Friday, August 13, 2010

WANAHABARI WANAPOKUTANA NA TAKUKURU

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Ruvuma Daudi Masiko, (Kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari wa Mkoa wa Ruvuma kuhusiana na baadhi ya wanasiasa walioshikiliwa kufuatia tuhuma za rushwa wakati wa mchakato wa kura za maoni CCM mkoani Ruvuma. wengine katikati ni Mwanasheria na Mwendesha Mashitaka wa TAKUKURU mkoa Maria Mwakatobe na Bertha madilu Naibu Afisa Elimu kwa Umma Takukuru Mkoa wa Ruvuma.
Kikao hiocho kiliitishwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma Juma Nyumayo kwa lengo la kuwekana sawa katika namna ya utoaji wa taarifa vitendo vya rushwa kutoka taasisi hiyo mkoani hapa na kupata ufafanuzi kuhusu mchakato wa kura za maoni ziloivyoendeshwa na wale waliotuhumiwa na vitendo vya kutoa au kupokea rushwa katika kusaka madaraka.
(Picha na Muhidin Amri--Ndolanga)

No comments:

Post a Comment