Friday, February 18, 2011

KINDAMBA NAMLIA MTANGAZAJI ANAYECHIPUKIA

Bw Kindamba Namlia (Pichani) Mtangazaji anayechipukia na kupendwa sana na wasikilizaji wa Jogoo FM- Songea Radio inayopasua mawimbi hadi Msumbiji. hata hivyo Kindamba naandika haya hapa chini kama wito kwako:
MIMI Kindamba naomba ushirikiano na wasikilizaji na wadau wa JOGOO FM- SONGEA Radio changa inayoleta changamoto za kimaendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni mkoani Ruvuma na mikoa ya jirani kama Mbeya, Njombe, Morogoro, Iringa na Katavi pia kule Rukwa bila kusahau Msumbiji.
utangazaji unachangamoto nyingi. naishukuru Blog ya Jamii ya wanaRuvuma kwa kazi nzuri.
Maneno hayo ni ya Kindamba alipofika Ofisini kwangu leo. nami nampa shavu kwa kibarua alichokianza hapa Songea.
(Juma NYumayo)

CHADEMA WALIPOTEMBELEA RUVUMA PRESS KUJENGA UHUSIANO

VIONGOZI wa CHADEMA wilaya ya Songea na MKOA wa RUVUMA wakiwa mbele ya Ofisi za RUVUMA PRESS CLUB wa kwanza na wa pili kushoto ni waandishi wa habari na watatu ni Diwani wa Majengo kupitia Chadema Mhe. Iddi Abdalah. Hawa wanajua wanachokifanya hasa baada ya kushinda kata 5 manispaa ya Songea na Kupata mgao wa Madiwani viti maalum wawili hao waliochuchumaa toka kulia Mhe Rhoda Komba na wa katikati anayeitwa Grace.

Mnara utakaozinduliwa waliponyongwa Mashujaa wa Majimaji

Nikiwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya maandalizi, Picha hiyo unayoiona tayari sasa kimekuwa kitu halisi. MNARA uliojengwa na VETA-Songea nyuma ya Ukumbi wa Songea Club pale waliponyongwa mababu zetu kupinga kutawaliwa na Wajerumani. Pamependeza kwelikweli. Mnara umebeba kinjenje, chibonga (Rungu) Mgoha (Mkuki) Chikopa (Ngao) na Juu kabisa Mwenge ishara ya nuru yenye matumaini. Nitakuletea unavyoonekana kama nilivyoupiga picha jioni leo.

Da siku nyingi sikuwepo hewani!

Hapa Juma Nyumayo Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club akimwelekeza jambo Kamanda wa polisi Mkoa wa Ruvuma Bw Michael Kamuhanda katika viwanja vya makumbusho ya taifa ya Majimaji Mjini Songea ambapo juma hili wageni kadhaa wenye hadhi tofauti watahudhuria maadhimisho ya Tamasha la kitaifa la Utalii wa Kiutamaduni katika mji wa Kishujaa na Kihistoria wa Songea. Tamasha hilo linakwenda sambamba na Kumbukizi za kunyongwa viongozi wa kingoni miaka zaidi ya 1oo iliyopita.

Saturday, January 8, 2011

MBWEMBWE ZA KU-PASS OUT MLALE JKT

OPERESHENI UZALENDO NI YA 100 toka kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa Mwaka 1963. Mkuu wa Kikosi cha 842 KJ Mlale JKT Songea mkoani Ruvuma, Major Abas Ahmed, aliwaambia wageni waalikwa na Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa habari Utamaduni Vijana na Michezo Dkt. Finella Mukangara kabla ya Kufunga Mafunzo ya awali ya Kijeshi yaliyochukua miezi 6 ya kuhenya ya Operesheni hiyo.
Kwa ujumla, Mlale JKT pamoja na Vikosi vingine huandaa vijana wasichana kwa wavulana na kuwafundisha utii, maadili mema pia mbinu za Kijeshi na stadi za kazi mbalimbali tayari kwa vijana hao kushiriki ujenzi wa taifa lao. Major Abas Ahmed anasema Operesheni UZALENDO ni ya aina yake na yenye kumbukumbu kubwa hapa nchini ambayo inaonesha hatua kubwa na kazi nzuri liliyofanywa na JKT katika kuandaa vijana wenye maadili mema ya kitanzania. faidi uhondo huu ambao haukumuacha kwenye kiti Naibu waziri wala Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenister Muhagama na wageni wengine kuingia uwanjani kulisakata rhumba la Bendi ya Mapipa ya Vijana hao wa Mlale JKT, Operesheni Uzalendo wakisaidiwa na Vijana wawili tu wa Operesheni Kilimo Kwanza kuyakung'uta mapipa hayo yaliyotoa muziki murua siku ya Tarehe 7/1/2011 mliopitia JKT mpo! (Picha zote na Maelezo na Juma Nyumayo)












































Sunday, October 31, 2010

Tunaendelea hivi Oktoba 31, 2010
















PILIKA ZA UCHAGUZI OKTOBA 31, 2010

Dr. Emmanuel Nchimbi mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini, akipiga kura yake leo saa 1:00 Asubuhi Kituo cha Kupigia Kura- Mateka Manispaa ya Songea kulia ni Msimamizi Msaidizi wa Kituo hicho, Gerwada Kapinga akitoa maelekezo.
Baadhi ya wapiga kura katika Kituo cha Shule ya Luhira Kata ya Mshangano, wakiwa katika Mstari wakisubiri kuingia kupiga Kura. Wakati huo huo Waandishi wa Habari wakitoa matangazo ya Mojakwamoja, Mwenye Suti ni Riporter wa Star TV na Redio Free Africa mkoani Ruvuma, Bw. Adam Mzuza Nindi na anayepiga picha hiyo ni Mpenda Mvula ambapo aliyepachika Camera begani akiwa katika mstari ni Muhidin Amri wa Majira.


Hiyo ni jana wakati kampeni za CCM siku ya mwisho kule Kiburang'oma Lizaboni, Manispaa ya Songea zikiwa zinafungwa rasmi, hapo juu na chini wapambe wakiwa makini kusikiliza sera na midundo ya muziki wa kizazi kipya kuipamba CCM na wagombea wake.














Foleni ya wapiga Kura bila kujali mwanamke au mwanaume eneo la Makumbusho ya Mashujaa ya Vita vya Majimaji Mahenge manispaa ya Songea leo saa 1:15 Asubuhi watu wameitika si mchezo.





Bw. Adam Mzuza Nindi, kwenye Kituo chake cha kupigia Kura Mjimwema Manispaa ya Songea akipokea maelekezo baada ya kukabidhi kitambulisho chake cha kupigia Kura leo majira ya Saa 5:45.