Monday, July 12, 2010

Wanafunzi wa UDOM katika Mazoezi Ruvuma Press!


Wanafunzi hawa wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakishauriana jambo katika Ofisi ya Mwenyekiti wa Ruvuma Press Club ambako wamepangiwa kufanya mazoezi kwa vitendo, Deogratias Ponera (Kulia) akimwelekeza jambo Englebert Nchimbi ambaye anamsikiliza kwa makini. Vijana hawa watakuwa katika shughuli hiyo kwa wiki tatu na baadaye kurejea chuoni kwao Dodoma. Chuo cha dodoma kinategemewa kudahili wanafunzi wengi zaidi kuliko chuo kingine chochote eneo la Afrika Mashariki na kati katika miaka michache ijayo.
(Picha na Juma Nyumayo)