Saturday, June 5, 2010

Utekelezaji Ilani Dkt. Nchimbi na Dkt. Kamala, meza moja Songea

Na Juma Nyumayo, Songea

ZIARA ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Diodorus Kamala mkoani Ruvuma imemkutanisha meza moja na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati wa kuelezea mafanikio ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa CCM.
Baada ya maelezo Dkt. Kamala alitoa wito kwa WAKULIMA wa Mkoa wa Ruvuma kuleta ushindani katika kuzalisha mazao ya chakula na biashara katika kulikabili soko la jumuia ya Afrika Mashariki.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki , Dkt Diodorus Kamala alitoa wito huo wakati akiongea na wadau wa maendeleo wa mkoa wa Ruvuma katika Ukumbi wa Songea Club Manispaa ya Songea katika siku yake ya kwanza ya kuelezea mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005.
Alisema wakati tunaendelea na ushirikiano wa jumuia hiyo wakulima wa Ruvuma mwanayo nafasi kubwa katika kuzalisha na kuuza mazao yao.
“Urasimu uliokuwepo wa kuuza mazao nje sasa haupo tena, “ alisema Waziri na kufafanua kuwa kikwazo hicho kimependekezwa kuondolewa hivi karibuni katika kikao cha Baraza oa Mawaziri la Afrika Mashariki.
Alisema kuwa soko hilo litasaidia sana kuwapatia kipato wananchi wa mkoa wa ruvuma ambao ni wakulima wazuri wa nafaka na mazao ya biashara kwakuwa soko hilo ni kubwa.
Alizitaja jumuia za nchi za Afrika Mashiriki(EAC), COMESA, SADC zinatarajia kuweka saini mkataba wa soko la pamoja ambao utawawezesha wananchi wanaoishi katika nchi hizo kuopata huduma bora ambazo zitapatikana kutokana na kubadlishana bidhaa na kuweza kudhibiti mfumuko wa bei unaotokana na uzalishaji mdogo wa viwanda vya ndani.
Dk Kamala alisema wakulima wa Ruvuma ambao wameongezewa ruzuku ya pembejeo toka sh billion 3 hadi Sh Bilioni 10.6 katika kipindi miaka mitatu wanafursa kubwa ya kulitumia soko hilo endapo watazalisha kwa wingi na ubora unaohitajika.

No comments:

Post a Comment