Tuesday, January 21, 2014

HABARI KATIKA MITANDAO YA KIJAMII



Mkurugenzi wa Demashonews Hamza Juma (Kushoto) akisikiliza maelezo toka kwa Mkurugenzi wa Jamii ya WanaRuvuma, Juma Nyumayo kuhusu mikakati ya kuwahabarisha wananchi kwa kutumia mitandao ya kijamii hivi karibuni.
 

Tuesday, January 14, 2014

MUFTI AWATAKA WAISLAMU KUACHA KULALAMIKA

SHEKHE Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba, ametaka Waislamu kuacha kulalamika, kwamba Wakristo wamekuwa wakipewa upendeleo, badala yake watumie fursa wanazopata kuondokana na malalamiko hayo. 

Akizungumza katika maadhimisho ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW), yaliyofanyika kitaifa mkoani Kigoma jana, Mufti Simba alisema chanzo cha malalamiko hayo ni Waislamu kushindwa kujitolea katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Akitoa mfano, alisema Waislamu wanapaswa kupeleka watoto wao kusoma elimu zote mbili na kuwaandaa kushika nafasi za kiutendaji ambazo wanalalamikia kuwa zimetolewa kwa upendeleo kwa Wakristo.

Alisema hata katika kukamata maeneo ya uwekezaji, Waislamu wamebaki nyuma kutokana na kushindwa kujitolea kuchangia fedha za kutosha za kuanzisha miradi ya maendeleo kwa ajili ya kuimarisha dini na kuendesha maisha yao.

“Msilalamike, tunisheni mifuko katika misikitini yenu muwe na fedha za kutosha zitakazokuwa kichocheo cha ninyi kushiriki katika shughuli muhimu za kiuchumi. Kosa ni lenu, msilalamikie Wakristo hawana tatizo hata kidogo katika hilo,” alisema Mufti Simba.

Madaraka misikitini Mjumbe wa Baraza la Ulamaa la Taifa, Ally Mkoyogore, alitaka Waislamu kuongeza bidii katika elimu na uchumi, badala ya kutumia muda mwingi kupigania madaraka misikitini.

Alisema kurudi nyuma kwa Waislamu, kunasababishwa nao wenyewe kushindwa kufuata maadili na misingi ya dini yao, badala yake wanagombea uongozi misikitini kwa ajili ya maslahi binafsi.

Maadhimisho hayo ya Maulid yalihudhuriwa na viongozi wa dini kutoka mikoa mbalimbali nchini, mashekhe kutoka Burundi huku Serikali ikiwakilishwa na Mkuu wa Mkoa Kigoma, Issa Machibya.

Mshikamano Akizungumza katika mkesha wa Maulid usiku wa kuamkia jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Rais mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alitaka Watanzania kujenga mshikamano kwa kusikilizana na kuvumiliana, kwa lengo la kudumisha tunu ya amani na utulivu iliyodumu kwa miaka mingi sasa nchini.

Katika salamu zake za siku hiyo, Alhaji Mwinyi alisema dini zote ukiwamo Uislamu, hazikatazi waumini kushirikiana katika masuala mbalimbali, hivyo ni wajibu wa kila upande kuusikiliza mwingine.

“Nchi zinaijua Tanzania kuwa kisiwa cha amani kisicho na utofauti wa dini, kabila wala rangi. Sote ni ndugu wamoja, tunapaswa kuendelea kuishi kwa usalama na amani.

“Pale inapotokea hali ya kutofautiana, tukae pamoja na kuzungumza ili tufikie mwafaka na si kugombana,” alisema Mwinyi.

Alisema Mtume aliongoza dini kwa kuhubiri mshikamano, kupenda wengine na kuthamini utu na si vurugu kama ambavyo wengine wanadhani.

Akimkaribisha Mwinyi kutoa salamu hizo, Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salumu, alisema amani na utulivu nchini ndio ujumbe wa sherehe hizo na kukumbusha Watanzania kuishi kwa umoja na kuwa watu wa Taifa moja lisilo na uvunjifu wa amani.

Kutokana na umuhimu huo, Shekhe Alhad alisema ndiyo maana sherehe hizo zikapewa kaulimbiu ya ‘Uislamu ni amani kwa wote’ lengo likiwa kukumbusha wanaofikiri kuwa misingi ya dini hiyo ni vurugu na kuhatarisha usalama au kujenga uadui kwa watu wengine.

Katiba mpya Shekhe Alhad pia alimpongeza tena Rais Kikwete kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa mchakato wa Katiba mpya ambao hivi karibuni utaingia katika hatua ya uundwaji wa Bunge Maalumu.

“Kama ni safari basi tayari mchakato wa Katiba umevuka Nungwi na karibu unaingia bandarini. Ni jambo la kumpongeza kwa sababu si mataifa yote yangeweza kufika hadi hapa tulipo bila vurugu, ila sisi tumeweza na hata pale palipotokea changamoto fulani, alikabiliana nazo,” alisema Shekhe Salum.

Alisema ni vema Watanzania wazidi kumwombea kiongozi huyo ili akamilishe salama mchakato huo na kumalizia muda wa uongozi na kumkabidhi mtu mwingine kuongoza Taifa. Miongoni mwa wageni waliokuwepo ni Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia. 

source: jumamtanda Blog

Monday, January 13, 2014

USIPITWE NA SOMO TOKA KWA SOPHIE LUCAS, SOMA HAPA

  1. Katika kijiji cha Matare wilaya ya
  2. Mugumu Serengeti, bwana
  3. Wambura alikamatwa kwa kesi ya
    kusingiziwa na kuhukumiwa kwenda
    jela miaka mitatu.
  4. Huku nyuma akiacha mke na
    watoto wanne waliokuwa
    wanasoma. Hukumu hiyo ilimtesa
    sana kichwa chake, alitamani kila
    mtu anayemhisi kuwa ana makosa...
    aingie katika moyo wake na
    kuupata ukweli.
    Alilia na umaskini wake, lambda
    angepata wakili mzuri angeweza
    kumtetea, kumkosa wakili
    kukahalalisha kifungo hicho!!
    Alikwenda gerezani huku akiumia
    sana rohoni. Aliyaanza maisha
    mapya kwa shida sana, akawa
    mnyonge kila mara na mwili
    ukapoteza afya kiujumla.
    Huko gerezani alifanikiwa kupata
    rafiki aliyekuwa na cheo ama
    jukumu la uzikaji wa wafungwa
    hasahasa ambao hawakuwa na
    ndugu ama ambao ndugu zao huwa
    hawajitokezi pale gerezani.
    Mzikaji alijaribu sana kumtia nguvu
    Wambura na kumwaminisha kuwa
    hiyo ilikuwa hatua tu ya maisha
    anapaswa kuizoea na siku moja
    ukweli utajulikana tu! Bwana
    Wambura maneno ya mzikaji
    hayakumuingia kabisa.. alizidi
    kunyong’onyea.
    “Siwezi kuvumilia kukaa gerezani
    miaka mitatu…..kama unajali kilio
    changu nisaidie nitoroke kwa
    namna yoyote ile ndugu yangu!!”
    Wambura alimsihi mzikaji.
    SIKU MOJA mzikaji akamwambia
    Wambura kuwa msaada
    umepatikana. Lakini yataka moyo!!
    “Nipo tayari kwa lolote ilimradi tu
    nitoke humu!!” alijibu kwa msisitizo
    huku akimtegea sikio mzikaji.
    “Msaada pekee wa kukutorosha
    humu ndani ni kwa njia ya jeneza…
    yaani mfungwa akifa mimi
    nakuunganisha naye kwenye
    jenerza…..” akashusha pumzi kisha
    akaendelea “Wewe ukisikia kengere
    ya msiba, njoo mara moja kwenye
    chumba cha maiti, utakuta tayari
    sanduku liko katikati ya chumba
    linakuwa halijafungwa, funua
    kifunioko ingia ndani yake ulale
    pembeni ya maiti kwani sanduku
    huwa kubwa la kutosha kila aina ya
    maiti na hata miili miwili inaingia.
    Kisha nitakuja na kulipigilia
    misumari. Baada ya muda
    tutalipakia kwenye gari na kutoka
    kwenda nje ya gereza makaburini
    nikiongozana na baadhi ya
    wafungwa na maaskari magereza.
    Tutakuzika huko lakini baada ya
    dakika 20 hadi 30 nitarudi
    kukufukua. Hautaweza kushindwa
    kupumua kwa dakika hizo, utatoka
    ukiwa huru.”
    JAPOKUWA wazo lilikuwa zuri lakini
    lilimtisha sana Wambura. Hata
    hivyo akaona afadhali afanye hivyo
    kuliko kukaa gerezani miaka mitatu
    bila kosa.
    Siku moja akasikia kengere ya
    msiba. Akafanya kama
    alivyoelekezwa na mzikaji. Akaenda
    na kuingia chumba cha maiti. Kweli
    akalikuta sanduku, akiwa na hofu
    kuu akaingia na kulala pembeni ya
    maiti iliyokuwepo. Mara akasikia
    mtu ameingia na kulipigilia
    msumari sanduku. Muda mfupi
    baadaye sanduku likainuliwa na
    kuwekwa kwenye gari.
    Gari ikatoka nje ya gereza hadi
    makaburini. Sanduku likashushwa
    na kuwekwa kaburini na kuanza
    kufukiwa.
    Wambura alijitahidi sana kuvumilia
    japo hofu ilizidi kutanda.
    Alimtegemea sana mzikaji na
    alianza kumuona mkombozi wa
    maisha yake.
    Kama alivyoambiwa, akasubiri
    dakika kumi, ishirini.. zikapita
    kimya!!
    Dakika thelathini kimya. Joto nalo
    likazidi kuongezeka.
    “Nitavumilia hadi afike…”
    alijisemea kisha akajiongezea kauli
    ya ujasiri.
    “Kama nilitakiwa kuishi gerezani
    miaka mitatu kivipi dakika kadhaa
    za hapa kaburini”
    KWA kuwa alishakaa gerezani kwa
    muda kiasi akatamani kujua
    aliyekufa ni nani… ni kwewli
    aliogopa kuitazama maiti lakini
    aliona kama inatisha zaidi ikiwa
    imefunikwa vile kuliko ikiwa wazi.
    Akaifunua upande wa usoni… Kwa
    kuwa kulikuwa na giza nene
    alikodoa sana macho kuitazama.
    LAHAULA!!! MACHO YAKAKUTANA
    NA SURA YA MZIKAJI!!!
    MZIKAJI ALIKUWA AMEKUFA NA
    AMEZIKWA NA AHADI ZAKE ZA
    UKOMBOZI!!
    ________________
    FUNZO::
    Usimtegemee sana mwanadamu
    katika maisha yako, kwanza ni
    dhambi!!
    Pili mwanadamu anakumbana na
    vikwazo kama unavyokumbana
    navyo wewe hadi kumwendea yeye.
    Hivyo kumpatia maisha yako ni
    kuzidi kuyaweka hatarini zaidi!!
    Umeonewa umesingiziwa
    unanyanyaswa….. mwachie Mungu
    afanye maamuzi…
    _______________
    Haya mzikaji aliyetegemea
    atamfukua naye ni maiti…… tazama
    mateso atakayoyapata hadi kufa
    kwake…..
    Bila shaka atatamani kurudi
    gerezani kwa miaka mingine kumi
    lakini haitawezekana tena!!!

Thursday, December 26, 2013

Mwanahabari Mkongwe Adam Mzuza Nindi afunguka


Mwanahabari Mkongwe, Mwakilishi wa Radio Free Africa na Star TV Mkoani Ruvuma, Bwana Adam Mzuza Nindi,  Amefunguka na tathimini ya kazi katika Blogu 
Haya hapa chini ndiyo Maneno  yake na picha hapo juu alipost katika Blogu yake ya : www. songeahabari.blogspot.com
  
Uchunguzi wa Habari za kuwa wafaa wananchi ni mhimu sana ,Hebu Tuone sasa tuna Maliza Mwaka yepi mazuri yaliyo fanywa na Wandishi wa Habari na Yepi mabovu yaliyo fanywa na Waandishi wa Habari. Tujitathini wenyewe tusipige katumba kuonyesha vidole kwa wenzetu Pale tulipo kosea tuji sahihishe na Pale tulipo fanya vizuri tuboreshe zaidi Bado siku chache za kumaliza Mwaka lakini lazima Waandishi Tujipange Hapo ni Mwandishi Mwandamizi Juma Nyumayo (aliyesimama) akiwa na Mkongwe wa Habari Adam Mzuza Nindi wakitathiminji mwaka 2013

Wednesday, December 18, 2013

LAKE OIL LTD KUFUNGUA MAUZO YA MAFUTA SONGEA

Mtumishi wa lake Oil Ltd, Bw. Moses Clemency, akiwa mbele ya moja ya Pampu mpya za mafuta katika Kituo hicho kilichopo eneo la Manzese, Manispaa ya Songea.

KAMPUNI ya mafuta Lake Oil Ltd ya Dar es Salaam, imefungua Kituo cha mafuta Manispaa ya Songea.

Kituo hicho kilichopo Mkabala na Ofisi za Zimamoto na kuangaliana na Soko la Wakulima Manzese mjini hapa, kimebadili Sura ya eneo hilo kutokana na Ukarabati na kujenga paa kubwa katika Pampu mpya za mafuta aina ya Diesel, Petroli na ya taa.

Kwa Mujibu wa Meneja wa Kituo hicho, Bw. Daud Mmasa Sevuri, alisema kuwa huenda Alhamisi wiki hii wakaanza kuuza mafuta kwa bei nafuu wakilinganisha na vituo vingine mjini hapa.
"Alhamisi wiki hii tunatarajia kuanza kuuza mafuta hapa songea," alisema.

Ujio wa Kampuni ya Lake Oil Mkoani hapa, utaongeza ushindani wa Biashara ya mafuta ya mitambo na Gas kwa matumizi mbalimbali na kusaidia kusukuma maendeleo ya sekta ya kilimo, madini, usafiri na utoaji huduma.

Mkoa wa Ruvuma haujaunganishwa na Umeme Grid ya taifa hivyo kuufanya kutegemea zaidi mafuta.
Kilio kikubwa cha wakazi wa mkoa huu kitabaki kupata wakala wa kuuza mafuta ya ndege.
Angelipatikana wakala huyo Uwanja wa ndege ulioko eneo la Ruhuwiko manispaa ya Songea, wenye ubora wa kutua ndege mbalimbali isipokuwa Boeng,  ungeweza kutumika ipasavyo kwa abiria na kupunguza gharama ya nauli wanayolipa sasa kwa kutumia ndege ndogo.

Tuesday, December 17, 2013

WABUNGE 160 WA CCM WALIA NA MAWAZIRI MIZIGO

Ukumbi wa Bunge, Dodoma
                                  DODOMA/DAR ES SALAAM.                                                                                                                                                                                                                                                                    WABUNGE 160 wa CCM wamejiorodhesha kuomba kuitishwa kwa kikao cha Kamati ya Wabunge hao kwa lengo la kuwajadili mawaziri wanaotajwa kuwa mizigo.

Pia wabunge hao wanataka Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahaman Kinana naye awepo kwenye kikao hicho.
Mjumbe wa Kamati ya Uongozi wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Hussein Mussa Mzee, alimwambia mwandishi wetu kuwa wamepokea barua iliyoambatana na orodha ya majina ya wabunge zaidi ya 160 waliotia saini kutaka kuitishwa kwa kikao hicho.
“Hata kama wangesaini wabunge 10 tu tungeitisha kikao. Bahati nzuri walisaini zaidi ya 160, kwa hiyo kikao kitaitishwa kwa kuwa ni haki yao kikanuni kutaka kukutana,” alisema.
Alipoulizwa kwa nini kikao hicho hakikuitishwa ndani ya wiki moja ambao ndiyo muda wabunge hao walioutaka kabla ya Kamati Kuu ya CCM kukutana wikiendi iliyopita, Mzee alisema hiyo lilitokana na Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kutokuwapo bungeni.
Mzee alisema pia kikao hicho kilishindwa kufanyika mara ya kwanza kutokana na Kinana kuwa safarini Afrika Kusini ambako alihudhuria mazishi ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Hata hivyo, alisema hawezi kujua ni lini kikao hicho kitafanyika lakini aliahidi kuwa itakuwa mara baada ya Kinana kurejea nchini.
Wiki iliyopita, gazeti hili liliandika kuhusu wabunge wa CCM kujiorodhesha ili kushinikiza kufanyika kwa kikao hicho.
Chanzo kimoja cha kuaminika kilisema kuwa fomu hiyo iliwasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa Wabunge wa CCM ikiambatana na barua inayotaka kuitishwa kwa kikao kitakachowakutanisha.
“Tuliwaomba waitishe kikao cha wabunge wa CCM ili mawaziri ambao tunawaona hawatimizi majukumu yao kikamilifu waweze kuhojiwa lakini wakawa wanasuasua,” kilisema chanzo hicho.
Kikao hicho kilitakiwa kufanyika Alhamisi iliyopita ili kuwahoji mawaziri hao kabla ya kikao cha Kamati Kuu.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikaririwa wikiendi hii akieleza kuwa mawaziri saba walihojiwa katika kikao cha Kamati Kuu na kumuachia Rais Jakaya Kikwete jukumu la kuamua kuwafukuza kazi, kuwahamisha au kuwataka kutekeleza majukumu yao kikamilifu. MWANANCHI

Monday, December 16, 2013

Simulizi ya Mandela

Toka kulia: Rais wa sasa Afrika kusini, Jacob Zuma , Rais wa kwanza mweusi wa Afrika kusini,  Mzee Nelson Mandela (enzi ya uhai wake) na Rais wa pili wa Afrika Kusini,  Thabo Mbeki

Ndugu Zangu. 
Nahitimisha simulizi za Mzee Wetu Madiba. Najisikia nimechukua jukumu langu la kugawana nanyi kile kidogo nilichoweza kukusanya kumhusu Mzee wetu Madiba.


Natumaini nitapata muda siku zijazo, nisimulie zaidi juu ya yale yenye kufanya maisha ya Madiba kuwa simulizi endelevu kwetu Waafrrika na watu wa dunia. 


Lakini, ukweli unabaki, kuwa leo dunia imemzika Mzee Madiba kijijini kwao Qunu. Yaliyobaki nyuma yake ni yale mema aliyoishi akayahubiri. Nasi tunapaswa kujifunza kutoka hayo.
Yumkini Mungu amechagua kupumzisha Mandela wakati muafaka. Maana, ni katika kipindi ambacho, Afrika Kusini inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani.



Chama kikuu cha ANC kinakabaliwa na changamoto za ndani ya chama na kwenye jamii. Kinapaswa sasa kijiandae kufanya mabadiliko makubwa yatakayorudisha imani ya wapiga kura wake wengi. Wapiga kura ambao wameanza kukata tamaa. Hawana furaha ya maisha yao. Wamekata tamaa ya kuona kuwa kesho yao yaweza kuwa bora zaidi.



ANC kihistoria imekuwa ikitegemea sana Jumuiya yake ya Vijana na Shirikisho la Wafanyakazi ( Cosatu) Jumuiya zote hizo zinaonekana kugawanyika. Kuna wanaoipa mgongo ANC. 


Na Mandela anausia; 
" The leader must keep the forces together, but you can't do that unless you allow dissent. People should be able to criticise the leader without fear of favour. Only in that case are you likely to keep your colleagues together"- Nelson Mandela. It is when Mandela gave a piece of advice to newly elected Party Leader, Thabo Mbeki at the ANC Congress in Mafikeng, 1997. 



Kwamba kiongozi unapaswa kuyaunganisha makundi, lakini, huwezi kufanya hivyo kama huruhusu sauti kinzani. Sauti za wenye kukupinga. Watu wawe huru kumshutumu kiongozi bila ya woga. Ni kwa namna hiyo tu kiongozi unaweza kuyaunganisha makundi. Mandela aliyasema hayo kule kwenye Mkutano Mkuu wa ANC uliompitisha Thabo Mbeki kuwa Rais wa ANC, ni mwaka 1997. 

Naye Askofu Desmond Tutu alipata kusema; 
"Kuna tofauti ya kimsingi kati ya kuwa huru na kuwa katika hali ya kukandamizwa. Kuwa huru ni pamoja na kupata huduma za msingi za kijamii, kuwa na ajira, maji ya bomba, umeme, makazi bora na huduma za msingi za afya. Kuna maana gani basi ya kuwa huru wakati ubora wa maisha ya watu haujaimarishwa? Kama sivyo, hata kura nazo hazina maana yoyote!" (Desmond Tutu- William Gumede; Thabo Mbeki And The Battle For The Soul Of The ANC, Uk. 67). 

Nkosi Sikelel i Afrika


Kwa hisani ya Juma Mtanda