Saturday, August 25, 2012

Tulipokwenda Kutalii Mikumi, Tukajionea wenyewe

Wajumbe wa Bodi ya Union of Tanzania Press Clubs UTPC, Tulibahatika kwenda Mikumi kuona wanyama na vivutio vingine, kwa lugha uliyozoeleka tulikwenda kutalii. Tuliingia pale na gali letu tukalipia pesa kidogo sana. Wanyama tuliowaona na maelekezo tuliyopewa kuhusu wanyama na tabia zao, ulaji, kuzaana, kutengana pia kujilinda kwao, ni maelekezo adimu kupatikanabila kutembelea maeneo hayo na kukutana na wataalamu wanaowafahamu wanyama hao kwa taaluma na kuishi nao miaka nenda rudi. Tulifaidika sana. Rais wa UTPC na baadhi ya wajumbe wa Bodi wametoa wito kwa waandishi na wananchi kutembelea hifadhi/mbuga na Bustani za wanyama hapa nchini kukuz uelewa na kufaidi Maliasili na rasilimali za Taifa.

Picha 1: Alama ya Taifa ni Twiga ambaye tulimkuta katulia akitushangaa wakati tunampiga picha,
Picha 2: Baadhi ya wajumbe mra baada ya kuteremk toka Hiace kwenda Ofisi ya mapokezi hapo Mikumi,
Picha ya Tatu ni mimi Juma Nyumayo kwenye kibao cha Mikumi National Park.




























No comments:

Post a Comment