Katibu Mtendaji wa Tanzania Council for Social Development (Tacosode) amesema ni muhimu kwa wananchi na serikali zao kushirikiana kwa karibu katika kufuatilia Rasilimali za Umma kwa maendeleo.
hayo ameyasema katika Ukumbi wa VETA Mjini Songea wakati akifungua mafunzo ya kujenga uwezo wa jamii wa kufuatilia matumizi ya fedha za umma katika Manispaa ya Songea, Wilaya za Namtumbo, Songea vijijini , Mbinga na Tunduru.
Bibi Kapinga amesema ni jukumu la watu kuhakikisha wanafuatilia mipango na utekelezaji wa shughuli zote kwa njia shirikishi kwani maendeleo ya kiuchumi na kijamii hayatafikiwa iwapo wananchi hawatajua namna ya rasilimali zao zinavyotumika na ushiriki ulivyo.
Washiriki wa mafunzo hayo pamoja na mada mbalimbali wanazojifunza wamevutiwa sana uamuzi wa Baraza la vyama vya Hiari na Maendeleo ya Jamii TACOSODE kwa uamuzi wa kuendesha mafunzo hayo mkoani Ruvuma kwa Ufadhili wa Foundation for Civil Society.
Akielezea umuhimu wa uamuzi huo kwaniaba ya wakazi wa Ruvuma, Katibu wa Mtandao wa Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali wilaya ya Songea SONNGo Bw. Mathew Ngalimanayo alisema Tacosode imechukua uamuzi ambao AZIse nyingi hazijawahi kuthubutu "Tacosode wameanza kuonyesha njia, tunaomba pia mashirika mengine yafuate nyayo ili kuharakisha maendeleo mikoa ya pembezoni," alisema na kumpongezaKatibu Mtendaji Theofrida Kapinga kwa kutoa wito kwa wanaRuvuma kujenga mahoteli mazuri kwaajili ya wageni.
Alifikia hatua hiyo kwakuwa wageni ndio huleta chachu ya maendeleo katika maeneo husika.
Monday, March 29, 2010
RUVUMA WAJENGEWA UWEZO KUFUATILIA FEDHA ZA UMMA
Wednesday, March 24, 2010
Maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu Duniani Ruvuma

Picha ya pili ni Askari wa Kikosi cha 401 KV akiwa tayari kwa kazi iliyoko mbele yake na kuitekeleza kikamilifu. wananchi wametakiwa kuwa kama askari kupambana na magonjwa kama Kifua Kikuu kwa kasi na Mbinu mpya ili kuutokomeza. (Picha na Juma Nyumayo)

Monday, March 15, 2010
Mambo ya Mkataba Souwasa!

Thursday, March 11, 2010
Mambo ya Mganda hayo!
Friday, March 5, 2010
Thursday, March 4, 2010
Mafunzo ya Dhana ya Jinsia TGNP

Mwezeshaji toka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) Beatrice Ezakiel, akisisitiza jambo huku Mwezeshaji mwenza Gloria wa TGNP akimwangalia wakati wa kuwakilisha mada kwa waandishi wa habari, wasanii na Wachora Vibonzo magazetini kuhusu mapinduzi ya Kijinsia na Vugvugu la kumkomboa mwanamke.
(Picha na Juma Nyumayo)
Uchaguzi wa Dar City Press Club


Hawa ni baadhi ya wanachama wa DCPC wakiwa na furaha mara baada ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi ambao uliweka historia ya Hamsini kwa hamsini (Fifty Fifty). Mkutano huo wa Uchaguzi Ulifanywa katika Ukumbi wa Habari Maelezo (Kama unavyouona kwa nje hapo pichani) Michael Chatta alichaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha miaka mitano. Nafasi yaMakamu Mwenyekiti imechukuliwa na Benjamin Masese.
Katibu Mkuu ni, Milan Divecha wakati Betty Tesha amechaguliwa kuwa Katibu Msaidizi. Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTPC, Lucy Ogutu, ameaminiwa na Kupewa nafasi ya Mweka Hazina akisaidiwa na Erodia Petter.
Wajumbe: Jane Mihanji na Beatrice Moses walifungana katika kupatakura nyingi na kuongoza kinyang'anyiro hicho. Wengine ni Samson Kamalamo, Salum Mwalimu, Fatma Nyangasa, Judica Tarimo, Abraham Nyantori na Dorice Lawrence.
Mwenyekiti wa Muda wa Uchaguzi huo alikuwa Shadrek Sagati toka habarileo na Msimamizi alikuwa Mjumbe wa Bodi ya UTPC, Bw Juma Nyumayo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club.
Tuesday, March 2, 2010
Subscribe to:
Posts (Atom)