Friday, November 16, 2012

Shirika la Kuhudumia wazee PADI lapata Tuzo

Na Juma Nyumayo, Dar

KATIKA hali ya kutia moyo na kuridhishwa kiutendaji, Shirika la Tanzania Mission To tha Poor and Disabled (PADI) lenye makao yake makuu, Mjini Songea mkoa wa Ruvuma limepata Tuzo likiwa ni Mshindi wa kwanza katika kuwahudumia watu hasa wazee na kusukuma mambo ya kisera serikalini.
Kabla ya ugawaji wa Tuzo hizo maelezo yalitolewa na viongozi wa The Foundation for Civil Society, na akaombwa Mgeni rasmi wa hafla hiyo kutoa Tuzo hiyo.
Tuzo hiyo si zwadi kwa Mtendaji Mkuu wa PADI Bw. Iskaka Msigwa na watumishi wenzake bali kwa Mashirika yote ya Mkoa wa Ruvuma, Serikali, wazee wenyewe na watu wote wa Songea ambao wamethibitishiwa kuwa kazi za PADI zimekubalika hapa nchini
Hongera PADI,

No comments:

Post a Comment