Monday, March 25, 2013

Kamishna wa Tume Mabadiliko ya Katiba azitaka asasi kusoma rasimu ya Katiba mpya

Maelezo ya Picha ya Kwanza ni Mwenyekiti wa Maboresho na Utetezi Bw. Harold Sungusia, Picha ya Pili ni Kamishna wa Tume ya mabadiliko ya Katiba Bw. Humphrey Polepole, (Mwenye saa Mkononi) Picha ya tatu ni baadhi ya Wajumbe wakiwa kwenye Chumba cha Mkutano hivi karibuni Jijini Dar.



Na Juma Nyumayo, Dar. Kamishna wa Tume ya mabadiliko ya Katiba nchini, Bw. Humphrey Polepole(Pichani juu), amewaomba viongozi wa Azaki nchini kuendelea kutoa elimu kwa wananchi umuhimu wa kusoma Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, na kuisoma Rasimu ya Katiba mpya na kutoa maoni  kupitia Mabaraza ya Katiba yatakayoundwa. Bw. Polepole aliyasema hayo wakati akitoa mada ya Muundo wa Mabaraza ya Katiba katika Ukumbi wa Kituo cha Haki za Binadamu -LHRC- Kijitonyama Dar Es Salaam.
Awali akifungua Mkutano huop amabao uliwashirikisha viongozi toka Mitandao ya mashirika yasiyo ya kisewrtikali ya Mikoa, Mashirika ya Kitaifa na ya Kisekta hapa nchini chini ya Uratibu wa Baraza la Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini NACONGO kwa Ushirikiano na Kituo hicho cha LHRC, Mwenyekiti wa Maboresho na Utetezi, Bw. Harold Sungusia. alisema kila mtu anawajibu wa katika kutengeneza katiba mpya na kuleta mabadiliko.


No comments:

Post a Comment