Saturday, September 15, 2012

ZM Mwanamuziki anayetamba Ruvuma arejea toka Dar



Kijana machachari katika kuimba, Zuberi Mohamedi, Maarufu kama ZM, Mwanamuziki wa kizazi kipya anayetamba kwa vibao vikali mkoani Ruvuma (Pichani Kulia ) akiwa na rafiki yake S. Komba ,wakitokea Kituo cha Redio Jogoo mjini Songea kuwafahamisha wapenzi wao kuwa amerejea toka Dar alikokwenda kujifua na kujinoa hadi kuachia Single moja akiwa na nguli wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature.

Hapo akiwa mitaa ya Soko kuu Mjini Songea karibu na NBC Bank Jengo hilo Jeupe kushoto, alipokutana nami akifanya mipango ya kwenda Madaba kusuuza nyoyo za wapenzi wake baada ya kupotea kitambo.

ZM alinishukuru kwakuwa nilimsaidia kumrusha katika Kituo cha TV Tunduru kwa mara ya kwanza na watu kumuona kwenye runinga tangu azaliwe. hayo yalifanyika wakati alipoanza muziki huo miaka ya 2000 mwanzoni. (Picha na Juma Nyumayo)

No comments:

Post a Comment