Tuesday, October 25, 2011

Maskini Gaddafi ! Soma hapa













OOOH! GOD!





The bodies of the Libyan leader, Muammar Gaddafi, his son Mutassim and a former aide have been moved from a commercial freezer in a warehouse area of Misrata in anticipation of burial, according to a security guard.
Ibrahim Beitalmal, a local military spokesman, said the burial was likely to take place on Tuesday. He said the three men would be interred in unmarked graves in a secret location to avoid vandalism.
Asked about the removal of the bodies from the freezer, he said he was unaware of the process of burial getting under way.
However, Salem al Mohandes, a security guard at the warehouse complex, said the bodies were moved late on Monday from the freezer, where they had been on display for the past four days.
"Our job is finished," al-Mohandes said. "[Gaddafi] was transferred and the military council of Misrata took him away to an unknown location. I don't know whether they buried him or not."
An Associated Press Television News team saw three vehicles leave the warehouse area late on Monday. The team then entered the freezer and found it empty.
An official from the National Transitional Council (NTC) said Gaddafi's (just like Thomas Sankara, Patrice Lumumba and Che-Guevara) burial will be in a secret desert grave.
'Loyalists executed'
The developments came as the New York-based rights group, Human Rights Watch (HRW), warned of a "trend of killings, looting and other abuses" by those who had fought against Gaddafi.
HRW said it had found 53 decomposing bodies, apparently Gaddafi loyalists, in Sirte, and that there were indications they may have been executed by revolutionary forces supervised by NATO.
The bodies were found on the lawn of the abandoned Mahari hotel, and some had their hands bound.
Peter Bouckaert, a researcher for HRW, said the hotel had been under the control of NTC fighters from Misrata before the killings took place.

The condition of the bodies suggested that the men had been killed between October 15 and 19, HRW said.Bloodstains on the grass and spent cartridges indicated that some were shot and killed at the spot they were discovered.
"This latest massacre seems part of a trend of killings, looting, and other abuses committed by armed anti-Gaddafi fighters who consider themselves above the law," Bouckaert said in a statement.
NTC fighters in Misrata, a city that had been besieged by Gaddafi's troops for weeks earlier this year, had no immediate comment.
The US state department termed the report "extremely disturbing".
Gene Cretz, the US ambassador to Libya, had "raised it with the National Transitional Council today and asked them to conduct a full investigation", according to a state department spokesperson.
Inquiry ordered
Earlier, the NTC ordered an investigation into the death of Gaddafi after international pressure to examine the circumstances surrounding his death.
A commission of inquiry is being put in place to investigate the killing of Gaddafi, who was captured by NTC fighters outside Sirte on Thursday and shot shortly afterwards, apparently while being transported to Misrata.
"In response to international calls, we have started to put in place a commission tasked with investigating the circumstances of Muammar Gaddafi's death in the clash with his circle as he was being captured," Mustafa Abdel Jalil, the head of the NTC, said in Bengazi on Monday.Abdel Jalil who is currently working as a puppet for NATO and US also announced that the process of forming a new interim government was already under way, and would be completed "within two weeks".
He said all Libyans "wanted to try [Gaddafi] for what he has done to them. From executions, to imprisonment, to throwing away the Libyan wealth ... or using that wealth against the Libyan people".
The NTC has insisted their lies to Africans and the whole world that Gaddafi was killed in "crossfire" between NTC fighters and pro-Gaddafi loyalists after his capture from a drainage pipe outside his hometown of Sirte.Some members of the NTC, as well as of the international community, have expressed doubt over this version of events.
The US, Britain and international rights groups have all called for an investigation into how Gaddafi was killed in what appeared to be one of the final acts of Libya's eight-month civil war.
Critics have also said that the fact that Gaddafi's body, along with that of his son Mutassim, was put on display raises questions about the NTC's commitment to the rule of law.
Abdel Jalil has said Gaddafi may have been killed by his own loyalists in order to escape being implicated by him in any trial.
"Some people may have wanted him to have been tried to extend their feeling of relief at his downfall," he said."Free Libyans wanted Gaddafi to spend as much time in prison as possible and feel humiliation as much as possible.My TakeWhatever those who refer themselves as free Libyans think might be, there is one thing they are not aware of. That they are going to be humiliated for the rest of their lives for allowing themselves to become a new Imperialist Colony. For him Abdel Jalil his prize is to become a new proxy symbol of new Libyan leadership whilst is a puppet just like Savimbi and Mobutu whom Imperialists used them during cold war. Abdel Jalil was a former minister for Gaddafi regime who made a deal to become a Western dog in order to get power and wealth.

Friday, October 21, 2011

Maskini kijana huyu! Ona kipondo hicho.

Kijana huyo alipata mkong'oto katikati ya Mji wa Songea baada ya kutuhumiwa kumuibia mama mmoja msafiri. Baadaye kijana huyo alipelekwa polisi kituo cha kati na karandinga la polisi. (Picha na Muhidin Amri)

Wednesday, October 19, 2011

AHIMIZA HAKI ZA BINADAMU

MKUU WA MKOA AHIMIZA WANANCHI KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU
Na Stephano Mango,Mbinga
WANANCHI Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wametakiwa kuheshimi haki za binadamu kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria ili kila mtu aweze kuishi kwa amani na upendo katika jamii yake na nchi kwa ujumla
Wito huo umetolewa jana kwenye Viwanja vya Magereza Kitai na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu mara baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyosomwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shaib Mnunduma
Mwambungu ambaye yupo kwenye ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Mbinga alisema kuwa kila siku ninaposoma taarifa ya maendeleo ya mkoa nakutana na taarifa ya vifo vya kujinyonga,kupigana,kuchinjana kutokanana na mahusiano ya kimapenzi na matatizo mengine ya kijamii na kwamba takwimu za vifo vingi vinatoka Wilaya ya Mbinga
“Nasikitishwa sana na taarifa hizo kwani mtu unayempenda huwezi kumuua kwa sababu za kukunyima penzi au kumkuta mpenzi wako na mwanaume mwingine au na mwanamke mwingine hivyo kama kweli unampenda utamlinda na vishawishi vinavyoweza kupunguza upendo wake kwako na sio kumuua”alisema Mwambungu
Alisema kuwa haki ya kuishi ni haki kubwa kuliko zote na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuondoa uhai wa mwenzake kwa sababu yoyote ile kwani mwenye uwezo na mamlaka hayo ni mwenyezi mungu pekee yake ni vema kazi yake tukamuachia
Alisema kuwa jambo hilo halipaswi kuvumiliwa hata kidogo hivyo ni vema viongozi wa dini na wakijamii pamoja na Serikali kushirikiana kikamilifu kudhibiti jambo hilo kwani kabla vifo havijatokea kunakuwepo na dalili za kutokuwa na amani miongoni mwa wapenzi hao tujaribu kusuluhisha migogoro kwa taratibu za mila na desturi na kwamba ikishindikana basi sheria itumike kudhibiti vifo hivyo
Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Mbinga Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Shaib Mnunduma alisema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 Halmashauri imekadilia kutumia Tsh 39,600,654,467.00 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na shughuli za utawala
Mnunduma alisema kuwa vipaumbele katika kutekeleza bajeti hiyo ni kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kufikia lengo lililopangwa,kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kufanya ukarabati wa Zahanati,Vituo vya Afya,Kupanua Hospitali ya Wilaya na kuhamasisha ujenzi wa Zahanati kwenye kila Kijiji
Aliitaja miradi mingine ni kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara,kuimarisha sekta ya mikopo kwa kuendeleza vyama vya kuweka na kukopa9Saccos),kufanikisha adhima ya kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu elimu ya msingi kujiunga na elimu ya sekondari
Mnunduma aliongeza zaidi kuwa miradi mingine ni ya kuboresha huduma za jamii na kusaidia miradi iliyoibuliwa kwa mbinu shirikishi jamii hasa ile ya elimu,afya,kilimo,maji na barabara na kuimarisha shughuli za hifadhi ya mazingira na hasa upandaji miti,kuzuia uchomaji moto misitu na kuhamasisha kilimo cha ngoro na makinga maji
MWISHO

Tuesday, October 11, 2011

Vibaka wanaoiba viporo vya wali wapungua



Hakika Songea ina mambo! leo nimetembelea maeneo ya Matarawe hapa Songea Mjini, na kuambulia hadithi hii hapa chini! Hongera zake RPC Kamuhanda Pichani










Eti wakazi wa eneo hilo wanashangilia kupungua kwa vibaka ambao Usiku huingia majumba ya watu na kula vipolo vya wali. wakazi wa eneo hilo wanasema wanashukuru sana falsafa ya ulinzi shirikishi au kwa jina maarufu Polisi Jamii chini ya Kamanda wa Polisi Michael Kamuhanda kuwa sasa vibaka hao wamepungua.

Mkazi mmoja kaniambia pia eti Yeboyebo yaani Pikipiki zinazosafirisha abiria zimesaidia kutoa ajira na kuwafanya vijana wengi kuacha wizi wa viporo vya wali au ugali majumbani mwa watu katika Mitaa ya Bombambili, Mjimwema, Mfaranyaki, lizaboni na ile ya katikati Mjini hapa kama Mfaranyaki na Misufini bila Kusahau majengo.





Thursday, September 22, 2011

CHADEMA YAKACHA KUMSIMAMISHA MGOMBEA UMEYA!

Chama cha Upinzani kilichochukua Kata tano Muhimu kati ya 21 katika Manispaa ya Songea,CHADEMA kimekacha kumsimamisha Mgombea katika Uchaguzi wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Siku ya Ijumaa Septemba 23, mwaka huu kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mstahiki Meya Ali said Manya aliyefariki na Kuzikwa nyumbani kwake Lizaboni mjini hapa. Mheshimiwa Manya alikuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea baada ya Ushindi katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 2010 na kuchaguliwa kuwa Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Lizaboni.
Chama cha Mapinduzi CCM ndiyo pekee kimemteua Mheshimiwa Charles muhagama Diwani wa Kata ya Matogoro kugombea Nafasi hiyo muhimu. Hivi sasa Manispaa ya Songea ipo chini ya Naibu Meya Mariam Dizumba mheshimiwa Diwani Viti maalum. Juu pichani wanaonekana Mheshimiwa Charles Muhagama (kushoto) akiteta jambo nje ya Ukumbi wa Songea Club na aliyekuwa Mstahiki Meya wa Songea Mheshimiwa Ali Said Manya na Marehemu Adam Ngongi maarufu Mzee Yapenda ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya SOUWASA. Ilikuwa Julai 20, 2010 wakati wa kusaini Mkataba mkubwa wa kuendeleza Programu ya maji.

Thursday, September 8, 2011

He kumbe migogoro ya kumiliki mali ni kukosa mahusiano mema wakati wa kutafuta?


Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam,

KUTOKANA na migogoro mingi inayoibuka katika ngazi ya kaya na familia hapa nchini kutokana na kuwa na mahusiano mabaya katika kuzalisha na kumiliki mali, familia hizo zimetakiwa kujenga na kuboresha mahusiano yao kwa kufuata vigezo vya uwazi na upendo hatua kwa hatua kabla mali wanazozalisha hazijawatesa kwa kuwagombanisha kwa kile kinachodaiwa nani mmiliki halali kati ya mwanamke na mwanamume.
Hilo ni moja ya azimio lililofikiwa na washiriki wa warsha ya Uchumi na Ukombozi wa mwanamke kimapinduzi inayoendeshwa na Chuo cha Mafunzo ya Jinsia cha TGNP katika Ukumbi wa kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha dar es Salaam.
Katika hali ya kubaini tatizo kuu la wanandoa pia familia nyingi kusambaratika kutokana na migogoro ya nani amiliki mali, au kurithi wanawarsha hao wamechambua mbinu mbalimbali na kuja na mapendekezo ambayo huenda yakapunguza tatizo linalozikabili familia nyingi hapa nchini hasa kutokana na mfumo dume unamtenga mwanamke kumiliki mali hasa zenye thamani.
Sheikh wa wilaya ya Liwale, Adam Mpelengana, alisema ni muhimu kwa wanaume wote kutambua kuwa wanawake ni wasaidizi wa mwanamume na ni jukumu la mwanamume kumpenda na kufanyia haki anazostahili badala ya kumuachia kazi nyingi bila usaidizi.
"Mwanamke anatakiwa aenziwe apendwe kwa kila namna, haifai kuendekeza mila na desturi za kumtumikisha mwanamke,' alisisitiza Sheikh Mpelengana.
Awali Mchungaji wa KKT toka Shinyanga, Odorus Gyunda , alisema ni muhimu kubainisha wazi ukatili wanaofanyiwa wanawake ni kinyume cha mapenzi ya mungu.
"imeelezwa wazi kuwa Mwanaume ampende mke wake na mwanamke amtii mumewe," alisema na kubainisha kuwa hayo hayawezekani kama hakuna upendo na mawasiliano mema katika uzalishaji na taratibu zote za kuishi.
Hata hivyo wanawarsha hao wamependekeza kuwa ili kusiwe na migogoro katika matumizi ya fedha na umiliki wa mali ni vyema wenza wakashiriki kikamilifu maamuzi ya kupanga utafutaji wa fedha au mali hatua kwa hatua mapema.
jambo jingine lililoelezwa ni wanawake na wanaume kwenye kaya zinazotegemea kilimo wajue mahitaji yao ya chakula mapema wakati wa kuandaa mashamba ili wasije uza chakula chote kwa tamaa ya fedha.
Wakijadili suala la kudhibiti matumizi na kuweka kumbukumbu za mapato katika ngazi ya kaya washiriki hao wamependekeza kuwe na daftari la pamoja la kuwekea kumbukumbu za mapato na matumizi katika kila hatua.
Aidha wamewaasa wanawake kuwa makini na mchango wa nguvu kazi zao katika kuhudumia familia pia kuzalisha mali katika kaya na kuhoji matumizi na shughuli za kila mmoja katika kaya husika.
Vilevile imeelezwa wazi kuwa usafi na kujali afya za wanafamilia ni mtaji mkubwa katika kuleta mahusiano mema katika kutumia muda na kumiliki mali za kaya.
Washiriki hao hawakuishia hapo, walisema hayo yatawezekana iwapo, kutatengwa walao siku moja katika wiki kuzungumzia masuala na maendeleo ya kaya husika kwa kuwahusisha mume, mke na watoto ili kaya ziendeshwe kwa shughuli na bajeti zenye mtazamo wa kijinsia zaidi.
MWISHO

Wednesday, September 7, 2011

Migogoro ya ardhi ikome!


WALALAMIKIA MIGOGORO YA ARDHI KUKWAMISHA MAENDELEO

Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam
MIGOGORO ya Ardhi inayoendelea katika mikoa mbalmbali hapa nchini imetajwa kuwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya wanawake katika harakati zao za kujikwamua kiuchumi pia kuleta ukombozi wa mwanamke na maendeleo stahiki hapa nchini.
Hayo yameibuliwa na washiriki wa warsha inayoendelea katika Ukumbbi wa Kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa uwasilishaji wa mifumo na vikwazo vinavyozuia wanawake kujikwamua kiuchumi.
Akiwasilisha Mada hiyo, Mwezeshaji toka TGNP, Rehema Mwateba alisema ni vyema washiriki wakaeleza hali halisi ya umiliki wa ardhi na migogoro inayendelea kujitokeza hivi sasa ikilinganishwa na mifumo iliyopo katika kumkomboa mwanamke kimapinduzi.
Mshiriki mmojawapo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Morogoro,Kibena Kingo, ametolea mfano wa mapigano yanayoibuka marakwa mara na yanayoendelea wilayani kwake kati ya wafugaji na wakulima, ambapo chanzo kikiwa ni matumizi ya Ardhi na kwamba mgogoro huo ni mkubwa.
Imeelezwa wafugaji hao wanaotokea mikoa ya kaskazini na kati wanalishia wanyama wao mazao ya wakulima bila kujali na hivyo kuwakwaza wananchi wewnyeji ambao wengi wao ni wakulima wa mazao ya chakula.
"Mgogoro wa ardhi ni mkubwa na waathirika wakubwa ni wanawake na watoto, hata hivyo ni lazima hatua zichukuliwe ili kutatua migogoro hii kabla hayajatokea mauaji makubwa," alishauri Kingo.
Wakati kingo akielezea mgogoro wa ardhi Morogoro bado Mwezeshaji toka TGNP Darus Badi alipaza sauti yake na kuthibitisha kuwa mtandao huo una rekodi ya migogoro ipatayo 60 ya ardhi katika mkoa huo na kwamba kuna haja ya kulichukulia uzito tatizo hilo.
" Tuna migogoro tunayoijua kule Morogoro na tukiwa kama wanaharakati lazima tushirikiane kuchukua hatua," alisema Badi.
Naye Makamu Mwenyekiti wa halamashauri ya Mbinga Prisca haule alisema migogoro mingi ya ardhi huko Mbinga imeibuka kutokana na wakazi wa huko kutafuta maeneo ya kulima baada ya kuishiwa ardhi maeneo ya milimani.
"Kuna migogoro ya ardhi katika familia na nje ya familia kupigania ardhi ya kulima," alisema na kubainisha kuwa bado kuna mipango mibovu na sera isiyoeleweka katika umiliki wa ardhi.
Hata hivyo lawama azikuachwa kwa wawekezaji katika vitalu vya mbuga za wanyama hadi migodi ya madini kama ya Buzwagi, Geita hadi huko Namtumbo kwenye Urani( Uranium) ambako wananchi wa kawaida na hasa wanawake wanaona kama mchezo wa kuigiza wasijue kinachoendelea kwenye ardhi yao.
Lawama kibao zimeelekezwa pia kwa Mamlaka za vijiji na Miji kugawa ardhi kwa upendeleo na hasa kwa wale wanaotoa kitu kidogo kwaajili ya kupata viwanja vya makazi na kuwaacha kabisa wanawake nyuma.
Wakati wa Ufunguzi wa warsha hiyo, Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia ya TGNP, Dkt. Diana Mwiru, aliwaasa washiriki kujadili mada mbalimbali kwa lengo la kujenga uelewa na kusaidi jamii tunapoelekea kusherehekea tamasha la Jinsia na Mika 50 tangu Tanganyika kupata Uhuru wake.
Dkt. Mwiru,alisema, katika miaka 50 iliyopita wanawake wa nchi hii wameendelea kuachwa nyuma katika kumiliki na utoaji wa maamuzi juu ya rasilimali ikiwa ni pamoja na ardhi.
Mwisho