
Friday, February 18, 2011
CHADEMA WALIPOTEMBELEA RUVUMA PRESS KUJENGA UHUSIANO
VIONGOZI wa CHADEMA wilaya ya Songea na MKOA wa RUVUMA wakiwa mbele ya Ofisi za RUVUMA PRESS CLUB wa kwanza na wa pili kushoto ni waandishi wa habari na watatu ni Diwani wa Majengo kupitia Chadema Mhe. Iddi Abdalah. Hawa wanajua wanachokifanya hasa baada ya kushinda kata 5 manispaa ya Songea na Kupata mgao wa Madiwani viti maalum wawili hao waliochuchumaa toka kulia Mhe Rhoda Komba na wa katikati anayeitwa Grace. 

Mnara utakaozinduliwa waliponyongwa Mashujaa wa Majimaji
Nikiwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya maandalizi, Picha hiyo unayoiona tayari sasa kimekuwa kitu halisi. MNARA uliojengwa na VETA-Songea nyuma ya Ukumbi wa Songea Club pale waliponyongwa mababu zetu kupinga kutawaliwa na Wajerumani. Pamependeza kwelikweli. Mnara umebeba kinjenje, chibonga (Rungu) Mgoha (Mkuki) Chikopa (Ngao) na Juu kabisa Mwenge ishara ya nuru yenye matumaini. Nitakuletea unavyoonekana kama nilivyoupiga picha jioni leo.

Da siku nyingi sikuwepo hewani!
Hapa Juma Nyumayo Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club akimwelekeza jambo Kamanda wa polisi Mkoa wa Ruvuma Bw Michael Kamuhanda katika viwanja vya makumbusho ya taifa ya Majimaji Mjini Songea ambapo juma hili wageni kadhaa wenye hadhi tofauti watahudhuria maadhimisho ya Tamasha la kitaifa la Utalii wa Kiutamaduni katika mji wa Kishujaa na Kihistoria wa Songea. Tamasha hilo linakwenda sambamba na Kumbukizi za kunyongwa viongozi wa kingoni miaka zaidi ya 1oo iliyopita.


Saturday, January 8, 2011
MBWEMBWE ZA KU-PASS OUT MLALE JKT
OPERESHENI UZALENDO NI YA 100 toka kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa Mwaka 1963. Mkuu wa Kikosi cha 842 KJ Mlale JKT Songea mkoani Ruvuma, Major Abas Ahmed, aliwaambia wageni waalikwa na Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa habari Utamaduni Vijana na Michezo Dkt. Finella Mukangara kabla ya Kufunga Mafunzo ya awali ya Kijeshi yaliyochukua miezi 6 ya kuhenya ya Operesheni hiyo.
Kwa ujumla, Mlale JKT pamoja na Vikosi vingine huandaa vijana wasichana kwa wavulana na kuwafundisha utii, maadili mema pia mbinu za Kijeshi na stadi za kazi mbalimbali tayari kwa vijana hao kushiriki ujenzi wa taifa lao. Major Abas Ahmed anasema Operesheni UZALENDO ni ya aina yake na yenye kumbukumbu kubwa hapa nchini ambayo inaonesha hatua kubwa na kazi nzuri liliyofanywa na JKT katika kuandaa vijana wenye maadili mema ya kitanzania. faidi uhondo huu ambao haukumuacha kwenye kiti Naibu waziri wala Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenister Muhagama na wageni wengine kuingia uwanjani kulisakata rhumba la Bendi ya Mapipa ya Vijana hao wa Mlale JKT, Operesheni Uzalendo wakisaidiwa na Vijana wawili tu wa Operesheni Kilimo Kwanza kuyakung'uta mapipa hayo yaliyotoa muziki murua siku ya Tarehe 7/1/2011 mliopitia JKT mpo! (Picha zote na Maelezo na Juma Nyumayo)
Kwa ujumla, Mlale JKT pamoja na Vikosi vingine huandaa vijana wasichana kwa wavulana na kuwafundisha utii, maadili mema pia mbinu za Kijeshi na stadi za kazi mbalimbali tayari kwa vijana hao kushiriki ujenzi wa taifa lao. Major Abas Ahmed anasema Operesheni UZALENDO ni ya aina yake na yenye kumbukumbu kubwa hapa nchini ambayo inaonesha hatua kubwa na kazi nzuri liliyofanywa na JKT katika kuandaa vijana wenye maadili mema ya kitanzania. faidi uhondo huu ambao haukumuacha kwenye kiti Naibu waziri wala Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenister Muhagama na wageni wengine kuingia uwanjani kulisakata rhumba la Bendi ya Mapipa ya Vijana hao wa Mlale JKT, Operesheni Uzalendo wakisaidiwa na Vijana wawili tu wa Operesheni Kilimo Kwanza kuyakung'uta mapipa hayo yaliyotoa muziki murua siku ya Tarehe 7/1/2011 mliopitia JKT mpo! (Picha zote na Maelezo na Juma Nyumayo)
Sunday, October 31, 2010
PILIKA ZA UCHAGUZI OKTOBA 31, 2010
Dr. Emmanuel Nchimbi mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini, akipiga kura yake leo saa 1:00 Asubuhi Kituo cha Kupigia Kura- Mateka Manispaa ya Songea kulia ni Msimamizi Msaidizi wa Kituo hicho, Gerwada Kapinga akitoa maelekezo.

Baadhi ya wapiga kura katika Kituo cha Shule ya Luhira Kata ya Mshangano, wakiwa katika Mstari wakisubiri kuingia kupiga Kura. Wakati huo huo Waandishi wa Habari wakitoa matangazo ya Mojakwamoja, Mwenye Suti ni Riporter wa Star TV na Redio Free Africa mkoani Ruvuma, Bw. Adam Mzuza Nindi na anayepiga picha hiyo ni Mpenda Mvula ambapo aliyepachika Camera begani akiwa katika mstari ni Muhidin Amri wa Majira. 
Hiyo ni jana wakati kampeni za CCM siku ya mwisho kule Kiburang'oma Lizaboni, Manispaa ya Songea zikiwa zinafungwa rasmi, hapo juu na chini wapambe wakiwa makini kusikiliza sera na midundo ya muziki wa kizazi kipya kuipamba CCM na wagombea wake.

Hiyo ni jana wakati kampeni za CCM siku ya mwisho kule Kiburang'oma Lizaboni, Manispaa ya Songea zikiwa zinafungwa rasmi, hapo juu na chini wapambe wakiwa makini kusikiliza sera na midundo ya muziki wa kizazi kipya kuipamba CCM na wagombea wake.
Friday, October 29, 2010
Haya Dr Nchimbi na kampeni za mwishomwisho
Dr. Emanuel Nchimbi anayepungia mkono wananchi mara baada ya kuhutubia mkutano wake katika kata ya Bombambili Mtaa wa Miembeni akisindikizwa kwa maandamano makubwa yanayoashiria kuungwa mkono kwa CCm. Kata hiyo inakabiliwa na upinzani toka Chadema katiak kiti cha Udiwani ambapo mgombea wake Ken Moto anamtikisa mgombe toka CCM ambaye alikuwa Diwani awamu iliyopita Golden Sanga.

Mtoto huyo hapo juu jina lake halikuweza kufahamika mara moja akiangalia manjonjo ya Dr Nchimbi kumuombea Kura mgombea Udiwani Kata ya Bombambili Manispaa ya Songea Golden Sanga maarufu Sanga One wote ( awapo Pichani) chini toka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club Muhidin Amri na Katibu wa Mbunge huyo Andrew Chatwanga na dereva wao Jogoo eneo la Mjimwema Manispaa ya Songea
Sasa Kazi, Vijana wa IGP Mwema chini ya usimamizi wa Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda wakifuatilia matukio na kulinda usalama wa raia katika mikutano ya mwisho ya kampeni kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010 Siku ya Jumapili, hapa wakivinjari viwanja vya Samora kule kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea.


Sasa Kazi, Vijana wa IGP Mwema chini ya usimamizi wa Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda wakifuatilia matukio na kulinda usalama wa raia katika mikutano ya mwisho ya kampeni kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010 Siku ya Jumapili, hapa wakivinjari viwanja vya Samora kule kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea.

Mkurugenzi wa Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula nchini, Charles Walwa akistaajabu mahindi yaliyopo nje katika Ghala la wakala huyo lililopo Ruhuwiko Mjini Songea. Mkurugenzi huyo ametangaza nguvu nyingi kuelekezwa vijijini na kuwahakikishia wakulima na wafanyabiashara kununua kiasi chote cha mahindi hata baada ya Uchaguzi. hadi juzi tani 30,000 zimenunuliwa mkoani hapa na kiasi cha tani 20,000 zitanunuliwa kwa mpango mzuri zaidi.

Subscribe to:
Posts (Atom)









