Wednesday, October 20, 2010

Peramiho na Mlale JKT, wengi mtakumbuka!


Kanisa la Peramiho na minara yake yote miwili hapo juu. Angalia huo mnara wa kulia na saa inayozidi miaka 100 bila kurekebishwa na haijapoteza Majira. Na hiyo picha nyingine chini, inaonyesha kanisa hilo la Peramiho ubavuni ukitokea Trade School upande wa Magharibi na kuelekea Hospitali na ni pale kwenye Mzunguko (Round Obout) Pameboreshwa kwa lami toka pacha ya Mbinga hadi Hospitali.




Kwa wale waliopitia Jeshi, ona picha hii (Katikati) Meja Haniu akiwa na maafisa wenzake toka Kambi ya JKT Mlale, Songea Vijijini. Kambi hiyo ni maarufu sana kwa uzalishaji wa mahindi na mwaka huu wameanza kuzalisha Mbegu za mahindi. Mashamba kule yana majina kama Embakassy nk. Kutokana na kazi nzuri Kambi hiyo ilipendekezwa wapewe trekta kusaidia kuzalisha mbegu bora za mahindi.



No comments:

Post a Comment