Monday, September 10, 2012

Mandamano ya Waandishi Ruvuma

Habari za kuandamana kwa waandishi wa Habari nchi nzima zimepokelewa na wadau wa habari kwa hisia tofauti mkoani Ruvuma.
Wadau kadhaa waliozungumza na Blogu hii wameunga mkono hatua za waandishi kujitetea dhidi ya nguvu kubwa, ukatili, uonevu na dharau ya kazi za wanahabari wawapo kazini hasa pale wanapowapiga, kunyng'anya vifaa vyao vya kazi na vunjajungu pale alipouawa kinyama Mwandishi wa TV ChannelTen Mkoani Iringa Bwana Daud Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Club ya Waandishi mkoni humo (IPC) kwa kulipuliwa na Bomu akiwa mikononi mwa Polisi ambao walikuwa na wajibu wa Kulinda uhai wake.



PICHA: Waandishi wa Habari wakiwa Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu wakipat hbari za maendeleo ya mkoa huo ili kuhabarisha umma hivi Karibuni


PICHA WALIOPO NA GARI NA MITAMBO: Waandishi wa TBC1 wakiunganisha matangazo ya nje wakati wa Sherehe za Eid El Fitr mara baada ya Kumaliza Mfungo wa mwezi wa Ramadhani Agosti, 2012. Je ni uungwana waandishi hawa kuwatesa, kuwadharau kuwanyanyasa na hata kuwauwa kwa kuwalipua na mabomu kama walivyofanya polisi kumuua kikatili Daud Mwangosi wa Iringa????????PICHA

No comments:

Post a Comment