zikiwa zinafungwa rasmi, hapo juu na chini wapambe wakiwa makini kusikiliza sera na midundo ya muziki wa kizazi kipya kuipamba CCM na wagombea wake.














Foleni ya wapiga Kura bila kujali mwanamke au mwanaume eneo la Makumbusho ya Mashujaa ya Vita vya Majimaji Mahenge manispaa ya Songea leo saa 1:15 Asubuhi watu wameitika si mchezo.





Bw. Adam Mzuza Nindi, kwenye Kituo chake cha kupigia Kura Mjimwema Manispaa ya Songea akipokea maelekezo baada ya kukabidhi kitambulisho chake cha kupigia Kura leo majira ya Saa 5:45.










No comments:

Post a Comment