Friday, September 21, 2012

Wazazi wawajibike kuwatunza wanafunzi waliomaliza Mitihani yao jana

Wazazi na walezi wa wanafunzi waliomaliza mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi hapa nchini jana (20/09/2012 wameombwa kuwalea kwa karibu watoto hao kimaadili wakiwa wanasubiri matokeo ya Mtihani huo muhimu.
Hayo yamesemwa na wanataaluma mbalimbali waliozungumza na mtandao huu wa www.ruvumapress.blogspot.com mjini Songea.
Wamesema licha ya wadau wa elimu kulaumu mtindo uliotumika wa kujibu maswali hata yale ya Hisabati kwa mtindo wa kuchagua, bado Elimu ya watoto hao ipo mikononi mwa wazazi na walezi.
Swala la Elimu bora au bora elimu sasa halina nafasi na kwamba ni muhimu kuitafuta elimu kwa kila namna.
Wanafunzi wengi  wanapomaliza mitihani yao huonekana wamemaliza elimu na kujikita kwenye shughuli ambazo hata umri wao haulingani.

Saturday, September 15, 2012

WIZARA YA ELIMU YATANGAZA MTIHANI KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2012



Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Kuhusu Mtihani Wa Kumaliza Elimu Ya Msingi Mwaka 2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI MWAKA 2012

JAMHURI2 YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI



Ndugu wananchi,
Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi Tanzania Bara utafanyika tarehe 19 na 20 Septemba, 2012. Jumla ya wanafunzi 894,881 wamesajiliwa kufanya mtihani huo ambapo wavulana ni 426,285 sawa na asilimia 47.64 na wasichana ni 468,596 sawa na asilimia 52.36.

Aidha, kati ya wanafunzi hao, wapo wanafunzi 874,379 watakaofanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili na wanafunzi 20,502 watafanya kwa lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo waliyoitumia kujifunzia.

Wanafunzi wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani ni 92 wakiwemo wavulana 53 na wasichana 39. Watahiniwa wenye uono hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 495, kati yao wavulana ni 238 na wasichana ni 257.Mtihani huu utafanyika kwa mara ya kwanza kwa kutumia teknolojia mpya ya ‘Optical Mark Reader’ (OMR), ambapo watahiniwa watatumia fomu maalum za OMR kujibia mtihani na majibu yao yatasahihishwa kwa kutumia kompyuta.

Masomo yatakayotahiniwa katika mtihani huo ni Kiswahili, English Language, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.

Ndugu wananchi,Maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, kusambazwa kwa fomu maalum za kujibia mtihani na nyaraka zote zinazohusu mtihani huo. Mafunzo maalum kwa ajili ya matumizi ya fomu za OMR yamefanyika kwa lengo la kuwaandaa watahiniwa, wasimamizi pamoja na viongozi wa elimu katika ngazi mbalimbali ili waweze kutumia ipasavyo teknolojia hiyo.

Ndugu wananchi,Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi ni muhimu kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla kwa kuwa unahitimisha ngazi ya Elimu ya Msingi na kufungua milango kwa ajili ya elimu ya sekondari.

Hivyo, matokeo ya mtihani huu hutumika katika uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na Elimu ya Sekondari.

Kwa kuzingatia umuhimu wa mtihani huo, napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa Maafisa Elimu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa mazingira yanakuwa salama na tulivu na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha udanganyifu.Napenda pia kutoa wito kwa wasimamizi wa mitihani kufanya kazi yao ya kusimamia kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu. Wapo baadhi ya wasimamizi ambao wamekuwa wakishiriki katika kuwasaidia watahiniwa kufanya udanganyifu kwenye mitihani.

Napenda kuwaasa tena wasimamizi kujiepusha na vitendo hivyo vya udanganyifu kwani serikali haitasita kuchukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote atakayebainika kukiuka taratibu za mitihani.

Kwa upande wa wanafunzi watakaofanya mtihani mwaka huu, ninaamini kuwa walimu wamewaandaa vizuri katika kipindi chote cha miaka saba ya Elimu ya Msingi. Hivyo, ni matarajio yangu kuwa mtaufanya mtihani huo kwa utulivu na kuzingatia taratibu zote za mitihani ili matokeo ya mtihani yaoneshe uwezo wenu halisi kulingana na maarifa na ujuzi mliopata katika Elimu ya Msingi. Serikali inawaasa wanafunzi wote kutojihusisha na vitendo vyovyote vya udanganyifu katika mtihani kwani watakaobainika watafutiwa matokeo yao yote ya mtihani. Ndugu wananchi,

Natoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kuhakikisha kwamba mtihani huo unafanyika kwa amani na utulivu wa kutosha bila usumbufu unaoweza kusababishwa na shughuli za kijamii hasa katika maeneo ya jirani na shule.

Mwisho, napenda kuwaasa tena wanafunzi, walimu na wananchi wote kwa ujumla kujiepusha na vitendo vya udanganyifu wa aina yoyote katika Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi.

Nawaomba pia raia wema wasisite kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapoona au kuhisi mtu au kikundi cha watu kinajihusisha na udanganyifu wa aina yoyote katika mtihani huo.Nawatakia watahiniwa wote heri na fanaka katika mtihani utakaofanyika tarehe 19 na 20 Septemba, 2012.

MHESHIMIWA PHILIPO AUGUSTINO MULUGO (MB) NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI15 SEPTEMBA, 2012

Jua Kali hadi mifukoni hapa Songea



Hakika hali ya uchumi hapa Songea waweza kuiona sehemu za masoko na hasa katika vitoweo.


"...jua kali hadi mifukoni." Wengi wanalia.

Hapa nilikuwa napita mitaa mbalimbali nikatokea eneo la Soko kuu la Songea pale wanawake wanapouza samaki wa kutoka Ziwa Nyasa ambalo linamzozo wa Mpaka Kati ya Tanzania na Malawi,

Samaki aina ya Mbasa, Mbufu, Mbelele na dagaa wale wadogo wa dogo na wakubwa ni maarufu sana, wanauzwa chini tu bila kujali, (Picha inajieleza)

Watamu, wanapendwa.

Nilisimamisha Gari eneo la Magharibi ya Soko Kuu la Songea amabako kuna mlango mdogo wa kutokea maarufu kwa kuuza samaki na dagaa kwa muda wa nusu saa sikuona mteja kuulizia samaki hao, Mama aliyekuwa akiuza kajifunika tu na Mwamvuli.

Mifuko ya wanunuzi nayo imepigwa na jua.

Haina miamvuli .

DMI wafanya maandamano kuadhimisha siku yao Songea

Shirika la Masista wa DMI, limefanya maandamano makubwa na maonyesho ya Bidhaa mbalmbali mkoani Ruvuma kuadhimisha siku yao hapa nchini.
Masista hao wa madhehebu ya Katoliki wanaojishughulisha na maendeleo ya wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum katika nchi kadhaa barani Asia, Afrika na kwengineko,walifanya maandamano hayo katika mitaaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupita katika Barabara ya Sokoine eneo la Soko la Songea mjini, Ukumbi wa Manispaa Songea na kuishia Viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ambako mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu, aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti, aliyapokea maandamano hayo, kukagua maonesho na kuwahutubia. Jambo jema ni mabango yaliyobebwa na waandamanaji yaliyodai wtoto yatima kupewa elimu, chakula na kusikilizwa. (Picha zote, Maelezo na Juma Nyumayo)


























ZM Mwanamuziki anayetamba Ruvuma arejea toka Dar



Kijana machachari katika kuimba, Zuberi Mohamedi, Maarufu kama ZM, Mwanamuziki wa kizazi kipya anayetamba kwa vibao vikali mkoani Ruvuma (Pichani Kulia ) akiwa na rafiki yake S. Komba ,wakitokea Kituo cha Redio Jogoo mjini Songea kuwafahamisha wapenzi wao kuwa amerejea toka Dar alikokwenda kujifua na kujinoa hadi kuachia Single moja akiwa na nguli wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature.

Hapo akiwa mitaa ya Soko kuu Mjini Songea karibu na NBC Bank Jengo hilo Jeupe kushoto, alipokutana nami akifanya mipango ya kwenda Madaba kusuuza nyoyo za wapenzi wake baada ya kupotea kitambo.

ZM alinishukuru kwakuwa nilimsaidia kumrusha katika Kituo cha TV Tunduru kwa mara ya kwanza na watu kumuona kwenye runinga tangu azaliwe. hayo yalifanyika wakati alipoanza muziki huo miaka ya 2000 mwanzoni. (Picha na Juma Nyumayo)

Wednesday, September 12, 2012

Ni haki Watoto wa Wakulima na wafanyakazi kuua?




PICHA NO Na 2:Baadhi ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Ruvuma, (Kuanzia kushoto) Nathan Mtega wa Radio One, Amon Mtega wa Jamboleo, Joseph Mwambije wa Majira na Muhidin Amri wa HabariLeo wakiangalia Picha ya mabaki ya aliyekuwa Mwandishi wa habari wa ChannelTen, Daud Mwangosi aliyeuawa kwa bomu huko Nyololo Iringa. Tukio hili walilifanya Tarehe 11, Septemba 2012, kabla ya Maandamano ya waandishi mkoani hapa kugonga Mwamba kutokana na sintofahamu ya Viongozi wa Ruvuma Press Club na wasaidizi wao kukosa mawasiliano na Waaandishi wenzao.


PICHA ya Kwanza: Baadhi ya wandishi wakiwa nje ya Ofisi ya Mwakilishi wa Radio One mkoani Ruvuma wakisubiri Maelekezo ya Maandamano ambayo hayakufanyika.


Picha ya Tatu: Askari waliomsulubu Mwangois hadi kumuua kwa Bomu na Kumjeruhi Mkubwa wao ambaye amenyosha fimbo juu.




Wote hao juu ni watoto wa wakulima na wafanyakazi wa nchi hii hakuna mwenyehaki ya kumuua mwenzie hasa wawapo kazini wakitafuta ridhiki kwa njia halali.




























Mtuhumiwa afikishwa Mahakamani, Mkono wa Sheria, haujali Bomu.

Vilio, Simanzi, Maandamano ya wanahabari na wadau wao huenda yakapozwa na hatua ya Mtu anayetuhumiwa kumuua Daud Mwangosi aliyekuwa mwandishi wa Habari wa ChannelTen na Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa Habari mkoa wa Iringa, Tarehe 2, Septemba 2012 kufikishwa mahakamani.

Si Mwingine ni huyo hapo aliyejifunika kichwa chake. Aibu. Ni Aibu kwake.
Bado Jamii ya watanzania wanataka wale waliomtuma kufanya hivyo kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Mkono wa Sheria haujali Bomu.
Unajali ukweli ili utende haki.
(Picha kwa Hisani ya Blogu ya www.francisgodwin.blogspot.com









Tuesday, September 11, 2012

Maandamano waandishi yagonga mwamba Ruvuma



Na Gideon Mwakanosya na Nathan Mtega ,Songea

MGOGORO mkubwa umeibika kwa waandishi wa habari mkoani Ruvuma baada ya Viongozi wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo kutoitisha maandamano na kuingia mafichoni kwa muda ili kuepusha kufanyika maandamano ya kuunga mkono maombolezo ya kifo cha mwandishi wa habari na aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa Daud Mwangosi aliyefariki kwa kupigwa na mlipuko uliosababishwa na polisi katika kijiji cha Nyololo mkoani Iringa.

Mgogoro huo umewagawa waandishi wa habari na kuwafanya baadhi ya waandishi kutishia kujitoa nafasi zao za uongozi na uanachama.

Waandishi wa habari mkoani Ruvuma walianza kwa walishangazwa na hatua ya viongozi wa ngazi ya juu ya chama hicho kutowajulisha muda na njia zitakazotumika kwa maandamano hayo hadi pale kwa njia ya simu na baadhi ya waandishi wa habari ambao walishapanga waandamane saa 10. Jioni baada ya kujihakikishia kuwa viongozi wao wamewatosa nan hawana ajenda muhimu ya kupinga m,aandamano hayo kwa hula.

Awali baadhi ya waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali ambao ni wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo (RPC) walijikusanya pamoja na kufuatilia matangazo ya vyombo mbali mbali vya habari yaliyokuwa yakiendelea huku wakiangalia baadhi ya picha zilizopigwa wakati na baada ya kifo cha mwandishi huyo wa habari ambaye alipatwa na mauti wakati akiwa kazini na walipanga wandamane saa 10 jioni muda ambao ndio Marehemu Mwangosi aliuuawa kinyama kupigwa na bomu na Polisi.

Katibu Msaidizi was Chama cha wqaandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma , Julius Konala, alionyesha ushirikiano mkubwa kwa wanachama ambao muda wote walikuwa wanadai rauba na hatua iliyofikiwa na viongozi wa chama hicho kwaqajili yua maandamano na kuwajulisha kuwa viongozi wake hawajulikani waliko na wanapinga kufanyika kwa mnaandamano hayo.

“Jamani mimi mtanionea tuu, Mwenyekiti na katubu wamesema kuwa UTPC imeyasimamisha maandamano yetu bila kutaja sababu,” alisema Konala ambaye alichukua hatua ya kuwasiliana na viongozi wa polisi mkoani hapa waliotaka kujua ni njia zipi zitakazotumiak katiak maandamano hayo ili walete askari waq kuyalinda maandamano hayo ya amani.

Tukio hilo limewakasirisha sana viongozi wa Chama hicho na kulazimika kuitisha mkutano wa dharura kwa baadshi ya wanachjama wengi wao wakiwa ni mamluki na kusababisha viongozi hao kuomba radhi kwamba wamekosa mawasiliano nao na baadhi ya wanachama wametushia kujiuzulu akuwemo katibu msaidizi Julius Konala kwa madai kwamba chama hicho kimeingiliwa na mikono ya wanasiasa.
“naona mbele yangu kuna wingu kubwa ambalo mwisho wake siujui, nafikiria kujiuzulu uongozi na kujitoa kataika chama, “ alisema Konala.

Baadhi ya wadau wa habari mkoani humo wamenesha kushangazwa na ukimya wa wanahabari wa mkoa huo liocha ya wanahabari wote nchini wakionekasna kwenye runinga wakiandamana kupinga ukatili huo iliofanywa dhidi ya Mwandishi wa habari akiwa kazini.

Hata hivyo Mkurugenzi wa muungano wa Vyama vya waandishi wa habari nchini UTPC Abubakar Karsan akiongea na Nipashe kwa njia ya Simu amekanusha vikali kwamba wao walitoa maelekezo kwa Ruvuma Press Club kwamba wasiandamane kwa madai kuwa viongozi hao waliwajulisha kuwa maandamano hayo yatatekwa na CHADEMA.
Mwisho

Monday, September 10, 2012

Nitakulilia daima, ukatili huuhukufanyiwa wewe tumefanyiwa sisi



Samahani kwa kuweka Masalia ya Mwili wa Daud Mwangosi, Mwandishi wa habari wa Channel Ten aliyeuawa kikaqtili baada ya kulipuliwa na Bomu mikonon mwa Polisi. Tutamlilia, machozi yetu yamwgilie mbegu za upendo kwa Polisi wa Tanzania pamoja na viongozi wanaowatuma kutekeleza unyama kwa raia wanaotakiwa kuwalinda.Mwangosi tunakulilia wenzio, najua hutusijii, wakatili wako wanatusikia wanatuona na kesho watatuona tukiandamana. Si kwaajili yako ni kwaajili yetu, watoto wetu na wao pia

Starehe kwa Amani Mwangosi, Msiba wako ni maumivu makubwa na mateso makubwa kwa taifa hili.

Mandamano ya Waandishi Ruvuma

Habari za kuandamana kwa waandishi wa Habari nchi nzima zimepokelewa na wadau wa habari kwa hisia tofauti mkoani Ruvuma.
Wadau kadhaa waliozungumza na Blogu hii wameunga mkono hatua za waandishi kujitetea dhidi ya nguvu kubwa, ukatili, uonevu na dharau ya kazi za wanahabari wawapo kazini hasa pale wanapowapiga, kunyng'anya vifaa vyao vya kazi na vunjajungu pale alipouawa kinyama Mwandishi wa TV ChannelTen Mkoani Iringa Bwana Daud Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Club ya Waandishi mkoni humo (IPC) kwa kulipuliwa na Bomu akiwa mikononi mwa Polisi ambao walikuwa na wajibu wa Kulinda uhai wake.



PICHA: Waandishi wa Habari wakiwa Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu wakipat hbari za maendeleo ya mkoa huo ili kuhabarisha umma hivi Karibuni


PICHA WALIOPO NA GARI NA MITAMBO: Waandishi wa TBC1 wakiunganisha matangazo ya nje wakati wa Sherehe za Eid El Fitr mara baada ya Kumaliza Mfungo wa mwezi wa Ramadhani Agosti, 2012. Je ni uungwana waandishi hawa kuwatesa, kuwadharau kuwanyanyasa na hata kuwauwa kwa kuwalipua na mabomu kama walivyofanya polisi kumuua kikatili Daud Mwangosi wa Iringa????????PICHA