Thursday, March 4, 2010

Uchaguzi wa Dar City Press Club



Hawa ni baadhi ya wanachama wa DCPC wakiwa na furaha mara baada ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi ambao uliweka historia ya Hamsini kwa hamsini (Fifty Fifty). Mkutano huo wa Uchaguzi Ulifanywa katika Ukumbi wa Habari Maelezo (Kama unavyouona kwa nje hapo pichani) Michael Chatta alichaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha miaka mitano. Nafasi yaMakamu Mwenyekiti imechukuliwa na Benjamin Masese.
Katibu Mkuu ni, Milan Divecha wakati Betty Tesha amechaguliwa kuwa Katibu Msaidizi. Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC, Lucy Ogutu, ameaminiwa na Kupewa nafasi ya Mweka Hazina akisaidiwa na Erodia Petter.
Wajumbe: Jane Mihanji na Beatrice Moses walifungana katika kupatakura nyingi na kuongoza kinyang'anyiro hicho. Wengine ni Samson Kamalamo, Salum Mwalimu, Fatma Nyangasa, Judica Tarimo, Abraham Nyantori na Dorice Lawrence.
Mwenyekiti wa Muda wa Uchaguzi huo alikuwa Shadrek Sagati toka habarileo na Msimamizi alikuwa Mjumbe wa Bodi ya UTPC, Bw Juma Nyumayo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club.

No comments:

Post a Comment