Friday, September 21, 2012

Wazazi wawajibike kuwatunza wanafunzi waliomaliza Mitihani yao jana

Wazazi na walezi wa wanafunzi waliomaliza mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi hapa nchini jana (20/09/2012 wameombwa kuwalea kwa karibu watoto hao kimaadili wakiwa wanasubiri matokeo ya Mtihani huo muhimu.
Hayo yamesemwa na wanataaluma mbalimbali waliozungumza na mtandao huu wa www.ruvumapress.blogspot.com mjini Songea.
Wamesema licha ya wadau wa elimu kulaumu mtindo uliotumika wa kujibu maswali hata yale ya Hisabati kwa mtindo wa kuchagua, bado Elimu ya watoto hao ipo mikononi mwa wazazi na walezi.
Swala la Elimu bora au bora elimu sasa halina nafasi na kwamba ni muhimu kuitafuta elimu kwa kila namna.
Wanafunzi wengi  wanapomaliza mitihani yao huonekana wamemaliza elimu na kujikita kwenye shughuli ambazo hata umri wao haulingani.

No comments:

Post a Comment