Sunday, April 11, 2010

Dkt.Emmanuel Nchimbi awakabidhi Sekondari wananchi!





























(Maelezo ya Picha Dkt. Nchimbi akimkabidhi Ufungua DC wa Songea Thomas Ole Sabaya Picha ya Pili DC Thomas Ole Sabaya akifurahia kukabidhiwa Tuzo ya Uongozi Bora Dunia ( Global Leadership Award) kwa niaba ya wananchi wa Songea, Tuzo hiyo alitunukiwa Dkt. Emmanuel Nchimbi Mbunge na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na kuitoa kwa wananchi wa Songea kwa heshima na upendo wao kumwezesha kufanya kazi iliyoonerkana na kuthibitika kimataifa kuwa yeye ni kiongozi Bora Duniani, Picha ya Tatu wananchi wakiwa katika foleni kungoja wali mweupe na pilau kujichana kufurahia kukabidhiwa shule ya Mkuzo. Mjumbe wa UWT pia Naibu Meya Elizabeth Ngongi, akimkabidhi fedha taslimu zaidi ya Shilingi 200,000 Dkt Nchimbi ya kuchukulia fomu ya kugombea Ubunge Muda ukifika, UWT wilaya ya Songea Mjini imeridhishwa sana na kazi zake Mbunge huyo Msomi Kijana. Picha Mashabiki wa Dkt Nchimbi wakifurahia jambo walipokutana na Msaidizi wake Naibu Waziri, Meja na Aliyesimama amevalia mavazi ya Kijani Sio Mwingine, Ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Songea Mjini Hemed Dizumba akimwaga salamu za CCM kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM uliofanya na Dkt Emmanuel Nchimbi Mbunge wao Picha zote na Juma Nyumayo wa Ruvuma Press)

WANANCHI wa Manispaa ya Songea wamekabidhiwa majengo ya shule ya sekondari ya Kidato cha tano hadi sita yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 112 toka kwa Mbunge wa jimbo hilo jana.
Mbunge huyo, Dkt Emmanuel Nchimbi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika hotuba yake kabla ya kukabidhi shule hiyo alisema ametekeleza ahadi yake kwa wananchi wa Songea ambao kwa muda mrefu walikuwa nyuma katika maswala ya elimu hasa ya sekondari.
" takwimu zinaonyesha wanafunzi darasa la saba waliofaulu ni 1373 lakini waliopata nafasi ya kujiunga na sekondari walikuwa 480 tu," aliwakumbusha wananchi waliohudhuria hafla hiyo huko Mkuzo nje kidogo ya Manispaa ya Songea.
Alijivunia harakati za kujenga shule za sekondari katika kata zte 13 za Manispaa ya Songea na kuruhusu asilimia 100 ya wanafunzi wote 3074 waliofaulu mwaka jana kujiunga na masomo ya sekondari .
" Sekondari kidato cha 1-4 tunazo za kutosha sasa, shule hii itasaidia wanafunzi kidato cha tano na sita," alisema Dk Nchimbi na Kufafanua kuwa itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wasichana na wavulana 400 kwa wakati mmoja na ikikamilika itaweza kuwachukua wanafunzi 800.
Hata hivyo Dk Nchimbi alizitaja changamoto kubwa ambazo amevalia njuga kuzishughulikia ni pamoja na upungufu wa walimu, vifaa na kuboresha majengo na miundombinu ya shule.
"Changamoto nyingine ni kuwalipa haki zao walimu na kujenga chuo kikuu," alisema Nchimbi ambaye alishangiliwa na wananchi wa Manispaa kwa salamu zao jukwaani na sanaa za maonesho.
Nao Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Songea Mjini, Hemedi Dizumba, Meya wa Manispaa ya Songea Gerald Ndimbo na DC wao Thomas Ole Sabaya, wamesema katika hotuba zao kuwa kitendo alichokifanya Mbunge huyo ni cha kijasiri kinachomthibitishia ni msomi aliyetekeleza agizo la Baba wa taifa Marehemu Julius Nyerere kuwa waliopata elimu wawasaidie wenzao.
Mwisho

No comments:

Post a Comment