Thursday, October 21, 2010

Siku kenda kuelekea Uchaguzi mkuu! Songea ipo hivi

Hiyo Ramani ya Tanzania, Jimbo la Songea Mjini lipo hapo kwenye mji wa Songea. Wananchi wengi mjini hapa wanamtakia mafanikio na heri katika uchaguzi Mkuu, Mgombea wa CCm Dkt Jakaya M. Kikwete na Ubunge wanategemea atapeta kwa kura nyingi Dkt Emmanuel Nchimbi na kukalia kiti hicho kwa miaka mingine mitano, hayo ni ya Songea.
Hapa Dkt Jakaya Kikwete (Kushoto) akimsalimia Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima nchini, Salum Mnjagila, alipotua Uwanja wa ndege wa Songea, mwishoni mwa mwaka 2009.

Hapa chini Dkt Emmanuel Nchimbi akifurahia jambo mara baada ya kukabidhi Majengo ya Shule ya Sekondari Mkuzo mwaka huu. Aliyevaa joho ni Aliyekuwa Meya wa manispaa ya Songea Mhe. Gerald Ndimbo ambaye sasa anatetea kiti chake cha udiwani Kata ya Ruhuwiko na anayefuatia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea Mjini, Hemedi Dizumba Luambano na kule nyuma ni madiwani awamu iliyopita. Wengi waliopita kwenye kura za maoni CCM.


No comments:

Post a Comment