Saturday, April 3, 2010

Manispaa ya Songea yaanzisha ubinafsishaji shughuli za Afya!


Manispaa ya Songea bila hiyana wala haya imewaalika wadau wake wapatao 300 kuzungumzia kubinafsisha shughuli za kuuweka mji safi. hivi karibuni Mwandishi wa habari Mwandamizi Adam Mzuza Nindi, Katika Safu ya Nionavyo aliandika Makala ya kudorora na kuporomoka kiusafi na kupoteza kabisa maana ya kuitwa Manispaa. Wadau walialikwa wakakutana kwenye Ukumbi wa Songea Club wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya Thomas ole Sabaya, watu maarufu, watendaji, wafanyabiashara, wakuu wa taasisi zote na Mashirika ya dini yote walielekezwa nini cha kufanya na kusikiliza mada na matokeo ya tafiti za kutoka kule Manispaa ya Morogoro. Pichani Afisa Mipango Miji na Mratibu wa Mpango wa Uendelezaji wa Miji na Usimamizi wa Mazingira(UDEM) Edward Alfred Kandonga, akitoa mada mbele ya washiriki hao 300.

No comments:

Post a Comment