Saturday, September 15, 2012

DMI wafanya maandamano kuadhimisha siku yao Songea

Shirika la Masista wa DMI, limefanya maandamano makubwa na maonyesho ya Bidhaa mbalmbali mkoani Ruvuma kuadhimisha siku yao hapa nchini.
Masista hao wa madhehebu ya Katoliki wanaojishughulisha na maendeleo ya wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum katika nchi kadhaa barani Asia, Afrika na kwengineko,walifanya maandamano hayo katika mitaaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupita katika Barabara ya Sokoine eneo la Soko la Songea mjini, Ukumbi wa Manispaa Songea na kuishia Viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ambako mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu, aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti, aliyapokea maandamano hayo, kukagua maonesho na kuwahutubia. Jambo jema ni mabango yaliyobebwa na waandamanaji yaliyodai wtoto yatima kupewa elimu, chakula na kusikilizwa. (Picha zote, Maelezo na Juma Nyumayo)


























No comments:

Post a Comment