Wednesday, September 29, 2010

Mahafali kidato cha nne Sekondari ya Msamala

Mama anapomzawadia bint yake akiwa amehitimu zsafari ya miaka 4. pichani Amina Nyumayo aliyekuwa anasoma sekondari ya Msamala manispaa ya Songea akipokea zawadi toka kwa mama yake Mzazi wakati wa mahafali ya sita ya Shule hiyo wiki iliyopita. (Picha na Maelezo na juma Nyumayo)

Monday, September 20, 2010

Unapajua hapo?




Wakati wa kampeni raha kama nini, je baada ya uchaguzi watapita humo. Hapa ni Mto Ruhuhu Mkoani Ruvuma na JK akishuka katika ardhi ya Mbeya Vijijini (Picha zote kwa hisani ya http://www.kalulunga.blogspot.com/)

Mambo ya Gemsat Kurasini!

Heheheee! Nimekutana na waandishi kibao toka Zanzibar tulikuwa Ali Othman na Haroub Hussein kule Tanga tulikuwa na Anna Makange pamoja na wengine wengine.

Saturday, September 18, 2010

Dorothy Mbilinyi wa TGNP ndani ya RUVUMA

Mama Dorothy Mbilinyi, (aliyekaa katikati) kaanza kazi mara moja kwa kueleza nini anatarajia kufanya katika mafunzo ya jinsia na Demokrasia hapa Ruvuma, katika picha anaonekana akihesabu point za kusisitiza kwa viongozi wa Dini mbalimbali na Mashirika yasiyo ya kiserikali. Wengine waliosimama Ni Steve Chindiye wa Ruvuma Press, Juma Nyumayo wa RUNECISO Fatuma Lazaro wa UDSM na Elizabeth Mbena wa UDSM aliyekaa kulia kabisa ni Judith Lugoye.
Mpiga Picha wa Gazeti la Mtanzania Bw Muhidin Sufiana (Kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma Juma Nyumayo baada ya kutembelea ofisi za Chama cha Waandishi wa habari mkoani hapa, hivi karibuni. wenginme ni happy Katabazi wa Tanzania daima na Editha Karlo wa Mtanzania.


Prof. Ibrahim Lipumba wa CUF Mgombea Urais Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010 akitoa sera kwa wananchi katika ngome ya CHADEMA viwanja vya stendi ya malori Majengo Manispaa ya Songea.
Picha nyingine baadhi ya watoto na watu wazima waliofika katika viwanja hivyo kusikiliza sera za CUF. (Picha zote na Muhidin Amri- Ndolanga)






Friday, September 17, 2010

JIONEE MWENYEWE MAMBO YALIVYO

Mama Lishe wa Manispaa ya Songea ambaye jina lake halikuweza kufahamika mala moja akimlisha chakula Mtoto wake.

Muuza samaki wa bichi kutoka Ziwa Nyasa akitembeza Samaki hao kwa nia ya kuboresha Lishe za wateja wake.


Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Eliza Mbena na Fatuma Lazaro wakivishana Vitambaa vya Chama Tawala CCM
Kijana akipata Chakula kutoka kwa mama Lishe katika eneo la Standi ya Mabasi katika Manispaa ya Songea