Sunday, August 19, 2012

Sikukuu ya Eid El Fitr kitaifa Songea - Ruvuma

HALI YA HEWA imebadilika hapa Songea, ni manyunyu ya Mvua yanayoambatana na baridi, hali ya utulivu, waumini wa kiislamu na wakikristu wakipishana kwenye mitaaa kadhaa hapa mjini Songea wakielekea kwenye nyumba za Ibada katika siku hii ya leo ya kumaliza Mwezi mtukufu wa mfungo wa Ramadhani 2012.
Watoto wadogo wakiwa wameshikwa mikono na walezi wao bado pia tunakumbuka, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kumshika mkono Rais wa Malawi Joyce Banda mwishoni mwa mfungo wa Mwezi huu wa Mfungo na kuwahakikishi wananchi wa nchi hizo mbili kuwa hapatakuwa na vita ya kugombea mipaka.
Hapa Songea umetolewa wito kwa waislamu wote nchini kuhakikisha kuwa wanauendeleza uadilifu na mafundisho ya dini hiyo ili kudumisha amani na usalama wa watanzania na majirani zao hpa duniani.

Maombi hayo yalikuwa ni sehemu ya Ibada ya swala ya Idd el fitr ilyofanyika katika Msikiti wa mkoa wa Ruvuma uliopo mjini Songea iliyohudhuriwa na maelfu ya waumini wa Dini hiyo wakiongozwa na mufti wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban Simba na Mgeni Rasmi kitaifa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambunga.

Immam wa Msikiti huo, Sheikh Shaaban Mbaya katika maombi maalum ya kuliombea taifa na viongozi wake wapate afya njema na uwezo wa kuwatumikia watanzania ili wawe na amani, alisema kuwa waumini wa kiislamu hawatakiwi hata kidogo kumbagua muislam au asiye kuwa muislam katika maisha yao ya kila siku.

Alisema, mafundisho ya dini hiyo yana sisitiza upendo na amani ili kuenzi uumbaji wa mwenyezi Mungu, ambaye ni mwingi wa rehema na kwamba viumbe vyote vya ardhi, majini na hewani ameviumba yeye mwenyewe bila ubaguzi kwa manufaa ya viumbe kwakuwa vinategemeana.

Alieleza zaidi kuwa waumini hao wafuate mafunzo toka kiongozi wao, Mtume Muhammad (SAW) ambaye aliweza kuwatunza mayatima na watu wasiokuwa na uwezo kiuchumi ambao wasiowaislamu na waislamu ili wapate furaha ya maisha yao ya kila siku licha ya shida na upweke waliokuwa nao.

"Ndugu waumin haina maana wakati huu wa sikukuuu mkajipamba kwa nguo safi na mkala vyakula vizuri wakati mioyo yenu na matendo yenu hayampendezi mwenyezi mungu," alisema Immam Sheikh Shaaban Mbaya na kusisitiza kuwa ni vyema wakaona umuhimu wa kuendeleza mafundisho waliyoyapata mwezi Mtukufu wa ramadhani kwa manufaa ya watu wote.

Aidha, Sheikh Mbaya alisema, Uchoyo na tamaa za mali, matendo mabaya na uroho wa madaraka na kudhalilisha wengine ndiyo chanzo cha kuvuruga amani iliyopo kuanzia ngazi ya familia, kijiji wilaya taifa na kimataifa.

No comments:

Post a Comment