Monday, March 15, 2010

Mambo ya Mkataba Souwasa!

Mkurugenzi wa Souwasa, Mhandisi Fransis Kapongo na Mhandisi Laurent Sechu wa Don Consult Ltd wakibadirishana vitabu vya Mkataba wakiangaliwa na Mwenyekiti wqa SOUWASA Adrian Komba (Kushoto) na Mkurugenzi wa Sajdi & Partners Izzat Sajdi toka Jordan (kulia) Shrehe hiyo ilihudhuriwa na Viongozi wa mamlaka za maji, Viongozi wa Serikali, Waheshimiwa Wabunge na Wakuu wa Wilaya toka wilaya za Songea, Mbinga, Namtumbo na Tunduru. Wahandisi washauri hao watafanya kazi ya kuandaa namna ya kuboresha upatikanaji wa maji katika miji hiyo midogo na Kuboresha Mtandao wa maji Safi na Taka Manispaa ya Songea, kwa Muda wa miezi 12 kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Bilioni 1.2. ambapo watatafutwa wakandarasi kwaajili ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa Muda wa Miezi 18. Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk Christine Ishengoma amewalaumu wananchi wa Manispaa ya Songea kutochangamkia fursa ya kutumia Mtandao wa maji safi na Taka uliopita kwenye maeneo yao.

No comments:

Post a Comment