Friday, August 27, 2010

Mkuu wa Mkoa Dkt Ishengoma ashangazwa na viroba!

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt Christine Ishengoma (aliyekaa) akipokea mkono wa Pongezi toka kwa Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari Mkoani Ruvuma ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya UTPC na Mwenyekiti wa Kamati ya Mafunzo na Maadili wa Umoja huo Tanzania Ofisini kwake mjini Songea hivi karibuni. Dkt Ishengoma alishinda katika kinyang'anyiro cha kura za maoni CCM Viti maalum wanawake Mkoa wa Morogoro. (Picha na Muhidin Amri) Picha ya Pili ni Mjasiliamali akiwa amebeba miwa kichwani akitafuta wateja katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani katika eneo la Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni (picha na Muhidin Amri), Picha ya tatu Mkuu w\a Mkoa wa Ruvuma dkt Christine Ishengoma akipokea maelezo toka kwa Meneja wa Wakala wa hifadhi ya Chakula Taifa (NFRA) Richard Mulokozi baada ya kushangazwa kuona mahindi yanahifadhiwa kwenye viroba badala ya magunia. Mavuno ya mahaindi yameongezeka maradufu mkoani hapa hasa kwajili ya usimamizi imara na matumizi mazuri ya mbolea ya ruzuku msimu huu ambapo mkoa ulitumia Pembejeo za zaidi ya Shilingi Bilioni 10.6. (Picha na Muhidin Amri maelezo yote na Juma Nyumayo)





No comments:

Post a Comment