Wednesday, September 12, 2012

Mtuhumiwa afikishwa Mahakamani, Mkono wa Sheria, haujali Bomu.

Vilio, Simanzi, Maandamano ya wanahabari na wadau wao huenda yakapozwa na hatua ya Mtu anayetuhumiwa kumuua Daud Mwangosi aliyekuwa mwandishi wa Habari wa ChannelTen na Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa Habari mkoa wa Iringa, Tarehe 2, Septemba 2012 kufikishwa mahakamani.

Si Mwingine ni huyo hapo aliyejifunika kichwa chake. Aibu. Ni Aibu kwake.
Bado Jamii ya watanzania wanataka wale waliomtuma kufanya hivyo kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Mkono wa Sheria haujali Bomu.
Unajali ukweli ili utende haki.
(Picha kwa Hisani ya Blogu ya www.francisgodwin.blogspot.com









No comments:

Post a Comment