Tuesday, November 15, 2011

TGNP ndani ya Ruvuma kiutafiti zaidi









Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP, wapo mkoani Ruvuma kwa utafiti kuelewa ni kwa kiasi gani vyombo vya habari vimecangia katika kutangaza na kusambaza habari kupitia kampenina harakai za Ukombozi wa mwanamke Kimapinduzi katika Mkoa wa Ruvuma.
Utafiti huu unaoumia mbinu za kukusanya taarifa kwa madodoso, majadilianao,kazi za vikundi, maswali ya uchokozi na Uchambuzi wa pamoja inawashirikisha washiriki wa semina zilizowahi kuendeshwa na TGNP mkoani Ruvuma katika Makundi matatu.
Makundi hayo ni Waheshimiwa Madiwani viti Maalum wa Manispaa ya Songea, washiriki toka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya wanawake na waandishi wa habari.
Utafiti huu unaoshirikisha zadi yawatu 30 unaongozwa na Bw. Badi Darusi toka TGNP makao Makuu Dar es Salaam, ambapo pichani anamuelekeza Judith Lugoye wa Ruvuma Press Club namna ya kutuma picha katika mitandao mbalimbali.
(Piha na maelezo Juma Nyumayo)