Tuesday, August 24, 2010

Wanachama wa Ruvuma Press wakiwa kazini


Baadhi ya wanachama wa Ruvuma Press Club wakiwa kazini ndani ya ofisi ya kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Ruvuma, Bw. David Masiko,(hayupo pichani) Mstari wa mbele toka kushoto ni Emmanuel Msigwa wa Majira, Editha Karlo wa Mtanzania na Juma Nyumayo wa Habarileo. waandishi hao walitaka kujua ukweli kuhusu baadhi magazeti kuandika kukamatwa kwa Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya (Mb) na wapambe wake kwa tuhuma za kuhusika na vitendo vya rushwa wakati wa mchakato wa kura za maoni za CCM mkoani hapa. Jambo hilo lilipingwa vikali na Taasisi hiyo na kusisitiza kuwa waandishi hao waliipotosha jamii kwakuwa wao hawakumkamata isipokuwa walimuita kwa mahojiano. Mhe. Manyanya ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa (MNEC) ni mlezi wa Ruvuma Press Club pia alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Jamhuri iliyoshughulikia uchunguzi wa RICHMOND.

No comments:

Post a Comment