Monday, August 27, 2012

Sensa, Sensa Makarani wakosa sare Ruvuma, zoezi laendelea














Picha 1: Baadhi ya Abiria wanaosafiri kwenda nje ya Songea wakipanda Gari la Kangaulaya kituo cha Mabasi Songea siku ya Sensa.

Picha 2: Kituo cha Afya Mjimwema Manispaa ya Songea, moja ya eneo litakalo nufaika na matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi 2012 ili kiamuliwe kuwa Hospitali ya Manispaa na kupunguza mzigo kw Hospitali ya Mkoa Songea inayolemewa na wagonjwa hata wale wa nje (OPD)


Picha 3: Gari la Wagonjwa lililotolewa zawadi na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Emmanuel Nchimbi (Picha zote na Juma Nyumayo)







Baadhi ya Makarani wa Sensa Manispaa ya Songea mkaoni Ruvuma, wamekosa Sare za kuwatambulisha.




haya yamejiri mkoani hap na taarifa hii Imethibitishwa na Ofisa Habari w Mkoa wa Ruvuma, Bw. Kasimb alipohojiwa na Mwandishi wa Blog hii ya http://www.ruvumapress.blogspot.com/ mbaye alisema zoezi lenyewe limeanza kwa mafanikio makubwa,






Bw. Kasimba amesema Katibu Tawala wa mkoa wa Ruvuma, Bw Hassan Bendayeko aliweza kutembelea Halmashauri za wilaya ya Namtumbo, Songea Vijijini na Manispaa ya Songea kujiridhisha na uendeshaji wa Zoezi hilo muhimu kwa taifa katika eneo lake mkoani Ruvuma.






Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Saidi Thabit Mwambungu, ameelezwa kuridhishwa na uhesabuji wa wtu katika Sensa ya watu n Makazi lililoanza 26/8/2012 na kuahidi kuifanyia kazi chagamoto ya Makarani kukosa sare, licha ya kuvaa kitambulisho.




Wakati huohuo, Baadhi ya wajumbe wa serikali za Mitaa mkoni hapa wamelalamikia posho ndogo wanayopata kwa kazi hiyo ya kuwaongoza makarani wa sensa katika maeneo yao.



Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mshangano Manispaa ya Songea, Paul Mangwe amesema Wajumbe hao wamelipwa Shilingi elfu nne tu(4,000/=) kwa zoezi lote la sensa.



Amesema wajumbe hao wanaendelea kufanya kazi hiyo shingo upande.



Sensa ya Watu na Makazi ni zoezi maalum lenye lengo la kupata idadi ya watu wote nchini ambapo taarifa zao za Kijamii na Kiuchumi hukusanywa na kuisadia serikali kufahamu mahitaji ya wananchi wa kila rika, mahali walipo na wenye mahitaji maalum.

No comments:

Post a Comment