Saturday, March 23, 2013

Wataka kutoa kafara mtu kisa maji



Jamaa wataka kafara mtu, wapate maji
Na Steven Augustino, Tunduru
KATA ya Namasakata Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma imesema kuwa ipo tayari kutoa kafara damu ya mtu ili kupata maji.
“tupo tayari mtu  achinjwe kwa ajili ya tambiko litakalo sadia Wananchi wa kata yetu kupata huduma ya maji safi na salama,”.
Kauli jiyo ilitolewa na Diwani wa Kata hiyo Mhe.  Masache Ally,  aliye  mwakilisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilayaya Tunduru  Mhe. Faridu Khamisi, ambaye alimweleza Mkuu wa Wilaya hiyo,  Bw. Chande Nalicho, kwamba kauli hiyo ameitoa kufuati Serikali kuwapiga danadana kila wanapo ahidi kuwapelekea huduma za maji safi na salama.
“…sisi wananchi wa kata Namasakata tumejiandaa na tuko tayari kumtoa hata mtu mmoja miongoni mwetu ili auawe kwa kuchinjwa na damu yake imwagike na kutumika kama kafara itakayo fanikisha kupatikana kwa maji na kuwaondolea kero wananch wa vijiji vya Namasakata na Mkasale” alisema Mhe. Diwani Masache.
Akifafanua  kauli hiyo Mhe. Masache alisema kuwa mbali na vijiji hivyo kushirikiana na wataalamu katika utafiti lakini wameishia kuahidiwa kupelekewa miradi ya maji ambayo haijatekelezeka kwa muda mrefu hali inayo wafanya wananchi kukata tamaa na kuhisi labda kuna mkono wa mtu.
Wakizungumzia hali hiyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Namsakata Bw.Yusuf Mkali, na Mkazi wa Kijiji cha Mkasale aliyejitambulisha kwa jina la Nuru Hasani waliosema kuwa Vijiji hivyo vinakabiliwa na hali mbaya ya upatikanaji wa maji tangu mwaka 1982 kiasi cha kutishia maisha ya wakazi wake.  
Walisema,  upande wa Kijiji cha Mkasale hali ni mbaya zaidi kutokana na kuwepo kwa shubiri ambayo huwapata akina mama wanaokwenda kujifungua katika Kituo cha Afya ambapo hulazimika kwenda kuchota maji Mtoni umbali wa zaidi ya Kilometa 2 huku wakiwa katika hatari ya kujeruhiwa ama kuuawa na wanyama wakali ambao pia huyatumia maji hayo kunywa.
Akiongea katika maadhimisho hayo,  Mkuu wa Wilaya ya Tunduru,  Bw. Chande Nalicho, alimtaka Mhandisi wa Idara ya maji Wilayani humo, Eng. Paschal Kidiku,  kushirikiana na wataalamu kufanya utafiti na kutoa majibu ya uhakika kwa wananchi hao ili wajue na kutoa maamuzi ya kukihama kijiji chao ama la.
Awali akisoma risala ya maadhimisho hayo kwa niaba ya Mhandisi wa maji wilaya ya Tunduru,  Eng. Paschal Kidiku,  Bw. Kasim Dinny,  aliye mwakilisha Mhandisi huyo alikili kuwa Vijiji hivyo vinakabiliwa na tatizo hilo kwa kiasi kikubwa na kwamba na kwamba hali hiyo inatokana na maji kupatikana mbali wa kina kirefu hali ambayo inawafanya wataalamu kuumiza vichwa jinsi gani wataweze kulitatua tatizo hilo baada ya miradi ya uchimbaji wa visima 7 kutoa maji kidogo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment